Tuesday

Miezi 2 tayari ndoa imekuwa ndoano-Ushuhuda!

"Dada Dinah na kushukuru sana kwa kuweka hii blog kweli inatusaidia, ,mimi ni yule dada niliye omba ushauri hapa heading ikiwa miezi miwili tayari ndoa imekua ndoano. Jamani ninawashukuru wote mliochangia mada maana ushauri wenu niliuchukua nakuufanyia kazi kwa kweli nimeona mabandikiko makubwa sana.


Ninasema asante na ninaomba mzipokee shukrani zangu za dhati. Niliongea na mume wangu nikamueleza ukweli kua mwanae nilinaye tmboni ananisababisha nichoke sana na mwili muda wote umelegea legea nikamueleza kua hatamasharti anayonipa yananipa wakati mgumu najikuta nina waza muda wote kwa kweli nashukuru maana sikuamini kama ange-react namna ile kwanza alilia sana nakuomba msamaha kwangu lakini pia alimuomba mwanae pia kama vile anamsikia.


Sikuamini na kuanzia siku ile ananisaidia kupika kama napika ugali basi yeye anapika mboga wakati mwingine nikirudi nakuta kasha pika kipo mezani yani nafurahia kwakweli maana siku akiona sijakaa sawa basi hata kuogeshwa wakati mwingine nikirudi nakuta ameshafua nguo zote kazikunja vizuri.

Kwakweli sikujua kama angeweza kubadilika namna hii, kama siku za weekend yupo off basi saa kumi na moja anakuamsha mama twende tukafue mapema ili upatemda wakupumzika, akiona unafanya kazi sana bila kupumzika ,unashangaa anakuita njoo chumbani ukifika unaambiwa njoo mama nifundishe kuimba huu wimbo au hebu niangalie kuna kipele mgongoni basi tu ili akupe muda upumzike, kweli kilio changu kimegeuka kuwa furaha muda wote .

Dada Dinah ninakushukuru sana kwa ushauri wako na wachangiaji wote mungu awabariki . "

Dinah anasema: Hongera sana kwa kufanikiwa hilo. Tubarikiwe sote!

No comments:

Pages