Tuesday

D'hicious.....a Year on!



Shukurani za dhati kwako wewe msomaji kwa ushirikiano wako, Rafiki zangu wote walioiweka D'hicious kwenye site zao kwa moyo mkunjufu na wenye furaha nasema Mungu awabariki sana kwa kuthamini mchango wangu ktk jamii ya Kitanzania "mtandaoni".

Katika safari hii ya miezi 12 nimekumbana na vishawishi vingi as you can imagine, nimekutana na kutengeneza mafariki wengi kutoka sehemu mbali mbali za Dunia, nimejifunza mengi kutoka kwa watu wengine na hata kukabiliana na "bullies".

Nisingekuwa nakiburi cha kuvuka miezi 12 na kusema nilichokisema leo hii bila ya Rafiki yangu mpenzi na wa Siku nyingi, Geeque aambae mimi huwa napenda kumuita "Jiikyuu" au GQ ambae siku zote usiku na mchana alikuwa pale kwa ajili yangu, huyu bwana ni kimbilio, nguzo na shujaa ktk maisha yangu "mtandaoni" ambayo time to time nilikuwa napata wakati mgumu kutokana na vitisho, abuse na vishawishi.

GQ unaja kabisa kuwa bila wewe D'hicious ingekuwa hadithi.......Asante kwa yote na Mungu akubariki sana.


No comments:

Pages