Wednesday

Ndoa ya mkataba....

Dada Dinah, unajua wakati mwingine najiuliza inakuwaje mambo kama haya yanafanyika na je yanauhalali gani kwa huyu na kwa mwingine isiwe hivyo!Wikiendi hii nikiwa nimejipumzisha kuvuta muda, unajua tena `funga’, ukiwa nyumbani inavyonoga.

Akaja binti jirani. Sikumuelewa awali, kwani alivyojistiri kinamna usingeweza kujua kuwa bado ni `mtoto wa watu'.`Nilikuja kumuona dada, nilikuwa na shida naye' alianza kujieleza kwa aibu, na niligundua kuna tatizo ambalo limemkwaza.

`Akija nitamuambia, kama ni lazima yeye' nilisema nikichelea nisije nikateleza na kuiathiri swaumu yangu.`Aaah, unajua ningemueleza mwanamke mwenzangu ni rahisi kunielewa, lakini hata wewe unaweza kunisaidia kwa ushauri, ingawaje najuwa wanaume mnalindana kinamna’.

Haya dada Dinah, kaa mkao wa kusikiliza kisa chenyewe. Binti huyu ni miongoni mwa wale mabinti wanaoolewa kwa kupitia mtu mwingine, anaweza akawa kaka mtu kamuolea mdogo wako, kwa hiari ya mdogo mtu.

Mwanaume muoaji ni wenzetu, wanaosoma na kubeba maboksi huko Ulaya, akaona asivunje taratibu na adabu za kwao. Aliomba wazazi wake wamtafutie `kimwana' huku bongo akirejea asisumbuke, kwani umri nao ulishaenda.

Na kweli wanandugu wakaifanya hiyo kazi barabara, na binti mrembo mwenye adabu na aliyekulia katika maadili akapatikana. Na akakubali kwa hiari yake mwenyewe kuolewa.Sasa ni mwaka wa tatu tangu ndoa ifanyike.

Bwana wanawasailiana na mkewe kwa barua na simu lakini hajafika, na `hawajaonana' na binti. Lakini mawasiliano, matumizi na mapenzi ya`telefoni' yalishamiri utafikiri walijuana kabla.Taarifa nyepesi nyepesi zikaja kuwa jamaa anaye mwanamama wa kizungu akipitisha naye muda kwa mkataba, kuwa akimaliza `masomo' yake wasijuane tena (nasikia hii ipo sana).

Na jamaa anawaambia rafiki zake kuwa ana mke home na huyu huku ni wa kupitisha muda tu, `rijali lazima uwe na kitu...'Binti kuipata hiyo akaona `anaonewa' kwanini iwe hivyo, kwanini kama ni hivyo naye asipate wa kupoteza naye muda kama mwenzake?


Yeye aliuliza na kuongeza, `sio kwamba nataka kufanya hivyo, sitaki kabisa machafu hayo, lakini nahisi sitendewei haki'Anaomba ushauri je upo uhalali wa namna hiyo? Zipo ndoa za mikataba? Je hata kama akija kutakuwa na mapenzi ya kweli, ili hali mwenzake keshaonja mapenzi ya kizungu?(akiwa na maana wenzetu `wadhungu’wanayajua mapenzi zaidi kuliko sisi, hivyo yeye ataonekana si kitu.Majibu niliyompa nayahifadhi kwanza, nisikie wenzangu mnasemaje na hili.

Na hasa hili jipya la `ndoa ya mkataba' je ipo ndoa ya namna hii.

Nawasilisha.emu-three

Jawabu: Hehehehe asante M3 ulivyoandika nimeburudika sana, nilifikiri nasoma liwaya. Uandishi wako unavutia kusoma. Shukurani kwa kuweka suala hilo hapa.

Nijuavyo mimi ni kweli kabisa kuwa kuna ndoa za "makaratasi" ambazo ndio tunaweza kuziita za mkataba japokuwa upande wa pili huwa hawajui kua ni ndoa ya "Muda", kwamba watu huamua kufunga ndoa na watu wengine ili baada ya muda fulani wapate haki ya kuishi nchi husika na muda huo unapokwisha basi talaka hutolewa kisheria na kila mtu anachukua ustaarabu wake.


Lakini ndoa hii inapokuwa imefunga ule upande wa pili (mara nyingi huwa wadhungu ) huwa hawajui kuwa wanaoa au kuolewa kutokana na Utaifa wao na sio mapenzi hivyo mapenzi hutolewa kama "ifuatavyo" na kila kitu kina kuwa kama uhusiano wowote ule wa ndoa mpaka hapo "mtaka makaratasi" anapopata Utaifa kama wa "mke/mume wake".


Huyu binti alihitaji kueleweshwa tangu awali kitu gani kinaendelea huko Ulaya na kwa uwazi kabisa kwanini kuna hiyo ndoa ya "mkataba" kisha angefanya uamuzi wa busara kabla hajafunga ndoa na "hewa" au Picha.

Huyu binti inaonyesha hamnazo kabisa au alibabaika kwa vile Jamaa yuko Ulaya, alikubali vipi kuolewa bila kujenga mapezi kwanza na "mume wake"? Anauhakika gani kuwa ataweza kuishi maisha yake yote na huyo "mume wake" na kuvumilia mapungufu yake? Tuyaache hayo.

Huyu binti kama mwanamke anaejiheshimu hapaswi kulipiza kisasi maana kuwa umbile la mwanamke linakuwa "ruined" kwa kungonolewa ovyo, pili matunda ya kungonoka ni magonjwa ya Zinaa na kumimbwa na hilo likitokea ni wazi kuwa atapoteza maisha yako kizembe na kijinga, pili akishika mimba na kuzaa ni wazi atakuwa amepoteza ndoa yake na wakati huohuo utakuwa na mtoto ambae huna uhakika kama baba yake atamuhitaji yeye kuwa mke wake.

Suala muhimu kwa huyu Binti ni kuzungumza na "mume" wake na kuomba kueleweshwa kwanini ndoa ya Mkataba ipo, faida yake ambayo bila shaka itamfaidia yeye pia na ukweli wa ndoa hiyo kuwepo kwa muda gani, kama mke basi ajaribu kumuwekea mipaka mume wake in terms of kutowa na familia ya "mkataba", ikiwa mume atakubali basi aendelee kuvumilia mpaka "mkataba" utakapokwisha.

Vinginevyo ni kutoa talaka ili awe huru kuendesha maisha yake nahatiame kukutana na mwanaume mwingine ambae atajenga mapenzi ya kweli na hatimae kukubaliana kufunga ndoa.

Suala la ujuzi wa kufanya mapenzi halina Uzungu ni mtu mwenyewe tu, uwezo kwa kufanya mapenzi, utundu wake, hali ya kutaka kujifunza na kujaribu mambo mapya, kuujua mwili wake, kuwa muwazi na mdadisi juu ya mwili wa mume wake......hey Dinah sio mzungu lakini niko juu zaidi ya wazungu wengi hehehehehehe.

Msalimie....

No comments:

Pages