Tuesday

Nifuate Moyo wangu au Imani ya Dini?-Ushauri

"Dear Dinah Naomba ushauri wako na wadau wenzangu wa blog yetu hii Mimi ni binti mwenye umri wa miaka 25 sasa niko Australia, ila ninatokea Mombasa na nimekulia Arusha.

Katika kipindi cha nyuma nilikuwa na mahusiano ya kimapenzi na watu tofauti kila nikipata mpenzi hanifai either hatuko sawa kidini au kifikra .Kwa kuwa nilikuwa disappointed na mimi mwenyewe na mahusiano yangu nikaamua kutafuta mvulana mwenyewe bila kutafutwa .

Nikafanikiwa kumpata kijana ambaye tumekua pamoja tunajuana vizuri tu (tumuite JP) .Mahusiano yetu yalikuwa ya kirafiki , baada ya muda akaniambia anahisi ananipenda tukawa na mahusiano ya mapenzi kwa mwaka mmoja. LAKINI mahusiano yetu kipindi chote yalikuwa kwa simu.

Kwa sababu mimi niko huku nje na yeye yuko Arusha. Tumewasiliana kwa kipindi kirefu tukafikia hatua ya kukubaliana kama Mungu akipenda tunaweza tufunge ndoa. Hivi karibuni mwezi mmoja umepita alikuja kunitembelea rafiki yangu wa kiume (rafiki wa kawaida tu) kutoka nchi jirani(tumuite LUCKY).


Tumekaa pamoja kwa muda wa siku kumi kipindi chote tulichokaa tulizoeana sana kupita mazoea ya mwanzo hisia za mapenzi zikajitengeneza ndani yetu na tukagundua tunapendana sana tu .


Tatizo linakuja nimempenda huyu rafiki yangu LUCKY sana ila yeye tunatofautiana kimila kitamaduni na kidini japokuwa kifikra tuko sawa sana na tunaendana kwa mambo mengi. Wakati JP tuna Dini moja japokuwa tamaduni tofauti na yeye hajachacha sana kielimu na kifikra yuko sawa vya kutosha japo kuna tofauti kidogo ambazo hazistui sana .

Ukweli ni kwamba JP naye nilihisi kumpenda, ila kwa sababu siajonana naye kwa muda mrefu mapenzi si strong sana na pia mapenzi yetu yalianza kufifia haswa kipindi LUCKY alipokuja huku kwangu.

Hivi karibuni nikaamua kuchukua uamuzi wa kumuacha JP kwasababu nilihisi ntampotezea muda. Kwasasa nahisi kama nilifanya uamuzi usio wa busara. Kwa sababu Wazazi wangu hawata kubali nioane na mtu wa dini tofauti na mimi mwenyewe roho inanisuta nahisi kama nitaikosea Imani yangu.

Ninashindwa kuelewa je nampenda LUCKY kweli au ilikuwa mapenzi ya muda. Je ni kweli simpendi JP au ni kwa sababu yalikwa mapenzi ya mbali na pia sababu hatujaonana kwa muda mrefu??

Au nimuache pia LUCKY nisubirie nyota yangu inimulikie mtu mpya? Yaani sina raha wala amani kwa sasa. Nakaribia kurudi nyumbani Rafiki zangu wote wanaolewa na najua swali litakalo fuata kwangu ni nitaolewa lini.

Kujieleza nampenda mtu Dini tofauti sitaweza. Sijui nifanye nini? Naomba ushauri je nibaki na LUCKY kwasababu nampenda niachane na Imani za kidini nifuate moyo.

Au nikapendane na JP kwa sababu ninamjua vizuri na ni Dini moja kuhusu mapenzi tutazoeana huko huko baaada ya ndoa? Au nisubiri labda nitapata bahati nyingine??

Ni mimi R"

Jawabu:Asante R kwa ushirikiano, kutokana na maelezo yako inaonyesha wazi kuwa kuna vitu 3 muhimu sana kwenye uhusiano wako wa kimapenzi, Mosi ni Imani yako ya Dini, Pili Uwezo wa kiakili wa mhusika na Tatu ni Tamaduni.

