Saturday

Mume ni "control freak" nifanyaje aache?-Ushauri

"Hi dada dinah, pole na mizunguko kazi na maswali mengine magumu hata kuyatatua mwenyewe. Mimi ni mama mwenye mtoto mmja nimeolewa nina miaka minne katika ndoa yangu nilizaliwa miaka kadhaa iliyopita but not below 23.


Mimi na mume wangu tulikua tuna pendana sana na mpaka sasa mimi bado nampenda tena sana. Dada Dinah tatizo langu kubwa kwa mume wangu ni kwamba simuelewi kwani tangu tumeanza kuishi pamoja hataki mimi niende nyumbani kwetu wala niwasiliane na ndugu zangu ila kwao na kuwasiliana na ndugu zake hanizuii.


Nimejaribu kumtumia mama yangu amuombe niende lakini bado anatoa sababu, kwa mfano mama alimuomba niende kuwaona mume wangu akasema muda bado. Muda ulipo fika akatafuta safari akaniaacha mimi nikashidwa kuondoka.

Dinah anasema; Nadhani hii tabia yake ya kukukataza wewe kwenda kwenu ni uoga unaoweza kusababishwa na uzoefu mbaya kutoka kwa watu wengine wanaomhusu, huenda ikawa ex's au hata ndugu jamaa na marafiki ambao wapenzi/wake zao walikuwa wakitumia kisingizo cha kwenda "kuwaona nyumbani" na huko walikuwa wakifanya mambo machafu.


Natambua kwenda nyumbani ni muhimu na wazazi wako wangependa kukuona sio tu wewe bali hata wajukuu zao lakini kama inashindikana kutokana na kutojiamini kwa mume wako basi jaribu kumshawishi muende wote kuwaona nyumbani, ikishindikana basi waombe ndugu zake waje kukutembelea nyumbani kwako.

Umesema kuwa unampenda mumeo, kama kweli unampenda basi jaribu kumuelewa. Yeye kama mwanaume wa Kibongo hata siku moja hawezi kukueleza yaliyomkuta huko nyuma hasa kama yalihusu mpenzi wake wa zamani au yanahusisha yeye kuonekana muoga wa "kuchezewa denge" na wajanja.

********************************************************************************

Pili siku hizi kabadilika sana kiasi najuta hata kuolewa yaani kidogo kanitukana mara mshenzi mara mjinga mara ananitisha kunipiga kwa kusema mimi simjui vizuri ndio maana nashindwa kufanya atakavyo, ukweli ninachanganyikiwa mume wangu anakuwa kigeugeu anaweza akakwambia mimi sipendi uvaenguo ndefu ukivaa fupi kwa muda huo aliosema anafurahi sasa itokee siku nyingine akuambie tutoke ukivaa hiyo nguo fupi anaanza unaenda kumuonyesha nani? unatakautongozwe kwani mimi sikutoshi? ukivaa ndefu au suruali ananyamaza.

Dinah anasema; Mumeo anaamini ktk umilikishi, pamoja na kusema hivyo uhusiano wenu unakosa mawasiliano kitu ambacho ni muhimu sana ili yeye akuelewe wewe na wewe kumuelewa yeye na hiyo itaepusha hali ya kuchanganyikiwa kwako.

Mumeo anadhani kitendo cha kukuoa wewe basi anakumiliki na anataka ufanye yale atakayo yeye bila kujali hisia zako. Mumeo hajui kuwa wanawake huwa tunavaa kutoakana na tunavyojisikiwa au "mood", mavazi hutufanya tujisikie wazuri, warembo na tunavutia, mavazi hutufanya tufurahie siku, mavazi hutufanya tuwe na huzuni, mavazi hutufanya tutake kufanya mapenzi n.k.

Sasa, ili mumeo aelewe hilo ni kazi wajibu wako wewe kama mwanamke kumuelewesha kwa kutumia moja ya nguzo muhimu ya kuboresha uhusiano nayo ni Mawasiliano. Wakati unawakilisha hoja yako hakikisha unaiwakalisha kwa upendo, upole ili akuelewe vema pia kumbukakutumia uanamke wako ili kupata utakacho.

