Saturday

Ndugu wanahatarisha Ndoa yangu-Ushauri

"Habari za kazi dada yetu mpendwa, baada ya kusoma ile stori ya kaka aliyemsaidia mdogoe na kisha kumpindua, nikaona nami niseme yaliyonisibu.

Mimi ni mdada wa 29 umri, nimebahatika kuolewa miaka 8 iliyo pita. Namshukuru mungu nina amani na ndoa yangu. Nia ya kuja hapa ni kutaka kujua hawa ndugu wadogo wa damu, binamu, mashangazi na wengineo tunao wakaribisha majumbani kwetu na kuwaonesha upendo wa juu na baadae kuharibu je tuwafanyaje?


Dinah mimi naweza kusema mume wangu kidogo Mungu kamjalia si sana ila kiasi cha pesa kwa mwezi mshahara unaridhisha. Sisi katika hili nikaona kwanini nisimwendeleze mdogo wangu Juma nimsimamie mpaka atakapo maliza miaka yake 3 au 4 ya chuo bila kuchukua mikopo.

Nikampanga mume wangu naye akaona ok, huruma bado ikaja kwanini huyu Hadija naye nisimtoe, ok kutokana na mambo mengineyo kama mwanamke au matatizo ya kwenu si kila mara unakuwa unamwambia mumeo utacho kwa bure, basi nikawa nafanya siri nikampangia H, chumba pale makumbusho huku akiwa ni waiter kwenye hotel.

Basi ikawa ndio mtindo kodi ikiisha anakimbilia kwa daad, baadae H akajisahau akaamua kuacha Uweitress, ikawa ndio mzigo unaongezeka zaidi kwani pamoja na kumlipia chumba kila mara ilinibidi pia kumpa pesa ya matumizi. Baadae nikasikia anaboyfriend ambaye kula kulala hana kazi ila yeye H ndio anamtake care, sio siri dada, roho iliniuma sana yaani miim nimpe pesa ya matumizi tena akamuonge boyfriend wake wakati wazazi wangu kijijini wanakaa bila matumizi ya kutosha.


Si ikabidi nikae nae chini na kunimuliza H mbona nasikia hivi na hivi, unajua yeye anaongea sana na mtundu mtundu kuliko mimi ila utundu wake si wakimaisha, majibu aliyonipa ni "hee kwani wewe utombwi? unataka nisitombw? wewe ulivyomleta bwana wako nani alikushauri, mume mwenyewe sura mbaya".


Dinah, nilishindwa kuvumilia nikamjibu kwa hasira "sura mbaya mbona pesa zake wazifutafuta?" pia nikamjibu "hao mahandsome nikiwataka ni wapo kibao pesa ninayo nikiamua namchukua napiga pamba anatoka, pamoja na sura mbaya ya mume wangu ila hatulali njaa huyo handsome utakula sura yake huko ndani? kwanza kwa huhandsome gani kiboy friend chenywewe sura mbaya, pesa ya kula hana, wa nini ?" nikamaliza. Basi yakawa malumbano, kitu ambacho kiliniuma sana.


Basada ya muda kupitai tukayasahau hayo yote, akawa na interest ya saloon nikaona njia bora ni kumpatia mtaji wa hicho akipendacho ili azuie kuomba matumizi kwangu. Nikajikaza nikatoa kama milioni 3 anunue vifaa pamoja na kukodi sehemu, kwani baada ya mwaka tena si mkataba ukaisha akawa hana tena pesa ya kurudia kulipia.


Mimi nikauchuna nikamjibu ukitaka funga rudi kwa wazazi kijijini nimechoka. Mwaka ukakata hana chanel nikamwita nikamwambie kasome upendacho ,nikalipa ada ya miezi sita kaenda shule mwezi mmoja tu, nikamuliza kunani? Akasema "ooh mimi sitaki kusoma" kwa sababu alishanunua vifaa vya salooni nikamomba atafute tena frem nitamlipia mwaka na nitampa tena mtaji wa madawa ya saloon, kweli alipata frem sayansi kwa mwaka laki 8 pamoja na bla bla milioni1.2 .

Jamani hata kufungua kinywa na kusema asante, nilibaki naduaa. Kuna siku anakaa na kumsifia ndugu yetu mmoja ambaye alishaolewa miaka 15 iliyopita ee wamejenga, wewe sijui utajenga lini? hao hao wamejisahau kuwa ndio chanzo cha kutokujenga kwangu kuwaangalia wao wamekula nini wamevaa nini watafua na nini, alafu mtu anakuja anakupitia wewe kimafumbo.


