Friday

Wakwe hawataki niolewe na Kijana wao, nahisi nina ujauzito-Nifanyeje?

"Za kazi dada, pole kwa kazi ya kuelemisha jamii.
Mimi ni mwanamke mwenye miaka 23 sasa, lakini bado sijabatika kuolewa japokuwa nina boyfriend ambaye nampenda sana ila tatizo limejitokeza hivi juzi alipoenda kuwataarifu wazazi wake kuwa anataka tufunge ndoa.

Wazazi wake wamekataa na kumwambia mke wa kwanza wa mtoto wao ni lazima wamkabidhi wao kama wazazi, baada ya mpenzi wangu kunipa habari hizo sikujua nifanye nini wala niseme nini kwake.

Yeye anadai kwamba ananipenda hawezi kuniacha, lakini nimvumilie kwa muda na ndani ya miezi miwili ili atimize mashariti ya wazazi wake kwanza kwanza ndio ajue nini cha kufanya, leo hii (Email imenifikia Dinahicius wiki iliyopita) ndio kaenda kuoa nami najihisi mjamzito ila yeye bado sijamwambia,

Naomba ushauri please, nifanye nini?"

Dinah anasema: Namshukuru mungu kwa sasa niko salama baada ya kukamatwa na Hay Fever na ndio maana nilishindwa kujibu swali lako mapema, samahani kwa hilo.

Pole sana kwa Mkasa unaokabiliana nao. Kwa kweli nashindwa kuamini kama kuna Makabila ambayo bado yanasisitiza/lazimisha watoto wao kuolewa na watu walioawachagua wao kama wazazi. Hili la mke wa kwanza atafutwe na wazazi alafu baada ya hapo ndio kijana aoe anaemtaka yeye ndio nimeliesikia hapa! Inasikitisha sana.

Nadhani kuna mawili hapa Moja, ni kuwa wazazi wanamlazimisha kufunga ndoa na binti waliomtafutia wao (Inanikumbusha wimbo wa Binti Kimanzi) kama kijana anaeheshimu wazazi wake na kuwaridhisha kwa kila hali ni wazi itakuwa ngumu kwake kutaaa matakwa yao (inategemea na Mila, Utamaduni wao na Uoga wake yeye kama mwanaume).

Baadhi ya wanaume hufunga ndoa za kulazimishwa na kuishi na wake zao ambao hawana hisia nao kwa muda bila kushirikiana nao kimwili na kuwapa vituko mpaka wake hao kuomba Talaka na baada ya Talaka jamaa huenda kufunga ndoa na yule ampendae ambae ni chaguo lake ambae aliendelea na uhusiano nae wakati yuko kwenye ndoa batili.

Kama hii ndio nia ya mpenzi wako then hakuna haja ya kuwa na wasiwasi as long as unajua nini kinaendelea na siku zote anakuwa kwako.....hii haikufanyi wewe kuwa the other woman bali unamsaidia kuridhisha wazazi wake. Kumbuka mke "mtafutwa" ndio the other woman....ukimsadia kufanya vituko ni wazi mwanamke yule ataomba Talaka mapema.

Pili, inawezekana kabisa kuwa huyu jamaa anashindwa kukuambia ukweli tu kuwa hataki kufunga ndoa na wewe kwavile sio "wife type", anakupenda sawa lakini haoni kama unafaa kuwa mke wake. Kuna wanaume wengi sana hasa Afrika wanatekereza zoezi hili, utakuna Girlfriend wake mzuri kwa kila hali na wamekua pamoja kwa miaka mingi lakini anaishia kuoa "kitu cha ajabu" (mwanamke ambae wala hawaendani) na baada ya ndoa jamaa ataendelea na Girlfriend wa zamani au kuwa na Girlfriend mwingine ambae wanaendana nje ya ndoa yake.

Hii ni kwa vile baadhi ya wanaume wa Kiafrika wanaamini kuwa mke ana viwango vyake tofauti na mpenzi mzuri alienae mwenye kujipenda, kupenda maisha, kujali na kujituma/jitegemea kiuchumi. Nadhani umewahi kusikia wengi wakisema Uzuri wa mwanamke sio sura bali ni tabia.....imani hii ndio inapelekea wanaume kuoa bila mapenzi au attraction na hivyo ku-cheat on their wives kwa kutokana wanawake ambao wanawavutia na pengine kuwapenda nje ya ndoa zao. Inasikitisha lakini ni ukweli.

Sasa, kwavile unahisi kuwa unamimba nadhani ni vema kama utamjulisha jamaa kuwa umeshika mimba, kama kweli anakupenda na anania yakufunga ndoa na wewe baada ya "kuridhisha wazazi" na anajali maisha ya mtoto wake atakaezaliwa mwakani hatoendelea na ndoa au hata kama ataendelea nayo na kufanya kama "Binti Kimanzi" kwamba mume hatoi ngono, hali chakula chake, halali nyumbani n.k basi itakuwa vema.

Lakini kama mjamaa yuko serious na mke "mtafutwa" na anataka ku-share kitanda na kum-treat kama mke then sahau kama alikuwa mpenzi wako, hakikisha anajua umebeba mimba ya mtoto wenu ili asaidie kwa matunzo na malezi ya mtoto hapo baadae.

Mtoto atakapozaliwa (Mungu akijaalia mwakani) utakuwa na miaka 24, bado ni binti mdogo na una nafasi kubwa sana ya kuweka sawa maisha yako na kumlea mtoto wako kwa mapenzi yako yote. Mungu atakujaalia na utakutana na kijana mwenye kujali ambae atakuwa mume mwema hapo baadae.

Ni vema ukajifunza kudadisi asili, mila na desturi za mpenzi wako mpya ili kujua taratibu za kwako. Hupaswi kumuuliza yeye mwenyewe bali zungumza/uliza watu wenye asili kama yake ili usirudie makosa.

Usijipe hofu kipindi hiki ambacho unakuza kiumbe tumboni, jaribu kutuliza akili na kumfiria zaidi mtoto wako huyo atakae zaliwa. Ingekuwa nchi zilizoendelea hakika jamaa wa huduma ya Afya wangekupa Ushauri Nasaha na kukupa nafasi kama unataka kuendelea kutunza mimba au kuisitisha ikiwa changa (mimba ya mwezi mmoja ambayo ni kijibulungutu cha damu kinakumbwa wa mbengu ya Apple na Kisheria nchi za Magharibi unaruhusiwa kutoa) kwa njia za kisasa na salama zaidi.

Kwa bahati mbaya Tanzania hatuna utaratibu huo japo kuwa watu wanatoa mimba kienyeji na kwa njia za kizamani ambazo ni hatari kwa maisha yako, hivyo nisingekushauri ufanye hivyo japo baadhi ya wachangiaji wamegusia hilo.

Nakushauri utunze hiyo mimba kama kweli ipo na lea mtoto wako kwa kusaidiana na baba yake.

Kila la kheri!

No comments:

Pages