Sunday

Tekinolojia na mapenzi inaendelea hapa.....

Sote tunatambua kuwa mahusiano yamekuwa yakivunjika mara kwa mara, ndoa hazidumu kama ilivyokuwa miaka 40 iliyopita na kama ndoa/uhisiano huo umedumu basi ujue asilimia kubwa ni uvumilivu wa mmoja wao kwa vile kuna watoto ndani ya uhusiano huo na mara zote mvumilivu huyo huwa na uhusiano mwingine nje.

Uhusiano huo unaweza ukawa wa kimwili (mambo ya kimada, nyumba ndogo na vipoozeo), uhusiano wa kihisia tu ambao mara nyingi huitaji kuonana na mwenza wako na huu ni ule wa kimtandao a.k.a internet, uhusiano wa kimapenzi wa simu kwa kutumia sms na ule wa kuongea kwa sauti.

Nitazungumzia mahusiano ya kimapenzi ambayo ni matunda ya Teknolojia kila uhusiano kwa nafasi ili kukusaidia wewe kuelewa na kutoa maoni au kuongezea yale niliyoyaelezea.

Mtandao a.k.a Internet.
Mtandao umekuwa sehemu kuwa ya maisha yetu hivi sasa, wengi wetu tunatumia muda mwingi kukaa mbele ya Komputa kuliko ule mda tunaotumia kukaa na wapenzi wetu.

Kwa baadhi ya wenza (couple) hujitahidi kujigawa ili mwenza wake asijisikie vibaya au kuhisi anatengwa au kutojaliwa na hivyo wapenzi hao huamua kutembelea tovuti tofauti usiku wa manene wakati wapenzi wao wamelala au ilemida ambayo wanamaliza kazi au wako kazini nakisingizio ni kuwa kuna kazi au Data wanapaswa kuzimalizia na zinahitaji uchunguzi "online".

Hapa inaweza ikawa muhusika (mwenza) akawa anatembelea chat rooms, Forums, Emails(sio zote za kikazi), kutembelea Tovuti za Porno au kama sio zile za kutafuta jamaa mliosoma pamoja, marafiki n.k.

Simu za mkononi.....sms!
Mpenzi hapa anatumia muda mwingi kutuma na kusoma sms kutoka kwa watu tofauti na baadhi huwa ni wapenzi ambapo hubandikwa majina yakiume ikiwa muhusiaka na mwanaume na kupewa majina ya kike ikiwa mhusika ni mwanaume.

Simu za mkononi-kuongea!
Mpenzi anatumia muda mwingi kuongea kwenye simu kuliko muda anaotumia kuongea au kufanya mambo mengine yanayohusiasha uhusiano wenu wa kimapenzi.

Tekinolojia hii pia inahusisha swala la kutembelea Gym, Salon......zamani hakukua na haya mambo sio, ila siku hizi utakuta bwana au bibi atumia muda mwingi kwenye kona hizo kuliko ule anaotumia na mwenza wake.

Natambua nimegusa wengi hapa.............karibu tujadili kuhusu hili, tufanye nini ili kuokoa mahusiano yetu ya kimapenzi na wakati huohuo kufaidi matunda ya Teknolojia?

Karibu sana.........

No comments:

Pages