Thursday

Ex anataka kuniharibia ndoa yangu-Ushauri

"Heri ya mwaka mpya dinah,
Mimi ni mwanamke wa miaka 30 nimeolewa na mume anaeni-treat vizuri sana. Hivi majuzi mume wangu alikua amesafiri nikapata namba ya mchumba wangu wa zamani ambaye ndio alikuwa bf wangu wa kwanza aliyenibikiri tukaanza kuongea kwenye simu tupo miji tofauti.


Nikawa so happy tukawa tunatombana kwenye simu nalegea kabisa lakini nikishamaliza kuongea nae najisikia vibaya sana kwanini namfanyia hivi mume wangu nikasema lazima ni-stop kuongea na huyu bf wa zamani.


Siku moja nikaamua kumwambia kuwa mimi nampenda mume wangu kwahiyo naomba tu-stop kuwasiliana. Alikasirika ile mbaya akasema atamwambia mume wangu kuwa nilikua nawasiliana nae sasa naogopa mume wangu ataniacha hata sijui nifanyaje dada dinah nampenda sana mume wangu naomba ushauri asante. "

Jawabu:Mwaka umechanganya kabla ya muda wake, heri ya mwaka mpya nawe pia. Asante sana kwa kuniandikia.


Sasa rafiki hata kama uliipata namba ya Ex kitu gani kilikufanya umsake na kuanzisha mawasiliano ukijuwa wazi kuwa penzi la kwanza huwa haliishi.....watapita wengi lakini wa kwanza daima atakuwa wa kwanza tu, ndio ulipojifunzia mambo, ndio ulipozijulia hisia za kupenda kiumbe wa jinsia tofauti na yako. Fanya yoote lakini stay away na 1st bf.


Kitendo ulichokifanya ni kibaya na kinahesabika kama "cheating" kwa vile ulipata hisia za kutamani, ulivuta hisia za alivyo huyo ex na ukajishikana na yeye akajipa mkono na hatimae wote mkafika mwisho wa safari......mkiwa simuni, mihemo, sauti za mahaba na kila kitu kilifanyika na kupenya kwenye akili zenu na mioyo yenu......shetani alikupitia eti??


Ofcoz mwanaume yeyote mjinga-mjinga lazima angekasirika, unalianzisha zali alafu sasa unamkatisha, kwani ulipoanza ulikuwa hujui kuwa unampenda mume wako?


Kama unaweza kufanya ngono via simu na Ex kwanini usingefanya hivyo na mume wako? Ni wazi kuwa unahisia fulani na Ex pia nahisi hiyo nambari yake ya simu ulikuwa nayo tangu zamani, ila ulikuwa unajaribu zali kuona itakuaje kukumbushiana enzi (hehehe just joking).....naelewa hilo na ndio maana huwa nashauri watu kukaa mbali na Ex hata kama waliachana kwa vita vya ghuba au kwa kuelewana.


Nini cha kufanya-Hakikisha huyo Ex hajui unapoishi na vilevile hajui mawasiliano mengine zaidi ya nambari yako ya simu. Kama nambari ya simu ya ndani (land line) basi waombe jamaa wa simu kublock nambari yake na ikiwa mlikuwa mnawasiliana via simu ya mkononi(mobile) unaweza kufanya hivyo mwenyewe (m-block) na kuanzia hapo cheza mbali (jitenge) naye au watu wengine walio karibu na ex wako huyo, ukifanikiwa hili utakuwa umeshinda na hakuta kuwa na sababu ya mume wako kujua nini kilitokea....hilo mosi.


Pili, ikiwa anajua mizunguuko ya mumeo na mawasiliano mengine kama emails basi hakikisha mume wako anajua nini kilitokea kutoka kwako moja kwa moja na sio kutoka sehemu ya tatu, kuwa wazi lakini usivuke mipaka ili kulinda hisia zake.


Tatu, Mueleze mumeo kuwa alipokuwa safarini, ex alianza kuwasiliana na wewe lakini hukuwa "comfortable" ukaamua kukatisha mawasiliano hayo kwa kumpiga marufuku huyo bwana (ex), na ulipofanya hivyo huyo bwana (ex) akakasirika na kusema kuwa atahakikisha ndoa yetu inavunjika.....alafu omba ushauri kwa mumeo kwa kusema mfanye nini?


Mumeo anaweza kukuhoji maswali ambayo baadhi ya wachangiaji au hata mimi mwenyewe nimekuhoji, hivyo hakikisha umejiandaa kutoa majibu ya kuridhisha vinginevyo anaweza kukushitukia kuwa wewe ndio ulianzisha zali.

Ndoa haiwezi kuvunjia kwa ku-cheat kwa simu japokuwa inaweza kusababisha mabishano makubwa, hasira baina yenu na hali ya kutokuaminiana ktk uhusiano wenu kwa kipindi fulani, lakini yote yatapita na hali itakuwa ya amani na furaha.......yote hayo yanategemeana wewe mwanamke utakavyojitahidi kurudisha Uaminifu ndani ya ndoa yenu.

Tafadhali jaribu kuheshimu ndoa yako ili kusaidia kurudisha thamani ya ndoa katka jamii.

Kila la kheri.

No comments:

Pages