Tuesday

Yaani hata sielewi nimjibu nini huyu EX-Ushauri

"Shikamoo dada Dinah, natumai wewe ni mzima wa afya na unaendelea kutusaidia sisi wenye matatizo mbalimbali ya kimapenzi. Hii ni mara yangu ya kwanza kuomba msaada kwako japo nimekuwa nikisoma article zako mbalimbali kupitia blog yako na kuona jinsi unavyosaidia watu mbalimbali.

Mimi ni msichana mwenye miaka 22, nipo masomoni nje ya nchi. Kabla sijaondoka hapo nyumbani nilikuwa boyfriend ambaye tulikutana kwenye pilikapilika za kimasomo (tuition). Sikuwa na uhakika kama kweli ananipenda lakini nikajikuta nimeanza nae urafiki na hatimaye kukutana kimwili.


Kwa nilivyouona uhusiano wetu nilihisi kama alitaka kuwa na mimi sababu ya uwezo wa kifamilia tulionao na si mapenzi sababu alikuwa na maisha ya kawaida sana (samahani kwa kutumia neno kapuku) na mara baada ya kufanya mapenzi nae alianza kunitreat tofauti na mwanzo. Hata nilipomwambia naenda kusoma nje hakurespond kama nilivyotarajia kwani hakuonyesha dalili ya kujali. Kwakifupi ilikuwa kama tumeachana japo hakuna alietamka.


Mara baada ya kufika huku nikamtumia namba yangu ya simu na tukawa tunawasiliana hadi niliporudi likizo yangu tukaendelea kama kawaida japo hali ya yeye kupenda kufanya mapenzi kila tukutanapo haikuisha. Alitaka tukutane kila wiki (ilifika kipindi hata nikiwa kwenye siku zangu alitaka tufanye na nikimgomea inakuwa ishu).


Niliporudi huku tuliendelea kuwasiliana tena kwa muda baadae akakata mawasiliano, nami nikaamua kukaa kimya nimuone atafanya nini lakini ndio akawa kimya moja kwa moja. Nikajua ndio tumemalizana.

Baada ya kuona kimya hicho nikaamua kuanzisha uhusianio mwingine na mtu mpya ambaye hakuwa mTanzania. Nilikuwa nae kwa mwaka na tulikuwa tunaendelea vizuri hadi alipo graduate na kwenda kwao na sitegemei kukutana nae tena.

Nilikaa kwa mwezi mmoja nikaanza kuwa na uhusiano na mvulana mwengine ambaye ni Mbongo mwenzangu. Najua dada unaweza kuniona somehow kicheche lakini naomba unisaidie maana nimechoka kubadili wavulana na tatizo langu kubwa siwezi kujizuia hasa mvulana akiwa mzuri.

Huyu mbongo nilienae sasa nilisoma nae O-level huko nyumbani. Kiukweli ni mzuri na historia yake ya nyuma alikuwa kigongo hasa kwa wasichana japo nilikuwa sijui wakati tunasomanae. Yeye mwenyewe ameniambia kweli alikuwa kicheche na akanipa album yake nimeona picha za hao wasichana wake wa zamani lakini kaniambia ameamua kutulia.

Nikaamua kujaribu bahati yangu kwa mara nyingine, nampenda sana huyu nilienae sasa na najaribu kumridhisha kwa kum-treat anavyotaka. (yeye ni out-going sana japo mimi si mtu wa viwanja kabisa). Yaani naona kama nimepata nilichokuwa natafuta kwa muda mrefu maana ana kila kitu nilichotaka mwandani wangu mtarajiwa awenacho ikiwemo elimu, uzuri, kujali na mambo mengine ndio maana najitahidi nim-keep ili tufike mbali na Mungu akipenda tufunge ndoa japo sina uhakika.


Dada kiufupi nimeshakuwa na wavulana 6 kabla ya huyu wa kwanza(1) alitaka tu awe wa kwanza kutembea na mimi na baadae alinidump. Wapili(2) alinipenda lakini alikuwa na elimu ndogo and tulikuwa tunaishi mtaa mmoja so nikam-dump. Watatu(3) nilikutana nae thru marafiki wa kalamu na tulisex siku moja baadae tukaachana sababu alitaka ndoa nami umri haukuruhusu naye alinizidi miaka7. Wanne(4) nilikutana nae kupitia rafiki yangu na tulishindana tabia tukaachana. Watano(5) ndo huyo tuliekutana nae tuition na tumeachana kimya kimya. Wasita (6)niliekutana nae huku kutoka Taifa lingine ambaye ame-graduate na kuondoka na wasaba(7) ndio huyu nilienae sasa katika wote hao niliekaa nae sana ni namba 5 & 6 wengine nilikaa nao si zaidi ya miezi3.


Tangu nilipojua nia ya huyo wa kwanza nikawa na hasira na wanaume so nikawa nawabadili kama nguo kulipiza kisasi lakini baadae nikaona ni ujinga na kuamua kutulia na huyo namba 5 nikajua nimepata.