Wanaume wanajua nini hasa huwavutia kutoka kwa wanawake, wapo wanaovutiwa na vifua, wengine wanavutiwa na sura na baadhi ni makalio na wengi huvutiwa na sehemu ya mapaja. sasa kama mumeo anavutiwa zaidi na mapaja yako niwazi kuwa hatopenda ku-share sehemu hiyo na wanaume wengine hata kama ni kwa kuyaangalia tu.

Anashindwa kukuambia moja kwa moja kuhusiana na kutojiamini kwake na badala yake anatumia lugha ya ukali ili kufikisha ujumbe kuwa "sipendi wanaume wengine waone mali zangu"....sijui unanielewa dada mdogo?

Kumbuka kuwa huyo ni mumeo hivyo anatsahili kuheshimiwa na kama akikataa kata kata wewe kuvaa nguo fupi nje ya nyumba yenu basi jaribu kumuelewa na wewe tafuta mavazi mengine ambayo yataendelea kukufanya uvutie, ujisikie mrembo na mwenye furaha...sio lazima yawe mafupi sana (juu ya magoti) yanaweza kuwa chini kidogo ya magoti nakuachia sehemu kuwa ya miguu yako kuonekana na hiyo itakufanya ujisikie swaaaaaafi kabisa.

*****************************************************************************

Nimefikisha mara mbili nakuta msg zisizoeleweka kwenye simu yake ukimuuliza anakwambia hivi mara vile ilimladi tu usiendelee kumuuliza. Lakini hivi yeye akipiga simu ikatokea nimechelewa kupokea akirudi kutoka kazini nyumba inakosa amani kabisa.

Dinah anasema; Unatakiwa kupangilia maswali yako ili kupata majibu ya kuridhisha kama ujumbe wa simu ulioukuta unahashiria yeye kutokuwa muaminifu, kamwe hata siku moja usikubali maelezo yake ambayo unahisi kutoyaamini.

Hakikisha unafikiri huku unaongea/uliza pia sikiliza majibu yake huku unayatafakari ili akimaliza kujibu unamtundika swali lingine hii inakusaidia kupata ukweli na kama ukihisi unadanganywa basi ni wakati wa kuweka rules kwenye uhusiano wenu.

Huyo ni mume wako, mmeoana na sio amekuoa hivyo basi unahaki ya kusikilizwa, kuthaminiwa, kujua marafiki zake, wafanya kazi wenzake, ndugu na jamaa zake, kujua anawasiliana na akina nani na uhusiano wao gani, wapi hufanya matembezi na nyingine zote uzijuazo wewe ndani ya ndoa yanu. Kama unahisi unakosa haki zako kwenye ndoa yako ni wakati wa kuzidai na kuhakikisha zinaheshimiwa.

**************************************************************************

Juzi simu yangu ilijizima nikiwa salon iliyo nje ya uzio wa nyumba tanayo ishi akampigia rafiki yake akaja mpaka saloon nikaongea naye kupitia simu ya rafiki yake jamani hakukaa mpaka muda wa kazi uishe karudi hakuna salam ananiambia utanieleza uliko kuwa huku anatafuta mkanda aanze shunghuli mimi nikamwambia labda anasababu zake tu nyingine lakini mimi sijatoka hata gengeni sikwenda.


Siku hiyo ndipo alipo muita mtoto wake mwenye miaka minne nilimkuta naye akamuuliza, ndipo mtoto akamwambia "mama leo hajaenda mahali zaidi ya saloon anako sema" mume wangu akaona aibu akaondoka dada hata sasa nikimuuliza kwa nini ananifanyia hivyo ananiambia nisimkumbushe anakasirika mpaka nashindwa hata kuendelea kumuuliza dada ni mengi lakini naomba niasidae kwanza kama haya mama na nikisema nimalize yote leo nita kesha naandika. Ni mimi Mama T"


Dinah anasema: Samahani nilipitiwa na kudhani nimekwisha kujibu, pole sana kwa usumbufu niliokusababishia. naja kumalizia....Mama T, mume wako hajiamini hali inayomfanya ashindwe kukuamini wewe. Ukijiamini kuwa ni mpenzi mwema, unajua wajibu wako kwa mkeo huwezi kuhofia vitu vidogo kama kutopokea simu......wanaume wengi ambao sio waaminifu ndio huwa na tabia hiyo aliyonayo mumeo.


