Wednesday

Niko nae kwa ajili ya mtoto wangu tu, sina hisia nae-Nitoke vipi?

"Hi dada dinah pole na kazi za kuisaidia jamii katika masuala muhimu ya maisha , mimi ni dada mwenye umri wa 25 nina mtoto mmoja wa miezi tisa sasa. Nimsomaji mzuri sana wa safu hii na nimefaidika sana katika suala zima la mapenzi.

Nilishawahi kuomba ushauri zaidi mara mbili na nilishauriwa vizuri nakutatua matatizo
yangu. Leo nimekuja tena kuomba ushauri katika haya yanayo nisumbua . Ninaishi na mchumba wangu ambaye ndio baba wa mtoto wangu huu ni mwaka wa pili sasa.

Nilikuwa nampenda sana ila sasa mapenzi yameisha kwani nina wasiwasi kuwa yeye hanipendi kutokana na vitendo vyake na pia hana samahani, hana pole, wala nakupenda tena wakati mwingine akikosa yeye atanigeuzia kibao mimi ndio niombe samahani.


Kwa mfano siku moja alilala nje ya nyumbani kwetu, aliporudi asubuhi sikumuuliza kitu nikakaa kimya, yeye alikwenda moja kwa moja kitandani kulala kwani ilikua 11 asubuhi na mimi kwakua usiku sikulala nikiwaza kapatwa na balaa gani nikarudi kulala, baada ya nusu saa hivi akaniambia oh kazini kulitokea wizi kwa hiyo haikuwezekana kuondoka.

Nikamuuliza mbona hujanitumia hata sms kua kuna tatizo limetokea unanipenda kweli?
akajibu "sikupendi! kwani nimekuletea mwanamke hapa ndani?akaniambia tena ndugu yako amewekwa ndani na kwakuwa ilikua Jumamosi hamna dhamana nika mwambia basi naenda kumuona huko nitaujua ukweli. Cha ajabu alikuja juu na kunikataza nisitoke nyumbani siku ile hata kwenda dukani hakutaka niende.

Dinah anasema: Kosa kubwa ulilofanya ni kukaa kimya, hii inaonyesha kuwa unamuogopa jamaa na yeye anajua kuwa unamuogopa na hivyo kuwa huru kufanya atakalo akiwa na uhakika hutosema kitu.

Tunapokuwa kwenye uhusiano na mnaishai pamoja technically mnakuwa mnaendesha maisha kama wanandoa hivyo kila mmoja wenu anakuwa na haki ya kuhoji mabadiliko yeyote yanayojitokeza Mf: uchelewaji, unajua muda wake ambao huwa narudi nyumbani sasa siku akichelewa kurudi katika hali halisi unapaswa kuhoji kwanini amechelewa au yuko wapi kwani muda umepita.

Aliporudi asubuhi yake, ulitakiwa kuhoji kilichomfanya alale nje na ungemwambia kabisa unataka maelezo ya kutosha na kuridhisha kwani kitendo chake kimekufanya ushindwe kulala kwa hofu, wasiwasi wa hali ya juu....sio kusema "kama kunatatizo ungeni sms".....alafu unaishia kuuliza "unanipenda kweli?".

Maelezo aliyokupa hakika hayaridhishi au niseme sio sababu ya kutosha ya kumfanya mwanaume mwenye familia na mwenye kujali kushindwa kuwasiliana na mpenzi wake na kumpa taarifa, kwa kifupi huyo mwanaume hana heshima juu yako na wala hajali hisia zako.

*********************************************************************

Siku nyingine tena nilituniwa sms na mwanamke akaniambia "hivi unajijua kua wewe ni bi mdogo tupo tulio anza?" nikamuuliza wewe nani? akajibu "siongei na mbwa naongea na mwenye kufuga mbwa", nikamwambia samahani maana inaonekana mimi ndio kikwazo cha wao kuwa pamoja akajibu "tuko pamoja wewe tu ndio ulikuwa hujui ila sasa umejua naona utapata presha".

Kwakuwa ile namba nilikua naijua toka mwanzo ni mdada ambaye tulikua tunakaa naye jirani ila alishahama nikaacha na naye, mume wangu aliporudi nilimuuliza na kumpa zile sms lakini cha ajabu aligeuka na kuniambia "hamuwezi kuniita mbwa kesho utaniambia vizuri la sivyo nitajiua au nitakuua nikafie jela" niliumia sana haijawahii kutokea.

Tangu siku ile sina tena wivu naye hata kidogo yaani hata akiamua kualala na mwanamke mbele ya macho yangu roho haini umi tena, niko hapa kwa sababu ya mwanangu kwani nampenda sana na sitaki ajeteswa na mama wa kambo.

Dinah anasema: Huna wivu kwa vile hakuna hisia za mapenzi juu ya mwanaume huyo, unajua wivu hujitokeza ikiwa kuna hisia kali za kimapenzi, sasa kama hakuna hisia za kimapenzi wivu utatoka wapi?

**************************************************************************
Imefikia mahali sasa kutoamini mwanaume hata siku moja, labda ashuke toka mbinguni lakini aliye zaliwa na mwanamke hapa Duniani sito thubutu kutoa moyo wangu tena. Huyu ndio aliye niingiza katika ulimwengu wa mapenzi nikamwamini sana lakini kwa sasa
nimemchukia zaidi ya upendo niliokua nao mwanzo.