Mwisho kabisa dada Dinah. Hivi karibuni huyo namba 5 ameanza kunitumia msg kuonyesha kuwa bado anajali baada ya kuwa kimya mwaka mzima ambao sikurudi huko, anasema ananipenda na alikuwa busy sababu ya maisha. Mimi sitaki kumrudia na hajui kama nilisha move on na kuwa na watu wengine.

Ninachotaka sasa ni kuwa na huyu nilienae lakini sijui jinsi gani nimwambie huyo wa huko Tanzania. Pia nimesikia mkilingana umri ni shida kuelewana, naomba imaana huyu wa sasa tuko nae sawa lakini naamini tutafika mbali japo sasa tuna miezi minne.

Natumai utanisaidia dada yangu.
Ni mimi Ney de great."

Dinah anasema:Marhaba Ney, mie ni mzima wa afya namshukuru Mungu. Asante sana kwa mail yako na kwa kueleza kwa uwazi historia ya maisha yako ya kimapenzi. Hakika umeanza kujihusisha na masuala ya Ngono na mahusiano ya kimapenzi mapema na kwa kasi kubwa sana.

Kutokana na maelezo yako inawezekana ktk ukuaji wako ulikosa sehemu fulani ya mapenzi kutoka kwa wazazi wako, kama ulivyodai kuwa kwenu mnauwezo wa kifedha. Mara zote familia zenye kujiweza huwa "busy" na shughuli za kuhakikisha pesa zinaingia na miradi inakwenda vema ili watoto na familia kwa ujumla kuendelea kuishi comfortably.....


Hii hufanya wazazi kujisahau na kutowapa mapenzi ya kutosha watoto wao na hivyo watoto ku-miss hayo mapenzi na matokeo yake baadhi huwa na tabia kama yako. Kwamba wanakuwa na msululu wa wapenzi wa muda mfupi ktk umri mdogo na kwa muda mfupi.


Nakuelewa uliposema kuwa uliamua kutoka au kubadili wanaume mara kwa mara (hope u were and still using Condoms) kwa vile ulikuwa unadhani unawakomoa, kitendo cha wewe kufanya hivyo au kuamini hivyo ni wazi ulikuwa umeathirika Kisaikolojia kutokana na uzoefu wako mbaya uliosababishwa na Mpenzi wako......baadhi ya wanawake huathirika vibaya kiasi kwamba wanapoteza hisia juu ya wanaume na kuibua hisia juu ya wanawake wenzao!


Lakini wewe ni mwanamke, na kwa kawaida mwanamke anachagua nani wa kumpa mwili wake na lini hivyo basi suala la wewe kushindwa kujizuia ikiwa mwanaume ni "mzuri" sio sababu ya kutosha kukufanya wewe kujipelekesha kwa wanaume hao ambao kwa namna moja au nyingine hawana mapenzi juu yako.....anyway, hatuwezi kubadili yaliyokwisha tokea tusonge mbele sasa.


Pongezi za dhati kwa uamuzi wako wa busara wa kuacha "katabia kale kachafu ka kulipiza kisasi", kutokana na maumbile ya mwanamke kitendo cha kufanya ngono na wanaume wengi hasa ktk umri mdogo unaweza kusababisha mabadiliko makubwa sana ya mwili wako hasa sehemu nyeti licha ya hivyo pia unaweza kupata maambukizo ya Zinaa.


Kutokana na umri wako mdogo na bahati uliyonayo ya kuendelea na masomo ni vema basi ukazingatia zaidi masomo na kufikiria maisha yako ya baadae kama ambavyo baadhi ya wachangia walivyokushauri.


Pamoja na kusema hivyo sina maana kuwa uachane na huyo mpenzi wako, la hasha! Endelea na uhusiano wenu lakini usiweke effort yote kwenye mapenzi na kum-treat kwa kila anachokitaka na badala yake jifunze kuwa na mipaka ili usije umia baadae ikiwa uhusiano hautokuwa vile unavyotaka hapo baadae.

Huyo Namba tano achana nae, Block namba yake au wewe badilisha namba yako, huitaji kumuambia chochote wala kumhabarisha kuhusu maisha yako na mpenzi wako wa sasa kwani hausiki in what so ever!

Kama kweli mnapendana na mmetulia (wewe na Mpenzi No.7) endeleeni hivyo na furahieni maisha yenu ya ujana. Kumbuka kuchukulia uhusiano wenu kawaida na kama Mungu anataka ninyi wawili siku moja kuwa mume na mke basi itakuwa hivyo, usilazimishe.

Kuwa muangalifu, na kumbuka mwanamke ana haki zote juu ya mwili wake, hakikisha men dont abuse it kwa kujiheshimu nakuheshimu utu wako, pia maisha yako ya baadae yapo mikononi mwako usiruhusu mtu baki akupokonye!

Kila la kheri!

No comments:

Pages