Nasikitika kusema kuwa yote hayo hayahusiani kabisa na mapenzi, unapompenda mtu huangalii wala kujali ananini? aina ya maisha yake, Dini, Umri,muonekano n.k.

Penzi linajitokeza popote, kwa yeyote na wakati wowote, huwezi kupanga kumpenda mtu hata siku moja jampokuwa kama wanadamu huwa tunapenda kujiwekea viwango fulani vya aina ya wanaume/wanawake tunaotaka kuwa nao kama wapenzi lakini ukweli ni kuwa sio lazima utakuja mpenda mwenye "viwango" vyote utakavyo ama atakuwa na tatu kati ya kumi au ukiwa na bahati basi itakuwa tano kati ya kumi.

Kutokana na umri wako bado unakua kiakili hivyo ni mapema sana kusema kuwa umekuwa "disappointed", katika kipindi ulichonancho wanawake wengi ndio wanaanza kuijua miili yao na pia kuharakisha maisha wakitaka kuwa wamefunga ndoa by the time wanaumri wa miaka 30 hali inayosababisha wengi kuhisi hawana "bahati" kwa kuacha au kuachwa kwa vile wanaharakisha mambo ambayo wapenzi hawako tayari kuyafanya (wanataka ku-enjoy life kwanza) hali inayosababisha kutokuwa na amani ndani ya uhusiano.

Nilichokigundua hapa ni kuwa upweke ulichangia kwako kutokuwa na msimamo juu ya penzi la PJ na wewe na ni sababu kuu ya wewe kujihusisha kimapenzi na rafiki yako Lucky.

Kwa kawaida mwanamke anapofanya mapenzi huwa anahisi kujiamini "sexually" na kupendwa, hapo ndio tatizo lilipojitokeza na kukufanya um-buti PJ lakini ukweli unaujua moyoni mwako unajua wazi kabisa kuwa unampenda PJ(maelezo yako yananieleza hivyo).

Ili kufupisha hadithi (usije hisi "nakudongoa" bure hehehehe), Kwa vile PJ ana vitu muhimu unavyovitaka mwanaume awe navyo Imani, Tamaduni na Uwezo wa kiakili ukiachilia mbali kuwa anakupenda (kajtolea kaka wa watu kukupa moyo wake japo ukombali na kukusubiri ni wazi kuwa mabegi kayashusha juu yako).

Mimi nakushauri urudi kwa PJ na kumuomba msamaha na kueleza kitu gani kilikufanya umtose (usiseme ulikuwa na Lucky kwani utamuumiza), Sio rahisi kumpata mtu ambae ana "viwango" 3 muhimu kati ya vitano utakavyo kutoka kwa mwanaume......PJ anavyo.

Unaweza kutumia sehemu ya maelezo yangu haya "Akili yangu ilikuwa haijatulia na nilikuwa sijui nataka nini, nilipagawa na nidhani kuwa nahitaji muda kidogo kujua nataka nini na ili kufanikisha hilo sikutaka kukupotezea muda kwa sababu sikujua nitaamua nini na ndio maana nikampa nafasi (kibuti) ili uwe huru incase ungeamua kupenda mwanadada mwingine badala yangu."

Tuombe Mungu PJ hajaamua kuendelea na maisha yake na alikuwa anakusubiri urudi (wanaume wakipenda kweli huwa wanasubiri urudi).

Nenda taratibu na maisha, hata siku moja usiharakishe na pia unapoamua kufunga ndoa fanya hivyo kwa kujua kuwa uko tayari na pia una mapenzi ya kweli kwa mwenza wako kwani ndoa ni milele.

Ndoa ni Muhimu na ni sehemu ya pili ya maisha yetu baada ya kuzaliwa lakini usilazimishe ndoa kwa vile tu rafiki zako wamefunga ndoa au kulazimishwa/songwa na familia ufunge ndoa haraka kabla hawajaondoka Duniani n.k.

Furahia kila siku kama inavyokujia na umshukuru Mungu kwa kukuwezesha angalau kuiona siku mpya kuliko kujaribu kufanya mambo haraka kuridhisha jamii na marafiki.

Kila la kheri!


No comments:

Pages