Monday

Nikirudi Bongo ndio itakuwa basi?-Ushauri

"Dada dinah pole na kazi, naomba niingie moja kwa moja na kile kilichi nileta hapa.
Dinah nina mpenzi ambaye tumeahidiana kuoana ingawa wote tuko shule mimi niko mwaka wa mwisho yeye bado kama miaka miwili hivi, na wakati wote huo tuko karibu sana kama mke na mume na tuko ughaibuni.


Tatizo ni kwamba tumekua tukigombana mara kwa mara na tunapatana wenyewe bila kumshilikisha mtu na kibaya zaidi huyu mwenzangu hua hajui kusema samahani hata kama anajua amekukosea, kiasi kwamba mtu unapata hasira.Mtu amekukosea halafu haombi msamahaa.


Siku zingine hua tunapigana kabisa kutokana kwamba yeye hataki kujishusha na mimi kama mwanaume sipendi kudharaulika mwisho wa siku tunaanza kupigana, Mbali na hayo inaonyesha kila mtu anampenda mwenzie kiasi kwamba hayuko tayari kumuacha.


Na kingine ni kwamba huyu mpenzi wangu ameumbika kidogo mungu kamjaalia.Na kipindi chote hiki nilichokua nae kweli tumefurahia mapenzi ingawa kuna ugomvi wa hapa na pale. Wanaume wengi wamemtaka lakini wote huishia kugonga patupu na wengi wanasubiri mimi niondoke baada ya kumaliza shule ndo wamtake kwani wanamwambia laivu ku wanasubiri niondoke.


Hapo ndio ninapoingiwa na wasiwasi je nikiondoka ataweza kuvumilia kweli?au ndo ahadi yetu itakua imekufa? pamoja na hayo namwamini sana lakini najua kuna kutereza, na mimi sipendi kuchangia hasa ukizingatia tumekuwa pamoja kwa muda wa miaka miwili na miezi sita sasa na baadhi ya ndugu wanajua uhusiano wetu.


Kipindi chote hicho wote tumekua sio watu wa kujirusha sana na wala hatutumii any alchohol. JE DADA DINAH NIWE NA MATUMAINI AU NDIO BAI BAI MAANA NATAKA KUJUA ILI NISIPOTEZE MUDA.

Naomba ushauri dinah na wadau wengine wa blog hii
thanx".

Jawabu:Asante sana kwa pole zako kwani zimefika wakati muafanya kwa vilemajukumu yameniandama sana tangu mwaka huu uanze lakini najaribu kujigawa kimtindo.

Sasa jamani mapenzi gani hayo ya kupigana magumi kwa vile mmoja hataki kudharauliwa na mwingine hataki kuwa chini? Hata siku moja haiwezekani mtu ajiweke chini kwani akifanya hivyo utamdharau kama ambavyo wewe hutaki. Kwanini wewe usiwe mstaarabu ukakaa kimya wakati yeye analalamika na akimaliza mpe jibu zuri, kwa upole na upendo badala ya kuinua mkono na kumdunda mwenzio ambae ni mwanake?.....tuliache hilo.


Suala la wewe kutaka kujua kama ni kweheri au usubiri unapaswa kumuuliza yeye mpenzi wako. Zungumzzeni kuhusiana na maisha yenu ya baadae na mipango yenu kama wapenzi. Weka wazi hofu na wasiwasi ulionao juu yake pale utakapokuwa unarudi Nyumbani na kumuacha yeye huko.

Mawasiliano ndio njia pekee ya kujua umesimama wai kwenye uhusiano wenu, mazungumzo yenu yakina yatakusaidia kufanya maamuzi ya busara iwe ni kusubiri au kuendelea namaisha yako kivyako.

Kuwa na mpenzi au kuwa kwenye uhusiano hakuzuii watu wengine kukutamani, kama mzuri anavutia na amejaaliwa umbile zuri kwanini asitamaniwe?!! Kutamaniwa haina maana kuwa mpenzi wako atatereza na kila atakae mtamani.....jivunie uzuri wa mpenzi wako ambao unavutia watu wengine.
Kila la kheri!

No comments:

Pages