Huenda hajawahi kutoka nje ya ndoa yenu ila yuko njiani kufanya hivyo ndio maana anaonyesha wivu kupita kiasi, kutokana na ego zao (wanaume) huwa hawapendi au niseme hawawezi ku-hadle the idea ya "kutiliwa/tombewa" mkewe achilia mbali mpenzi wake, sasa kama yeye anafanya hivyo au anataka kufanya hivyo anataka kuhakikisha hakuna wa kulipiza kisasi kwa mkewe kwa kudhani kuwa atakaefanikiwa kukufanya wewe atafaidi kama yeye anavyo/atakavyofaidi mwanamke mwingine.


Suala muhimu ni kuzungumzia matatizo yenu kwa wazi na bila kuhusisha hasira. Unapozungumza na mumeo kamwe usianze kwa kuuliza maswali kama "kwanini unanifanyia hivi au vile" na badala yake unamuweka katka mazingira mazuri na tulivu kiakili na kimwili (usihusishe ngono, kwani atakupa majibu ili kupata mambo na sio kumaanisha) kisha unazungumza nae sio kutaka majibu kwa kuuliza bali akusikilize na kukuelewa.


Unaweza kuanza..MF-"Ayoub nakupenda sana mume wangu, najua kuna vitu vingi sana nafanya ambavyo huwa havikufurahishi lakini kati ya hivyo hakuna hata kimoja kinahusisha mimi mkeo kusaliti ndoa yetu. Naomba mpenzi wangu ujenge uaminifu kwangu kamavile ninavyokuamini".....wakati unasema hayo na mengine unayodhani ni muhimu ili kusaidia kubadilisha tabia yake mbaya basi unapaswa kutumia uanamke wako kumfanya aendelee kuwa interested kukusikiliza.

Wanaume wakati mwingine wanahitaji muongozo kutoka kwa wake zao as if ni mama zao, sio ktk kuwa-control,lisha, ogesha,beba n.k bali kuwaelekeza namna ya kuishi kama pea/wapenzi/wenza......sisi wanawake tunabahati kuwa tunafundishwa kabla hatujaishi na wanaume au hata kuolewa. Wanaume wengi wanajifunza wenyewe tu hapa Duniani hivyo basi kuna mengi hawayajui hasa namna ya kuishi na mwanamke lakini wewe kama mwanamke unatakiwa kuongoza (sio kwa kumuambia hujui kitu la hasha! tumia busara na mapenzi).


Sasa, ikiwa hamtoelewana ninyi kama wapenzi basi ni vema kupeleka matatizo yenu juu zaidi. Kwa kawaida wanandoa huwa tunakimbilia kwa wazazi, lakini kumbuka wazazi wanatupenda sisi watoto wao hivyo kwa vyovyote vile kutakuwa na "kaupendeleo" upande mmoja tofauti kabisa kama mkikutana na mtu baki lakini anauzoefu au niseme mtaalam wa mambo ya ndoa na mahusiano itakuwa vema zaidi.


Labda nikuulize au unaweza kujiuliza mwenyewe....je unampenda mumeo? Uko tayari kujaribu kuifanya ndoa yenu iwe bora au unahisi kuchoka na mapenzi yanapungua kutokana na visa vingi, ila unakaa ndoani ili "usidhalilishe" wazazi wako na jamii kw aujumla?

Kumbuka kwamba, tunafunga ndoa kwa vile tunapendana na tunataka kuishi pamoja kila siku za maisha yetu kwa furaha, amani na upendo mpaka kifo kitutenganishe. Lakini kama ndoa inakosa au haina vile vigezo muhimu kwanini hasa ilifunga ndoa kwanini uendelee kuwepo ndani ya ndoa hiyo?

Majibu utakayopata kuhusua hisia zako juu ya ndoa yako, uhusiano wako na mumeo na hisia zako za kimapenzi kwa mumeo zitakusaidia kufanya moja ya maamuzi makuu mawili yafuatayo:-

1-Kwa kushirikiana nyote wawili mjitahidi na kufanya ndoa yenu iwe bora.
Au
2-Kuvunja ndoa hiyo na kila mmoja wenu kuendelea na maisha kivyake.

Kila lakheri.

No comments:

Pages