Thursday

It's Two!!


Leo ni Siku na Mwezi ambapo D'hicious inasheherekea Miaka miwili tangu ianzishwe. Siku hii ni maalumu (Special) sana kwangu, sio kwavile ni muanzilishi wa Dinahicious Blog/Live na labda mwanamke wa kwanza kuzungumzia "Unyago" kwa uwazi na kwa faida ya kila mtu (wake kwa waume) bali pia tarehe kama hii kuna tukio muhimu sana lililo badilisha maisha yangu lilitokea hivyo basi ninafuraha sana.....miaka 2! Huh!
Kabla sijasema mengi napenda kuchukua nafasi hii kutoa shukurani zangu za dhati kwako wewe Msomaji, Mchangiaji, Msikilizaji wa Bongo Radio na Muuliza maswali, wote kwa pamoja ndio mnaifanya D'hicious Blog/live kuendelea kuwepo. Pia shukrani kwako wewe uliyoiweka D'hicious kwenye blogs/tovuti yako.

D'hicious imefanikiwa kwa kiasi kikubwa tangu ianzishwe miaka miwili iliyopita. Dinahicious imerudisha mahusiano mengi ambayo yalivunjika au yalikuwa yakielekea kuvunjika. Dinahicious imefanikisha baadhi ya wasomaji wake kufanikiwa kushika Mimba na kuzaa kwa kutumia njia asilia kabisa.

Dinahicious imerudisha ndoa na kuboresha ndoa nyingi, Dinahicious "imesababisha" watu kupata wapenzi na hatimae kufunga ndoa kwa kutumia mbinu zilizoelezwa mahali hapa, vilevile D'hicious imefanikisha wake kwa waume kubadili mienendo yao na kufurahia maisha na mafanikio makubwa kupita yote ni kwa Jamii ya Kibongo taratibu sasa inakubali kuzungumzia Ngono, Mahusiano na Mapenzi kwa uwazi bila uoga wala aibu.

Dinahicious ilivyoanza hakukuwa na blog au tovuti ya Kiswahili yenye kuzungumzia Ngono kwa uwazi katika mtindo wa kufundisha na kukumbusha. Lakini hivi sasa hali ni tofauti kwani wengi wameibuka na kujisikia huru kuizungumzia ngono bila aibu.....ni mafanikio makubwa kwa upande wangu na ninahisi faraja sana kuona kuwa, kwa kufanya kitu kidogo tu nimeweza kusababisha mabadiliko kwenye sehemu fulani ya Jamii yangu ya Kibongo.

Kama ambavyo mmeshuhudia tangu kuanza kwa mwaka huu kumekuwa na mabadiliko kwa maana kuwa, nimekuwa nikijibu maswali zaidi kuliko kutoa mafunzo kama ilivyokuwa hapo awali. Hii yote sio tu kutokana na uwingi wa maswali ninayopokea bali pia ni kwasababu matumizi mabaya ya kazi zangu.

Baadhi ya Magazeti ya Udaku na Blogs wamekuwa wakitumia kazi zangu bila kuweka vielelezo kuwa wametoa kwangu au kuweka anuani ya D'hicious, sasa ili kupunguza matumizi mabaya ya kazi zangu nimeamua kufanya mafunzo kwa njia ya sauti (radio) na sio maandishi (blog).

Kwa maana hiyo basi D'hicous itaendela ku-publish maswali yote ninayopokea na nitakuwa nayajibu kwa uwazi kabisa kama kawaida yangu na mafunzo yataendela kupatikana Radioni.

Juma Pili hii kutakuwa na kipindi maalum radioni kwa ajili ya kuadhimisha Miaka miwili ya blog na kipindi chenyewe, unakaribishwa sana ili kutoa mchango wako kwa njia ya simu.

Mungu aendelee kukupa uzima na endelea kujikumbusha/kujifunza mambo muhimu ili kuboresha uhusiano wako wa kimapenzi kupitia D'hicious blog/live.

**GQ, Dj Dennis, Mpenzi Mume wangu na SamChom bila ninyi heri nitoweke Duniani.

Mwisho mzuri wa wiki,
Asante sana.

No comments:

Pages