Thursday

Miaka 5 na Mume wa Mtu-Ushuhuda

MIAKA MITANO NA MUME WA MTU - USHUHUDAPole da dinah kwa kazi ngumu ya kuelimisha jamii. Nakumbuka mada hiyo hapo juu niliitoa mwaka jana ila nashukuru kuna walionipa ushauri mzuri nikaweza kufanikiwa japo kuna walioniponda.


Dada yangu nimeamua kusalimu amri nimeshaachana na mume wa watu na kuamua kukaa kutulia kuhangaika na maisha yangu huku nikimwomba Mungu anisamehe sana. Ila nahitaji ushauri nini cha kufanya kwa sababu jamaa kakataa kuwaweka wazi kwa ndugu zake na hata mkewe kuwa hayuko na mimi.


Tena anasema walivojua tunauhusiano ndo watakavojua tumeachana sasa kinanishinda kitu kimoja coz mkewe ananitumia sms za matusi kila kukicha, mara anapiga simu nashindwa la kufanya sipokei wala kujibu Je nifanyeje ili huyu mwanamke asiendelee kunisumbua na ajue its over me na husbad wake? Naomba ushauri wako dada pamoja na wachangiaji wote.
Niwatakie siku njema"

Jawabu:Asante sana kwa kurudi tena na kutuma "feedback". Miaka mitano sio "kitoto" yeye huyo mwanaume mwenye tabia chafu haamini kabisa kuwa wewe kama mwanamke unaejiamini umesimama na kumwambia sasa imetosha na kila mtu achukue ustaarabu wake.


Sio wanawake wengiwa Kibongo wenye kujiamini kama ulivyoamua kuwa wewe hasa ukizingatia mume huyo wa mtu alikuwa akikuangalia ktk hjaliz zote hasa kiuchumi. Hali ya yeye kukufanyia kila kitu ali-relax nakujua kuwa "imetoka" yaani huwezi kuacha maraha anayokupa na mapesa na ndio maana hataki kabisa kuliweka wazi hilo kwa ndugu na jamaa zake. Chukulia kuwa hilo ni tatizo lake na anapaswa kurekebisha mambo na mkewe ili apate kile alichokuwa akikifuata kwako.

Huyo mwanamke anahasira sana na wewe, kama ambavyo mwanamke yeyote angeweza kujisikia baada ya kuibiwa mumewe. Tofauti ni kuwa mwanamke huyu badala ya kufanyia kazi suala zima la kwanini hasa mumewe alitoka na wewe kwa kipindi kirefu hivyo na kujaribu kujirekebisha na kuimarisha ndoa yake anapoteza muda kukutukana wewe....again chukulia kuwa hilo ni tatizo lake kwani wewe umekwisha nawa mikono na huusiki na lolote linalotokea kwenye uhusiano wao hivi sasa.

Kutokupokea wala kujibu ni uamuzi mzuri sana, sasa ilikuondoa usumbufu wa huyo mwanamke badilisha nambari yako ya simu na hakikisha hakuna mtu kutoka pande hiyo anaijua nambari mpya hiyo.

Kuwa na siku nzuri.

No comments:

Pages