Monday

Mimi ni mzuri, nifanye nini kuwa nae?-Ushauri

"Dada dinah naomba msaada wako kuna Kaka fulani nampenda sana na najua mimi ni mzuri hawezi kunikataa ila sitaki kumuambia kwamba nampenda sijui nifanye nini ili niweze kuwa naye naomba msaada wako dada"

Jawabu: Asante kwa barua pepe,kutokana na maelezo yako mafupi ni kuwa "umefika bei" lakini unahofia kukataliwa ndio maana hutaki kumwamabia kuwa unavyojisikia juu yake. Suala la uoga wa kukataliwa (kutokuwa na uhakika kama utakubaliwa) pia huwakumba wanaume lakini kwa vile wanaume wameumbwa na ujasili wanayo namana ya ku-deal na "rejection" kitu ambacho sisi wanawake hatuna.

Mwanaume ukimkatalia atajitahidi kukushawishi na mwishoni unajikuta unaanza kudondokea kidogo kidogo, mwanamke ukikatataliwa inakupunguzia ile hali ya kujiamini, aibu mbele ya mwanaume huyo na ukimfuatilia ili kujaribu kumshawishi utaonekana unawalakini kwa vile mwanamke sio muwinaji bali anawindwa.

Kitu muhimu unachopaswa kutambua ni kuwa hakuna uhusiano kati ya uzuri wa mtu na mapenzi kwa vile uzuri wa mtu uko machoni mwa mtu(mtazamaji) huenda wewe ukajiona umzuri sana na pengine rafiki na jamaa wa karibu wanakuona na kukusifia kama vile Mungu alitumia muda wake vizuri sana alipokuwa akikuumba wewe. Hiyo sio tiketi ya yeye kukupenda au kutaka kuwa na wewe kwa vile mimi na wewe hatujui kama anakuona mzuri kama unavyojifikirua/jijua.


Kwa vile huna uhakika kama na yeye anahisia juu yako(hujagusia kwenye maelezo yako kana na yeye anaonyesha "interest") kumwambia moja kwa moja haitokuwa sahihi hivyo unahitaji kuwa karibu nae kwa kurafikiana kwanza, kama mwanaume atajua wazi kuwa "unamzimia" na hakika atakutokea lakini kama hana hisia za kimapenzi juu yako basi hatofanya hivyo namtabaki marafiki tu.

Njia rahisi ni kutafuta mawasiliano yake kama anuani ya barua pepe au nambari yake ya simu kisha anzisha mazungumzo nae lakini hakikisha unabaki na ahiba yako kama mwanamke. Kama jamaa hana mpango na wewe utatambua na ikiwa jamaa anampango na wewe pia utafahamu.

Akionyesha kuwa na mpango na wewe basi unaweza kumualikwa kwa ajili ya kinywaji pale dukani kwa Mangi (popote patulivu) au kwenda kwenye tamasha/mkutano/kanisani n.k. vilevile kama kuna sherehe basi jaribu kumpa taarifa mapema ili aweze kuhudhulia hali itakayokufanya uwe karibu nae zaidi kwani kati ya wageni/watu wote watakao kuwepo mahali hapo ni wewe tu ndio atake kuwa anakujua hali itakayo mfanya asicheze mbali.

Wanaume ni wepesi kutambua ikiwa wanapendwa bla hata kuambiwa hivyo baada ya muda fulani atajua tu kuwa unamtaka na atakutokea/tongoza au vyovyote itakavyokuwa ilimradi tu lengo lifikiwe ambalo ni kuwa nae kama mpenzi wako.

Kama huna namna ya kupata nambari yake ya simu njoo nikupe mbinu moja rahisi sana ya kufanikisha hilo.

Kila la kheri.

No comments:

Pages