Naomba mnisaidie ushauri je! niendelee kuishi na huyu mwanaume au ni toke nduki? Maana ninao uwezo mkubwa tu wa kumlea mwanangu bila baba yeke na kumove on with life all alone na sitopenda tena. Lakini nikiondoka mwanangu itakuaje maana sitaki kumuacha kwa kwa baba yake.

Dinah anasema: Huyu mwanaume aliekutambulisha kwenye Ulimwengu wa mapenzi ameumiza hisia zako vibaya mno na ndio maana umepoteza imani kwa wanaume kwa kunadhani kuwa wanaume wote wako hivyo, ukweli ni kuwa sio wote wanatabia za kishamba n akibinafsi. Wapo wanaume wametulia sana kiakili na wanajua kuthamini na kuheshimu wanawake.

Hamjafunga ndoa na huna hisia za kimapenzi juu ya huyu jamaa kutokanana vitendo vyake viovu hakika hakuna cha kupigania hapo ili ndoa isimame Imara! Nakubaliana na wewe kwenye kutoka nduki, tena wala usiangalie nyuma.

Kumbuka kuwa kuzaa sio uzee, wewe ni binti mdogo sana (nadhani unaona kina mama wa miaka 45-60 wanavyolazimisha ujana) sasa imagine wangekuwa na umri wako wa miaka 25? Tunza mtoto wako lakini kumbuka kuwa huyo ni baba wa mtoto wako na hivyo anatakiwa kuchangia matunzo ya mtoto wake na ana haki ya kumuona mtoto au mtoto kumuona baba yake. Hakikisha tofauti zenu zisisababishe mtoto kutomjua baba yake.

*****************************************************************************

Angalizo tu ni kwamba sina ndoa na huyu mtu, ilikua tufunge ndoa lakini mwezi ule ambao tulipaswa tufunge ndoa mama yake alifariki dunia na ndoa ikaahirisha na mpaka sasa hakuna kilichoendelea .

Nilimpenda sana na anauhakika siwezi muacha kwani nilimpa moyo wangu wote nilimfanyia kila kitu alichotaka, nilimtreat kama mtoto akiumwa naomba ruhusa kazini namhandle kama katoto kachanga na mlisha namuogesha namuimbia nyimbo hadi analala.

Inauma jamani ukimpenda mtu alafu akaku dissapoint kiasi hiki, yaani kweli sito penda tena! mwanzo na mwisho kupenda mtu anaye vaaa suruali. Naona niishie hapo maana machozi yanani tiririka kwa uchungu nilio nao kazi njema dada yangu.

Nitafurahi kama niyapata msaada wenu wa mawazo.


Dinah nasema: Pole dada mdogo kwa machungu unayokabiliana nayo, wala usilie kwani huyo mwanaume hastahili machozi kutoka kwa binti mrembo, mwenye kujali, ujuae kupenda na kijana kama wewe. Nimetoa maelezo yangu kutokana na maelezo yako hapo juu.

Ngoja nikupe kisa changu kilichotokea years ago ambacho natumaini kitakusaidia kuelewa situation yako. Mimi nilipokuwa nakua na hata kufikia umri wako nilikuwa mpinzani mkuu wa suala la ndoa, lakini hayo yote yalibadilika baada ya kushawishiwa na kimapenzi.

Wiki mbili kabla ya kufunga ndoa kuna kisa cha kifamilia kikajitokeza, nilikasirika sana na nikaomba ndoa ife, kwamba sikutaka kuolewa tena. Mdogo wangu wakati huo alokuwa na umri kama wako akaniambia " Da' Dinah mshukuru Mungu kuwa Mkasa huu umejitokeza kabla hamjafunga ndoa, huenda ni onyo juu ya huyo mchumba wako".

Nikaendelea kuishi na yule Mjamaa (mchumba) niliekataa kuolewa nae kutokana na issues za kifamilia....then from nowhere jamaa akaanza kuwa abusive(Emotinally as in masimango, lawama zisizokuwa na mwanzo n.k).....ikabidi nitoke nduki bila kuangalia nyuma...Lol! Nikaanza maisha yangu upya kama Mimi kwa kuhama mjini, kubadili kazi namtindo wa maisha yangu na baada ya mwaka na nusu hivi nikakutana na huyu ambae ndio Mume wangu wa sasa ambae ni mwema.

Ninachojaribu kusema hapa ni kuwa kuna mambo Mungu huruhusu yajitokeze ili kutufumbua macho, sasa mama yake alipofariki ndio pazia lilifunguliwa ili wewe uone ukweli wa tabia ya mchumba wako. Imagine mngefungandoa then alafu akaamua kuendelea na tabia zake chafu? Ingekuwa ngumu na ingekuuma zaidi ya inavyokuuma hivi sasa......Mshukuru Mungu amekuonyesha tabia halisi ya Mpenzi wako ambae soon atakuwa Ex.

Natambua kuwa bado unahasira sana, lakini ukijitoa kwenye maisha ya kunyanyasaji kutoka kwa baba mtoto wako utakuwa huru na utapenda tena.

Ni matumaini yangu kuwa maelezo ya wachangiaji wengine na nyongeza ya kisa changu halisi yatasaidia kwa kiasi kikubwa kufanya uamuzi wa busara na kuendelea na maisha yako.

Kila la kheri!

No comments:

Pages