Mbaya zaidi huyu ni mdogo wangu wa damu toka nitoke hana udogo wa sana kupishana kwetu miaka 2 tu. Si huyu tu Dinah nimemtaja huyu kwasababu wa damu, nimemseidia binamu, akatoka kunisimanga kwa watu, ni wengi ndugu waliopata msaada wangu ila naambulia kutetwa na kusimangwa.


Hebu nielekezeni niishi vipi na hawa ndugu? Sometimes nasema hili nalifumbia macho ila utakuta roho inanisuta nkuona haifai, pia wanaponizidi nawaeleza mimi si tajiri wa hivyo wanvyofikiria siwezi kusaidia kila mtu, kwani hata Kikwete ana ndugu ambaao hawezi watosheleza itakuwa mimi kapuku?


Kuna baadhi ya Makabila wakiona na unaishi kwenye nyumba kubwa, gari 2, 3 zinapumua garden, basi kila mmoja anataka kuishi kwako.hususani kabila la ........ni hayo tu Dinah na wachangiaji wengine, naomba mnishauri nifanyenini ili dungu wasije haribu ndoa yangu?"


Jawabu:Hihihihi ni kweli kuna Makabila Fulani Fulani akyanani huwa wanaamia na ukishangaa-shangaa na mumeo wanachukua, tena basi wengine hata undugu wenye ulipoanzia wala hujui. Mbaya zaidi hawajali kama umepanga au umejenga, kinachoudhi hata kama unachumba kimoja wako radhi kulala jikoni au kwenye upenyo ilimradi tu wakuharibie uhuru na mumeo.....tuliache hilo!


Shukrani kwa ushirikiano wako na uvumilivu kwa kipindi ambacho nilikuwa nahamisha makazi. Suala lako sio geni miongoni mwetu au niseme kwenye sehemukubwa ya jamii nyingi za kiafrika, ndio kitu pekee kinatufanye tuwe tofauti na jamii nyingine Duniani kitu hicho ni “Family values”.


Ni wazi kabisa kama wewe ni mkubwa kwenye familia yenu unalelewa ktkmazingira ya kuwa mfano kwa wadogo zako, kuwa kiongozi wao na pale unapokuwa mtu mzina na kuanza maisha yako unahisi kuwa na majukumu Fulani juu ya ndugu zako na vilevile kuna kahatia Fulani unahisi ka kusaidia wazazi hasa kama hawana kipato au umri umekimbia (wazee).


Kitu ambacho huwa tunashindwa kukivumbua kama alivyosema mmoja kati ya wachangiaji ni kuwa kuzaliwa tumbo moja kwa maana ya baba na mama moja haina maana kuwa mtakuwa na uwezo wa kufikiri wa aina moja, upendo na kuthamini wengine in the same way.....ndio ni ndugu wa damu lakini tukumbuke sote ni “individuals” na tunafanya mambo “individually”.



Nia na madhumuni yako ilikuwa kumsimamamisha mdogo wako lakini kwa bahati mbaya hana shukurani na wala hathamini jihudi zako za kutaka kumsimamisha kimaisha ili ajitegemee nap engine awe na kidogo kama wewe au kama akiongeza bidii basi afanye makubwa zaidi ili asaidie wengine.


Kuna ndugu ambao huwa na mafanikio lakini huwa wawasaidii wenzo kijikwamua na badala yake huwapa samaki wenzao na sio nyavu kama alivyo gusia mchangiaji mwingine hapo kwenye maoni (nimependa sana msemo wako Kaka uliyesema mpe nyavu akavue samaki na sio kumpa samaki kwani atarudi tena kuomba samaki).


Sasa wapo watu wanahisi fahari kuombwa-ombwa kila kukicha na ili kuhakikisha hilo linaendelea watakuwa wanakupa “samaki” badala ya kukupa “nyavu” ukavue Samaki utakao. Wewe dada yangu ulitoa samaki na kisha Nyavu lakini mdogo wako anazidi kukurudisha nyuma kimaendeleo na kuonyesha kuwa hajali anakucheka kuwa unashangaa tu wakati wenzako wana majumba.


Hey, hakuna radhi ya ndugu si ndio?!! Timua huyo mdogo wako asie na heshima, adabu wa shukurani, na sasa “focus” kwenye familia yako, linda ndoa yako kwa kutumia muda mwingi na mumeo badala ya kufikiria hao wanandugu wajinga-wajinga, andaa maisha ya watoto wako ambao ndio wajibu wako na ukishangaa sasa na jambo likatokea ujue hao ndugu zako watasimamnga na kusumbua watoto wako kama wanavyokufanyia wewe hivyo mama changamka na anza kuwarekebishia maish ayao ya baadae hivi sasa.

Huyo mdogo wako ni mtu mzima na anapaswa kuendesha maisha yake kivyake.

Kila lililo jema mdada.

No comments:

Pages