Monday

Hivi tutafunga ndoa au? Mawasiliano Sufuri...

"Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 25 ninamchumba ambaye tuna miaka 2 katika uhusiano wetu, anasema kuwa anatarajia kunioa ila sina uhakika kuwa ni kweli. Mimi nipo Arusha na yeye yupo Dar, ila sina uhakika maana naona siku hizi kapunguza mawasiliano na mimi sio kama mwanzo. Naombeni ushauri wenu kama kweli ananipenda au ananidanganya tu.
Ester."


Jawabu: Ester, asante sana kwa ushirikiano wako. Mchumba wako ndio amesema kuwa anatarajia kukuoa sio kwamba mmepanga (yeye na wewe) kuoana hivyo kufanya nyote wawili kutarajia kufunga ndoa na kuishi pamoja mpaka kifo kiwatenganishe?

Natambua kuwa ni kawaida au asili kwa mwanamke kusubiri mwanaume atangaze ndoa au atake kuoa lakini ktk hali halisi ndoa ni makubaliano ya watu wawili wanaopendana na wenye nia moja ya kwenda kuishi maisha yao pamoja, japokuwa kwenye baadhi ya Jamii wazazi wako ndio wanakubaliana na sio ninyi mpendanao.

Kwenye hili, naona mambo mawili ambayo yanaweza kusababisha hofu yako juu ya u-serious wa mpenzi wako kwako. Mosi, huenda yeye haamini kama kweli unataka kufunga nae ndoa kwani maelezo yako hayajaonyesha wewe kutaka au kutaraji akufanya hivyo bali yeye ndio anatarajia kukuoa.

Pili, umbali kati yenu na gharama za maisha hasa linapokuja suala la mawasiliano inazweza kuwa sababu kubwa ya ninyi kutokuwa na mawasiliano ya mara kwa mara kama ilivyokuwa huko mwanzo, pia kunauwezekano mkubwa kuwa unasubiri yeye ndio awasiliane na wewe na sio kuwa mnawasiliana kwa maana ya wewe una-check nae na yeye anafanya hivyo. Inaonyesha yeye ndio mtendaji mkuu kwenye uhusiano wenu hali inayoweza kusababisha uchovu na yeye kuhisi kuwa anafanya too much na wewe kazi yako ni kusubiri tu.

Uhusiano wowote wa kimapenzi unajengwa/boreshwa kwa kuzingatia nguzo kuu tano na moja kati ya hizo ni kushirikiana, ninaposema kushirikiana ninamaanisha kiuchumi, kihisia, kimwili, kimawazo na maamuzi. Nasikitikakusema kuwa kutokana na maelezo yako hakuna dalili ya ushirikiano kwenye uhusiano wenu na vile vile mawasiliano sio mazuri sana kutokana na umbali kati yenu.

Kitu muhimu cha kufanya ili ujue kuwa jamaa hakudangaji juu ya suala la kufunga ndoa na wewe, ni wewe kujitahidi na make an effort kwenye uhusiano wenu hasa linapokuja suala la mawasiliano, zungumza nae kuhusiana na ahadi yake na sasa ifanye iwe ahadi yenu kwamba mnaahidiana kufunga ndoa na hakikisha unamshawishi afanye kweli kwa kuchumbia kwenu na sio kuishia kusema tu "nitakuoa", "lazima nikuoe", "natarajiakukuoa" au "wewe mchumba wangu".

Suala la yeye kukupenda au kukudanganya nadhani itakuwa ngumu kwangu mimi na wasomaji wangu kujua kwani hujatueleza kwa undani na kwa uwazi zaidi, wewe Ester ndio mtu pekee unaeweza kujua kama Mchumba wako anakupenda kwa kuzisoma hisia zake, ukaribu wake kwako, anavyoku-treat n.k.

Tafadhali zingatia hayo machache niliyokueleza na mengine kutoka kwa wachangiaji wangu na ujaribu kuyafanyia kazi ili kufanikisha kile ukitakacho kutoka kwenye uhusiano wako. Kwa case yako ni ndoa basi hakikisha unafanyia kazi uhusiano wako ili kupata hiyo ndoa....kwa mbinu zaidi kama utahitaji basi unaweza kurudi tena mahali hapa.

Kila la kheri!

No comments:

Pages