Thursday

Utachumbiwa lini.......? Make him(II)

White Gold & Diamond!
4-Ni mwiko kuwa tegemezi, hakikisha unafanya kila uwezalo kuonyesha kuwa unaweza kufanya mambo yako kivyako bila kuomba-omba (vibomu) unless umekwama kweli kweli yaani malipo yamechelewa au biashara hajaenda vema mwezi huu na mwenye nyumba anatishia kukuweka nje, hakikisha tukio hilo halijirudii mara kwa mara.

Kumbuka kuzungumzia malengo yako ya baadae (sio ndoa) malengo yako kimaisha kwamba ungependa unatafuta kiwanja ili ujenge nyumba hata ya chumba kimoja Mungu akikujaalia, ungependa kununua shamba mahali na kufanya kilimo cha mboga-mboga n.k.

Sahau au usithubutu mambo ya kisistaduu uchwara ya ningependa kufungua duka la kuuza nguo, kufanya pati kubwa ya kuzaliwa kwangu au kununua Prado.....haitosaidia kwani ni kama vile unamwambia akupe mtaji.....zungumzia vitu vikubwa vya kudumu.....atakuona una akili ya kimaendeleo na unafaa kua wa milele Daima.


Sisemi kuwa usipokee zawadi au "mshiko" aki-offer si kajitolea bwana.....hiyo bomba lakini kale ka mchezo ka' kumfanya mpenzi wako kitega uchumi sio njema kwani kila mtu anamajukumu yake ujue! Mwanaume akionakuwa unaweza kujitegemea bila kuwa na kiburi (uswawa kwa sana)anakuwa na uhakika na maisha yenu ya baadae kama familia, na hivyo kusogeza swala la ichumbana ndoa karibu zaidi kuliko alivyopanga kuwa mpaka ajenge nyumba, kumiliki biashara kubwa n.k.


Kwani atajua wazi kuwa mtashirikiana na kufanikisha mambo haraka zaidi ikiwa mko pamoja kama mke na mume......ni kweli ukiwa mwenyewe kufikia malengo inachukua muda mrefu sana (kutokana na uzoefu wangu) lakini mkiwa wawili ktk ndoa malengo yanafikiwa chap-chap....kumbuka usemi usemao umoja ni nguvu na...........!

Hivyo mwanamke usibweteke fanya bidii ktk shughuli zako na onyesha kuwa unaweza kuweka tofauti ktk maisha yenu (ikiwa mtafunga ndoa) hali itakayomvuta mpenzi kutangaza ndoa.


5-Kamwe narudia tena kwamwe usiruhusu amalizie manii yake ndani hakikisha na ni mwiko kutumia madawa ya kuzuia mimba (kisa cha kubadili mwili/maumbile yako) kwa mwanaume ambae hajakuchumbia, hakikisha manatumia "condom".....Kwanza hurushisiwi kabisa kufanya ngono lakini kutokanana mfumo wa maisha wa sasa, wadada tunabaki shuleni kwa muda mrefu tofauti na miaka ile na kuizuia nature inakuwa ngumu hivyo inabidi tu ufanye ngono nje ya ndoa.

Sasa kama huruhusiwi kufanya Ngono b4 ndoa kwanini unamruhusu mwanaume akumwagie ndani wakati unajua kabisa uhusiano wenu sio "commited" kwa sasa....nina maana hakuna pete ya uchumba? Ukimimbika je?Kumbuka unafanya ngono kabla ya ndoa ili kufurahisha mwili na sio kujenga familia (which is the Main reason ya kukutanisha miili yetu kwamujibu wa Sayansi na Dini)......kama anakupenda kweli, yaani kafika mwisho wa Reli lakini unamzuia kumalizia ndani ni wazi kuwa ataharakisha mambo ya kutangaza ndoa ili apate uhuru.......wenyewe wanasema "kumiliki mwili wako nje na ndani".


Baada ya kufanya yote haya na mengine ya kumfurahsiha na kumridhisha kitandani na nje ya kitanda ktk mwaka mmoja na bado hajatangaza ndoa? Aaaah lazima kuna kipengele nimekiacha, sasa hebu niambie mpenzi wako anapenda nini zaidi yaani kama vipi anaweza hata ngono akaiweka pembeni ili amalize anachokipenda na ikiwa hakijaenda alivyotaka basi ngono inakuwa "out of the window".

Nikipata majibu yako then nitakupa Mbinu ya mwisho (nitaweka ktk mtindo wa Polls kulia kwa site hii) na baada ya hii (mbinu ya mwisho) ndoa haijatangazwa basi no matter how much you love the guy ujue you are not enough to be his wife acha kupoteza muda, tafuta ustaarabu mwingine, maisha mafupi atii!

Kila la kheri.

No comments:

Pages