Wednesday

Nguzo 5 za uhusiano bora wa Kimapenzi!


Nakumbuka zamani nilipokuwa mdogo, kulikuwa na akina mama ambao walikuwa wakijadili mambo yao ya kimapenzi kila wanapokutana pale kibarazani (mbele ya nyumba) mida ya jioni mida ya jioni wakichambua mchele au kumenya viazi tayari kwa mlo wa jioni.
Wamama hao walikuwa wakijadili mambo mengi sana ila moja ninalokumbuka ni kuwa "ili usiachike ni lazima umpe mumeo kila akitaka, umpikie mapocho-pocho, uwe msafi, umuwekee maji bafuni na kumkogesha, umkande miguu na kupenda ndugu zake".

Kutokana na maisha ya sasa kwa wengi wetu ukiachilia mbali kuwahi kuangalia Isidingo (Tv 4 u) kufanya hayo niliyoyataja inakuwa mbinde kidogo kwa vile tunafanya kazi nyingine ili kuchangia kipato ktk familia zetu na unaporudi nyumbani unakuwa umejichokea, sana sana utafanya moja kati ya hayo si unajua tena mambo fulani (mwenzi mtukufu mwee!).

Alafu ndugu wa mpenzi/mumeo huitaji kuwapenda unapaswa kuwaheshimu au kuwaonyesha heshima tu, kumpenda kijana wao isiwe taabu kha!

Tuachane na hayo basi, tuendelee.....Mimi kama Dinah naamini kuwa haijalishi unapesa kiasi gani, "libido" iko juu kiasi gani, Umzuri au Umrembo kiasi gani, "mnato au mdebwedo", unampenda jinsi gani au unatabia njema kiasi gani ktk uhusiano wako wa kimapenzi kama hakuna hizi kitu 5, nenda shule kajifunze!

1-Ushirikiano
2-Masikilizano na Maelewano
3-Heshima
4-Mawasiliano (angalia picha)
5-Kujali

Hayo mambo matano yanavipengele ambavyo vingine viko wazi sana na sitoweza kuviweka hapa kwa vile watu tumefunga.

Nakaribisha mchango, maoni, maswali na nyongeza ktk hili.

Msikilize Dada Stara

Ty.

No comments:

Pages