Friday

Hatubadiliki bali tunakua/pevuka

Sote huwa tunasikia kama sio wewe unauzoefu tayari wa kulalamikiwa na mpenzi kuwa tumebadilika. Utasikia mkizozana kidogo mwenza wako anasema "siku hizi umebadilika sana, zamani hukuwa hivi" anaweza hata akakupa mifano hai lakini wewe unaweza ukabisha kwa nguvu zote na kushangaa au kujiuliza umebadilika nini? Mbona uko vilevile tu kitabia na kimuonekanao.


Lakini katk hali halisi huwa kuna kuwa na mabadiliko makubwa sana(ukuaji), wewe huyaoni kwavile ni sehemu ya ukuaji wako hivyo unabadilika automatically bila wewe kutambua. Ukiangalia nyuma ulipokuwa teen ni tofauti na sasa ambapo uko kwenye early 20s na unapofikia late 20s utakuwa na tabia tofauti na hapo awali hali kadhalika unapofikia miaka 30, 40 na kuendelea.


Wenza wengi hugombana na kutofautiana kwenye mahusiano ya kimapenzi kwa vile huwa wanategemea wapenzi wao waendelee kuwa vilevile walivyo kutana nao miaka 6 au 15 iliyopita. Hawajui kuwa inategemea zaidi umekutana nae akiwa na umri gani, ukikutana na mpenzi yuko kwenye late 20s au early 30s huwa hakuna mabadiliko......lakini kama ulioa/olewa nyote mkiwa watoto au mmoja wenu ni chini ya miaka 27 basi mimi hapo wala sina la kuongeza!

Huu ndio ukweli wa Ijumaa ya leo? Unanyongeza? basi nafasi ni yako.....

Mwisho mzuri wa wiki. XXX

No comments:

Pages