Monday

Alinichumbia lakini akaoa mwingine, sasa ananisumbua, nimkomeshe vipi?

"Nawasalimu wote,
Mimi ni mdada mwenye umri wa miaka 33 hivi na nina mtoto mmoja wa miaka miwili na nusu. Nilitokea kupendana na kijana mmoja hivi wa kichaga ila kweli alichonitendea sitasahau. Ukweli mimi nilimpenda kutoka rohoni na sikuangalia ana nini ila nilisikiliza roho yangu na nikampenda, na kwa wakati ule niliamini pia na yeye alikuwa amenipenda kwa dhati.

Tulikaa muda wa kutosha na wote kwa pamoja tuliamua kuanza process za kuoana na kwa wakati huo nilikuwa na miaka 28, basi tulikubaliana kuona na mipango mbalimbali ilianza ikiwa ni pamoja na kunivalisha engagement ring.

Mimi nilishauriana na wazazi wangu na ikaamuliwa shughuli ya engagement ifanyike nyumbani kwetu, na ndivyo ilivyokuwa. Baada ya engagement nilisafiri kikazi nikaenda Nje na nilikaa huko kama wiki nne hivi, wakati wote huo nilikuwa nalazimika kumpigia mchumba wangu simu mara kwa mara kumjulisha hali.

Baadaye nilirudi Tz baada ya kazi iliyonipeleka huko kuisha. Kama mwezi hivi tangu nirudi nikagundua kuwa nilikuwa mjamzito, sikushtuka nilijua kisingeharibika kitu kwa sababu nilikuwa nimeshaweka mambo wazi.

Wakati huo nikaanza kupata tetesi kuwa huyo kaka ambae sasa ni mchumba wangu alikuwa ana uhusianao na mama mmoja aliyekuwa ameachika kwa mume wake akiwa na watoto watatu, hivyo huyo kaka alikuwa akiishi kwa huyo mwanamke, mimi sikuwahi hata kumshtukia kwa sababu pia mimi kazi zangu nyingi zilikuwa za kusafiri mara kwa mara.

Nilipofuatilia nilikuta ni kweli na ushahidi ni kuwa siku moja nilikamata wallet yake ikiwa na vyeti viwili vya angaza kimoja kikiwa na jina la huyo aliyekuwa mchumba wangu na kimoja kikiwa na jina la huyo mwanamke.

Kumbe walishakubaliana kuona, hata hivyo kulikuwa na picha ndogo ya huyo mwanamke kwenye wallet hiyo ya mchumba wangu. Nilipomuuliza alikana akasema sio wallet yake eti ni ya rafiki yake.

Niliendelea kukuza mimba yangu bila hata kupata msaada wowote kutoka kwake, na wakati huo ndio alikuwa akila maisha na huyo mwanamke aliyekuwa akiishi kwake na wakati huo huyo mwanamke alikuwa amemkabidhi Rav 4 ya Bluu, taratibu za kufunga ndoa na mimi zikawa zinapigwa chenga tu.

Kila nikimuuliza alikuwa hana jibu kamili, sasa na mimi nikaacha kumuuliza maana yake mtu mzima niliona kufunga ndoa sasa ni ndoto, siku moja kipindi cha Xmas huyo aliyekuwa mchumba wangu aliondoka na huyo mwanamke hadi nyumbani kwao Moshi kwenda kumtambulisha kwa wazazi wake hao hao waliomsindikiza kuja kwetu kunivalisha engagement ring ndio hao hao walimpokea huyo mwanamke na kukaa naye kwa muda wa wiki mbili.

Wakati akimpeleka huyo mwanamke kwao, nilikuwa nimebakiza wiki mbili tu kujifungua, Mungu akasaidia nikajifungu salama, na alikuja Hospitali, lakini hakutoa hata Shilingi moja na bili iliyokuwa inatakiwa ni 148,000.

Siku niliyokuwa natoka Hospitali alisingizia kuwa alikuwa anaenda Airport kumpokea rafiki yake lakini ukweli ni kwamba alikuwa ameenda kwa yule mwanamke. Hiyo haikuwa tatizo kwangu, kama niliendelea kujitunza mwenyewe kwa kipindi kile cha Ujauzito bila yeye kujishughulisha sitoshindwa sasa.

Huyo mwanaume alikuwa akija nyumbani kwangu na kutoa maneno ya kashfa na alikuwa akikuta mtoto amelala anamuamsha, haikuishia hapo, maternity ilipoisha, nilirudi kazini kwangu, na ndipo aliponifuata na kuniomba msamaha huku akalia.

Mimi nikamsamehe kwa sababu niliona labda hatarudia tena, basi nikampa sharti la kuhama ule mji tuliokuwa tukiishi mwanzo tukahamia mji mwingine na akafungua bisahara zake huko ambazo kweli ilibidi nimuongezee mtaji, niliamini angetulia.

Lakini kumbe haikuwa hivyo, baada ya kuona bisahara imekolea akaanza ufuska tena, na kwa kuwa mimi nilikuwa nafanya kazi field zaidi, basi kila nikisafiri alikuwa anaoa, wanawake wa kila aina, pete ya engenement aliyonivalisha akaichukua akamvalisha mwanamke mwingine tena, ikawa ni vurugu tu.

Nikirudi nyumbani nakuta Condom zimetumika zimetupwa chini ya uvungu, na siku moja nilikuta condom saba zilizotumika zimetupwa bafuni. Kweli ni story ndefu na siwezi kuandika yote. Niligundua huyu mwanaume alikuwa akipenda hela zangu sana kwani kila mshahara ukitoka anautaka wote hata senti habakizi, usipompa ndani hakukaliki.

Basi nilioona hali inakuwa mbaya nikaamua kuachana naye nikatafuta kazi sehemu nyingine nikapata, nashangaa alikuja katika huu mji ninaoishi akaulizia watu hadi akapajua ninaposihi sasa ameanza kunitishia, mara ataniua, mara atanifanya hiki na kile.

Shida yake anataka arudiane na mimi na baada ya mimi kuachana naye biashsra zake zimeyumba, manake hana msimamo ni kuhonga wanawake tu hana kai nyingine, na mpaka sasa mtoto ana miaka miwili na miezi 4 hajui anakula nini, anavaa nini wala anaishi vipi.

Sasa naomba mnishauri nimfanyeje manake nimeshatamani hata angetoweka duniani tu, maana hana anachofanya cha maana zaidi ya kunikosesha amani, mpaka sasa nimeamua kuishi na mwanangu tu. Naombeni msaada, ni nini naweza kufanya ili nimkomeshe.
Asante".

No comments:

Pages