Thursday

Mume wangu hataki tuzae-Ushauri!

"Habari dada dinah na wasomaji wengine, naomba msaada wenu wa ushauri na samahani kwa maelezo marefu. Mimi nina umri wa miaka 28 na mume wangu 37. Tunaishi Europe. Niko kwenye ndoa miaka 2.


Tulikubaliana na mume wangu tusizae kwa muda fulani kwasababu ya gharama tulizopata wakati wa harusi na pia ili tujenge. Muda wa kutozaa unaisha mwezi wa 12 hivyo ikifika muda huo natakiwa kutiana kwa nguvu zote ili nimimbike.


Kuna siku nilimkumbushia mume wangu kuhusu muda wa kupata mimba unakaribia hivyo tuanze kujiandaa, akawa mkali na kuniambia nisahau kitu kuzaa kwasasa kwasababu ana majukumu mengine ya kuwasomesha wadogo zake wawili ambao ni mtoto wa kaka yake na masikini mmoja anamsaidia na mtoto wake alimzaa na mtu mwingine alipokuwa chuoni.


Mimi nikamwambia anaweza kupunguza majuku kwa kuwaachia ndugu zake mdogo wao mmoja na yeye akabaki na mdogo mmoja kwasababu kwao wako 9 na huyo mtoto wa kaka yake amuachie kaka yake amsomeshe mwanae ili na sisi tuzae wa kwetu na tujenge na kufanya mipango mingine akanambia hatofanya hivyo kama siwezi kusubiri majukumu yaishe nitafute mwanaume asiye na majukumu nizae nae.


Ndugu zake wengine wanauwezo wa kawaida mbao yeye ameshawasaidia kwani alishawapa mtaji wabiashara, na kuwajengea nyumba ya familia na pia mambo mengi anawasaidia. Jamani nisaidieni sielewi nifanye nini. Na nimeshaambiwa nitafute mwanaume mwingine, kuzaa nataka na ndoa yangu sitaki ivunjike"

Jawabu:Asante sana kwa barua pepe yako, nadhani mumeo alijibu kwa hasira kwa kufikiria kuwa kwa vile tu amekuoa unataka asahau familia yake (kumbuka umeolewa miaka 2 tu) hivyo majukumu yake aliyonayo aliyaanza kabla yako na hivyo hana buni kuyamaliza. Yeye kama mwanaume tena wa Kibongo haitaji mwanake kumuambia nini cha kufanya hasa linapokuja suala la ndugu zake. Hivyo basi tamko lake la kutafuta mume mwingine usilitilie maanani.


Katika mambo yote kwenye uhusiano wowote wa kimapenzi hata siku moja usiingilie mambo ya familia ya mwenzio, hata kama atakuomba ushauri hakikisha unampa ushauri utakaomsaidia na kwamwe usiponde ndugu zake hata kama wamemuumiza mumeo na badala yake msikilize, mpe matumaini na kumtuliza hata siku moja usijarubu kujiingiza kwenye masuala ambayo wewe hayakuhusu......hujui makubaliano yako kama Familia.


Badala ya kumuambia mumeo apunguze majukumu ulitakiwa kumwambia kuwa "kipato changu" kinatosha kusaidia majukumu mengine yakiongezeka moyoni ukimaanisha kuwa unataka mzae, lakini kama kila kitu ni juu yake inamuuwia vigumu hasa ukizingatia kulea mtoto Ulaya sio lele mama kwa maana ya kiuchumi.

Natambua unavyojisikia na hofu yako ya kuchelewa kuzaa, wewe bado kijana ungekuwa na umri wa miaka 33 na ukawa na hofu hiyo ya kuzaa ningekuelewa, lakini kumbuka unaweza kufurahia maisha yenu ya ndoa bila kuwa na mtoto mpaka pale mtakapokuwa tayari na kuwa na uhakika wa kufanya hivyo.


Najua wanawake wa Kibongo kuzaa wanaona mwisho wa matatizo au njia pekee ya kulinda ndoa kama sio kum-keep mwanaume, yaani wewe kuwa mwanamke basi ni lazima uzae lakini wanasahau kuwa (1) Ni majaaliwa na (2) Ni chaguo la mtu. Kuzaa sio lazima na haijalishi una umri gani kama Mungu alitaka siku moja uwe na familia basi itakuwa hivyo.


Hivyo mdada tulizana, acha kujipa mawazo bila sababu ya msingi, furahia maish ayako ya ndoa, Mpe ushirikiano mumeo ktk kukabiliana na Majukumu uliyomkuta nao ili kumpunguzia stress, fanya bidii kwenye shughuli zako kiuchumi ili kukusanya senti kwa ajili ya mtoto atakae zaliwa, pale mtakapo elewana kufanya hivyo.

Ukimuonyesha mapenzi, ukiwa mwenye furaha, ukijitahidi kumuondolea stress na kushirikiana nae ktk kila jambo bilakujiingiza sana kwenye masuala ya familia yake, hakika mumeo atapata ujumbe na kama ni mtoto ndio unataka basi atakupatia......tumia uanamke wako kupata utakacho.


Pssst! Usikute hana uwezo wa kuzaa ila anashindwa kukuambia, mana'ke wanaume wakikaribia miaka 40 huwa na haraka sana ya kuzaa no matter what kama unahisi the same basi baada ya mwezi wa 12 tumia ila mbinu ya "kumtegeshea" siku za hatari na usiposhika mimba utajua ukweli na ukishika basi utakuwa umepata ulichokitaka.

Ikiwa unatumia aina yeyote ya dawa za kuzuia mimba basi ni wakati wa kuacha na kutumia njia asilia au Condoms ili kujiweka sawa kushika mimba hapo baadae.

Kila la kheri.

No comments:

Pages