Monday

Mam'mkwe hanipendi je niolewe?...Ushauri

kelly said..."Habarini za saa hizi wadau wote wa dinah.... mimi jamani nina jambo linanitatiza ningependa dinah na wadau wengine mnisaidie, kama nimetoka nje ya mada basi mnisamehe bure.... mimi nina mchumba uhusiano wetu mpk leo unamiaka minne,mwaka wa tatu nilivalishwa pete sasa tatizo ni kuwa mchumba wangu hataki nionane na mama yake kwa madai mama yake mkorofi ila ndugu wengine wote nawajua nawananijua na wanataka tuoane hata kesho,kwetu pia anajulikana.

Yeye anaishi kwao na mimi naishi kwetu na kila siku tunaonana na weekend tunashinda wote.... ila linapokuja swala la mama yake yupo sehemu fulani basi hatutaenda hiyo sehemu ili tu nisionane na mama yake.... sasa wadau kama jamaa anataka niwe mkewe itakuwaje hapo?


Nilishaambiwa na wifi zangu kuwa mama yake hanipendi,na yeye ndio kipenzi cha mama yake,siku moja nilimwambia kama mama yako akikataa tusioane itakuwaje akasema ooh atake asitake mimi nikishajipanga nakuoa yeye shauri yake.

Kwa upande wangu mimi sitaki kuoana nae kama mzazi wake huyo hatokuwa radhi na pia sikotayari kumpoteza kwa vile nampenda sana..... wadau na dinah naomba msaada wenu wa mawazo kama nitakuwa sijaeleweka niulizeni nitawafafanulia pale ambapo hamjanielewa nawapenda wadau wote wa dinah "

No comments:

Pages