Wednesday

Mume wangu amebadilika sana,nifanye nini?

"Dada Dinah nakupa hongera sana kwa kazi unayoifanya kwa ajili yetu. Baada ya kuwa mpitiaji wa blog yako na kujifunza mambo mbali mbali kuhusu ngono na kukusoma jinsi unavyowaelezea watu kwa upeo wa hali ya juu nimeamua kuchangia tatizo langu ili nipate malezo kutoka kwako.

Nimekuwa kwenye ndoa na mume wangu kwa muda wa miaka 15 na tumejaaliwa kuzaa watoto watatu. Nilivyofunga nae ndoa mimi nilikuwa sio mtu wa kujishughulisha sana kutokana na kutokuwa na Elimu ya awali kama wewe na matokeo yake nimejifunza mambo mengi hapa na kwenda kuyafanyia kazi kla ninapofanya mapenzi na mume wangu.

Tumekuwa tukifurahia zaidi maisha yetu kitandani kuliko ilivyokuwa hapo zamani na cha kushangaza mume wangu hajawahi kuniuliza kuhusiana na kubadilika kwangu kitandani lakini amekuwa akiwahi kurudi nyumbani lakini kinachonikera ni tabia yake ya kunichunga kwa kunipigia simu kila wakati na kuuliza nilipo, sio kawaida yake.

Je ananichunga kwa vile yeye ndo mtokaji au imekuwaje? Naombeni ushauri wenu ili nisije kuwa nachezwa shere. Ashura"

Jawabu: Shukurani Ashura nafikiri mpenzi wako anajitahidi kukuonyesha kuwa anakujali na kukupenda. Huenda kabla ya hapo (haikuwa kawaida yake) hakuwa na hofu ya "kuibiwa" kwa vile ulikuwa hujamuonyesha uwezo wako wa kufanya "mambo fulani", katika hali halisi alijua kabisa kuwa "kingono" hujiamini kama ulivyosema wewe kuwa hukuwa mtu wa kujituma mlipofunga ndoa.

Lakini baada ya kujifunza na kufanyia kazi yale uliyojifunza kupitia hapa amegundua kuwa mambo yako ni makubwa na akishangaa-shangaa iwe kutokukuridhisha kingono au kutokukuonyesha anakujali na kukupenda basi mtu mwingine anaweza "kupata mambo" anayopata hivi sasa.

Mume wako anastahili pongezi kwa kutokukushutumu au kukuhoji umejifunza/julia wapi na badala yake anafurahia na wewe na kujitahidi kukuonyesha yuko pale kwa ajili yako(najua ni tabia mpya na hakika inakera kwa vile hukuzoea) lakini hana jinsi zaidi ya kuhakikisha Mke wake yuko salama popote alipo na hakuna mtu atakaethubutu "kutaifisha mali zake".

Kwa kawaida wanaume wengi huishiwa hali ya kujiamini ikiwa wapenzi wao ni wakali/watundu na hapo utaona "ulinzi" unaongezeka.

Hongera sana na kila lililojema kwenye maisha yano ya ndoa na familia.

No comments:

Pages