Saturday

Tangu nimeachana na wangu, sitaki Demu-Ushauri!

"Eti dinah wewe ni profesheno kwenye mambo ya LOVE???mi namatatizo kichizi ya kisaikolojia ,Tangu niachane na chick wangu feb 2007 mpaka leo sitaki demu na wala sijisikii kabisa kuwa na uhusiano vipi ninamatatizo gani???

Aalafu kwa nini simpati demu mwenye sifa ninazotaka?? best wishes"

Jawabu:Shukurani kwa kukubali ku-share tatizo lako hapa kwa faida ya watu wengine wenye tatizo kama lako au ambao watakumbana nalo hapo baadae.

Sidhani kama unatatizo, hiyo ni hali ya kwaida inatupata watu wote tunapoachana na wapenzi wetu ambao tulikuwa tukiwapenda sana au tumekuwa nao kwa muda mrefu. Inakuchukua muda mrefu kabla hujaondokana na hilo yaani kwa kifupi ni kuwa alikuumiza sana au uliumia sana kumaliza/ua uhusiano hali inayokufanya upoteze imani na wanawake kwa ujumla ukihofia wao kuwa kama yeye at the end. Japo kuwa sio kweli kwani wanawake tunatofautiana. Hivyo all u need is time to heal jeraha lako.


Sio rahisi kupata mwanamke mwenye sifa zote uzitakazo kwani huyo atakuwa "perfect" na "there is no such thing" hapa duniani, kwani hata Malaika hawako hivyo. Ukiwa tayari kupenda tena au kuwa kwenye uhusiano basi fuata moyo wako lakini suisahau akili yako.

Jiwekee sifa utakazo kwa mwanamke lakini ikiwa utamdondokea mmoja ambae ana-tick box 5 muhimu out of 10 mchukue nyingine utarekebisha ukiwa ndani ya uhisiano. Kitu muhimu cha kuzingatia sio sifa alizonazo bali hisia zako za kimapenzi juu yake na je utakuwa mtu mwenye furaha ukiwa nae karibu?

Sasa take your time to get over kilichotokea alafu ukiwa sawa/tayari mambo yatakuwa bomba kuliko ilivyo kuwa na EX, kumbuka kwenda taratibu, kuwa wazi na boresha mawasiliano ili ikusaidie kumfahamu mwenzio zaidi.

I hope nimekujibu vema na umenielewa.

No comments:

Pages