Tuesday

Kanitambulisha kwao, anamtu yaani sielewi-Ushauri

"Jamani me dada Dinah nina jambo ila sifahamu tu wapi ni kutumie kwa mail gani lakini hii issue imekaa hivi: Mimi nina mpenzi ambae tunapenda sana sana na siku ya kwanza alivyoniona tu akawaambia ndugu zake kuwa ameshapata mke yule ambae anamuhitaji na kumuelezea mama yake mzazi. Mimi nimekuja kuambiwa na Binamu yake kuwa najulikana kabisa home cha kushangaza hajaniambia chochote hiyo moja.

Pili huyu anamtu amezaa nae na uzuri ameshaniambia kama anamtoto kinachoniuma mpaka leo wanaendelea kula bata mimi roho inaniuma sana sana sio siri, mtihani ulionipata ni kwamba nilimpigia simu kama mara 4 hivi hajapokea imepita masaa kadhaa anipigia na kunifokea "we si unajua kama niko na huyu mwanamke kinachokufanya upige non stop nini? sipendi mgambane ndio mana nimeamua kutopokea simu yako"


Kwa kweli imeniuma sana huwa hasemi lakini siku hiyo alinidhihirishia kabisa kwamba asipo pokea simu yangu nielewa tu yuko na huyo mwanamke. Niligomba sana pasipo kujibu neno lolote haikutosha nilituma msg za kumkashifu mwanamke pamoja na yeye yote ni hasira tu, nikawa kimya na yeye kimya.


Nikajirudi kwa kuona kimya kimezidi, na chat nae tuna story kama kawaida lakini hana mapenzi tena na mimi yaani inaniuma sana sana kumkosa. Alikua akinipa gudtime sana sikua nikipiga simu kwake yeye ndio alikua akipiga lakini sasa mimi ndio napiga na nisipopiga yeye hapigi. Nikituma msg za malalamiko kwanini anafanya hivyo? yeye hanijibu.

Sasa hapa sielewi kanimwaga au vipi ni bora anitamkie tu kama hataki kuendelea na mimi lakini si kukaa kimyaa jamani inauma sio siri kukaa kimyaa ina maanisha nini jamani mbona mwenzenu niko njia panda?

Naombeni ushauri nifanye nini?"

Dinah anasema;Pale ulipolitumia ndio mwake kabisa, shukrani kwa ushirikiano wako.
Kutokana na maelezo yako inaelekea sehemu ya familia ya jamaa yako hasa Mama yake kama ulivyogusia hawampendi huyo mwanamke aliyezaa nae sasa ktk kuwazuga ikabidi atafute mwanamke mwingine ambae ndio wewe na kumtambulisha kwa Mama yake huenda ni kwa jina, picha, au kwa mbali yaani unakatiza kwa mbali mtu anaonyeshwa "yule dada ndio mpenzi wangu nataka kuoa".

Kuna uwezekano mkubwa kabisa kafanya hivyo ili asipate "radhi" ya mama'ke au anataka tu kumfanya mama yake apunguze kidomodomo ili yeye na mama watoto wake waendelee kuishi vema. Kinachosikitisha ni kuwa wewe umezama kwenye mapenzi na mwanaume wa mwanamke mwenzio kwa maana nyingine inakuwa kama vile umeingilia mapenzi yao (well hii ndio itawajia kichwani wanawake wengi) lakini ktk hali halisi haikuwa hivyo, wewe ulipendwa na kijana huyo kisha ukampenda alafu ndio ukajatambulishwa kuwa kuna mwenzio ambae amezaa nae.


Ulichokosea hapo ni kuendelea na uhusiano na huyo Njemba huku ukijua kabisa kuwa unachangia na mwenye mali (aliyezaa nae) na mara kwa mara anakuwa huko na anathubutu kukufokea kabisa kuwa "unajua niko na yule mwanamke, kinakufanya unipigie non stop nini ?"hapo ni wazi kuwa hajali hisia zako na hakuthamini wewe kama mpenzi wake. Siku hiyo ungenawa mikono kutoka kwenye uhusiano huo.


Sio lazima mtu akutamkie kuwa hakutaki au hataki kuwa na wewe, wakati mwingine unasaoma vitendo vyake (Mf, kutokupokea au kukupigia simu), namna anavyoku-treat(Mf,anakufokea) na kadhalika. Huyu Jamaa hakuhitaji tena, kwani alichokitaka tayari kimepatikana nacho ni kufunika ukweli kwa Mama yake kuwa yeye bado anaendeleza uhusiano na mzazi mwenzie.


Natambua unavyojisikia, nafahamu maumivu ya kimapenzi unayokabiliana nayo lakini ni vema kuumia sasa na kujitahidi kumsahau huyo jamaa, kuyasahau yote mliyokuwa mkiyafanya pamoja kama wapenzi.

Njia nzuri ya kumsahau ni kumchukulia kuwa ni "kicheche", kumbuka kuna UKIMWI, fikiria.....kama ingekuwa wewe ndio umezaa na huyo jamaa alafu kijimwanamke kingine kinamsumbua bwana wako kwa simu ungejisikiaje?

Mungu atakusaidia na utasahau kila kitu na utakutana na Kijana mwingine asiye na mtu.
Kila la kheri.

No comments:

Pages