Wednesday

Alini-treat kama taka, sasa yu mahututi...nijimuvuzishe?

"Dada Dinah,Mimi ni mdada wa miaka 38, ninaishi ughaibuni. Ninaelimu, kazi na ya kunipa kipato cha kunitosha. Miaka miwili iliyopita nikiwa 36 nilikutana na kijana wa kitanzania ambae alikuwa 29 wakati huo.

Alihamia kwangu na tuliishi vizuri tu, hakutaka rafiki yake hata mmoja ajue anaishi wapi. Katika kipindi tunaisha wote nilipata mimba, alipogundua nina mimba alitaka nikaitoe lakini nilikataa akaanza kunitomba kama ugomvi na alihakikisha kila siku tunatombana tena dog style!


Siku moja nikiwa kazini nikaona damu imeanza kutoka, niliomba Mungu isiendelee lakini jioni ya siku ile nilijua tu mimba haipo tena ilekuwa kama ya wiki 5-6. Baada ya kuishi kwangu kwa miezi kama 4-5 siku moja aliniambia amepata apartment yake na kwamba yeye na mimi tutakuwa tunatembeleana.


Alipohama alibaki na funguo za nyumba akawa anakuja mara nyingi mwisho wa wiki, lakini hataki rafiki zake wajue kama anakuja kwangu. Kwakuwa ninataka sana mtoto basi niliamua kutombana nae ili nipate mimba lakini kila tukitombana anamwaga shahawa nje.


Mwezi wa tisa mwaka huu kulitokea tatizo ambalo lilitufanya tukutane mahali ambapo alikuja na rafiki zake, pale alijifanya kunisalimia kama tu mtu anaemfahamu na akawa yuko karibu na wasichana wengine, nishindwa kuvumilia nikamwambia mimi na yeye iwe mwisho ana funguo zangu anirudishie.

Alikuwa akibembeleza sana na nilimrudisha mwezi wa kumi na moja mwanzoni, ila funguo sikumpa.Kuna siku aliniambia anakuja, lakini hakutokea, kesho yake nilimpigia simu na simu yake ilikuwa imefungwa, sikuwa na mtu wa kumuuliza kwani rafiki zake siko karibu nao. Baada ya mwezi ndiyo nikagundua kuwa alipata ajali ya gari na sasa hivi ni mgonjwa mahututi hospitali.
Dinah ninaomba ushauri."

Jawabu-Pole sana kwa kupoteza mimba, sasa dada yangu ilikuwaje mpaka ukawa unaruhusu akungonoe kwa nguvu na kwa mtindo ambao ulijua wazi kuwa unaweza kusababisha mimba kutoka? au ndio mapenzi ya dhati?


Natumaini ulienda kwa Daktari wakakuchunguza na kukusafisha, kwasbabu usipofanya hivyo unaweza usishike mimba tena au ukawa na matatizo mengine ya viungo vya uzazi hapo baadae. Ikiwa hukwenda basi hima, fanya haraka na weka mihadi na Daktari kwa uchunguzi na umueleze ilivyokuwa kwa uwazi.....namna ulivyokuwa ukifanywa kwa fujo ili mimba iharibike.


Huyu bwana huenda anaendesha maisha mengine bila wewe kujua, usikute Bongo ameacha familia na anahofia kuharibu uhusiano wake na watu wake na ndio maana alikuwa naficha uhusiano wane kwa watu wengine ambao wako karibu sana na yeye. Kutokana na maelezo yako huyu bwana alikuwa anakutumia.

Uamuzi uliouchukua wa kumaliza uhusiano ulikuwa wa busara kwani huyo sio mtu mwenye kujali na wala hana huruma, kama hakutaka kuzaa na wewe kwanini basi asingekuwa akimwaga nje tango mwanzo? Na hata kama hakuwa tayari au hakutaka kuzaa na wewe, kitendo cha kukufanya kwa fujo ili kuharibu mimba ni cha kinyama na hapaswi kusamehewa. Hicho kitendo alichokifanya kinaweza kabisa kukusababishia matatizo makubwa hapo baade, wakati huo utakuwa umeshasahau.


Lakini kwa vile mlikuwa mmerudiana mwenzi wa kumi na moja lakini kwa bahati mbaya hakutokea kwako baada ya kupeana mihadi na wewe baadae ukagundua kuwa amepata ajali na yuko mahututi, kama mpenzi wake na unampenda ni vema basi ukaenda kumjulia hali huko Hospitali.


Mungu akimjaalia na akapona basi mpe kitu cheupe a.k.a live, kuhusiana na kuficha uhusiano wenu na matokea yako ndio kama ilivyokuwa. Kisha mpe msimamo wako kuhusiana na aina gani ya uhusiano unataka, nini unategemea kutoka kwenye uhusiano huo na nia yako ya kuwa mama.......kuwa muangalifu hapa ktk maamuzi. Ikiwa kapata ulemavu basi tambua kuwa atakubali haraka haraka so u can look after him......


Katika hali halisi, huyu kijana hajakomaa/kua kiakili na hajui majukumu yake kama mwanaume, najua unajua kuwa hakufai........hivyo sioni sababu ya wewe kupoteza muda wako na mtu kama huyo mwenye akili ya ki-teenager.

Zingatia furaha yako kwenye uhusiano wa kimapenzi uutakao, hata kama unataka sana mtoto hakikisha unazaa na mwanaume ambae anania kama yako ya kuwa na mtoto, kumpenda, kumjali, kumtimizia mahitaji na kuwa pale kwa ajili yake.


Angalia hamu yako ya kuwa na mtoto isikufanye ujiingize kwenye uhusiano "abusive" kama wa huyu kaka aliepata ajali. Chukulia kila siku kama inavyokuja na hakika siku moja utakutana na Mkaka mwenye nia nzuri tu yakutaka kuwa "baba".


Usikimbilie Vijana "single" ambao wanadai hawajawahi kuoa kabisa, nenda kwa wanaume "single" ambao ni wajane (kuwa makini na hoji nini kilimuua mke wake) au "single" waliotalikiwa (kuwa muangalifu na dadisi nini hasa kilisababisha mwanamke mwenzio kutoa/kupewa talaka). Hii jamii akilini huwa wametulia na hawana haraka/mapepe vilevile wanauzoefu mzuri sana wa kimaisha tofauti na wale "BNNK" a.k.a bado nipo nipo kwanza.

Kila la kheri.

No comments:

Pages