Wednesday

Ndoa imenishinda, Mume anitaka tena-Ushauri!

"Dada dinah! Baada ya kusoma blogu yako na kuona unawasaidia wengi nami leo nimeamua kuandika mkasa wangu. Mimi nina umri wa miaka 28 nimeolewa miaka minne iliyopita na kwenye ndoa yetu tumebahatika kupata mtoto mmoja wa kike.


Dada dinah kabla ya kuoana na mume wangu tulikuwa wachumba kwa takriban miaka minne, kwenye kipindi cha uchumba ni mwaka mmoja tu ndo tuliishi kwa mapenzi ya kweli na raha za kila aina mwaka uliofuata akaanza visa, mara namfuma na msg za wanawake nikimuuliza anakuwa mkali, nikienda kwake nakutavipodozi au nguo za ndani nilizoacha zimefichwa.


Dada dinah mapenzi yakawa hayapo tena, naweza nikakaa wiki mbili sijaenda kwake na siku nikienda yeye amechoka na hataki tufanye chochote. Kuna siku nilienda akanikatalia tusifanye kitu, kesho yake asubuhi nikawa nafanya usafi wa nafagia nje nikakuta mfuko ndani kuna condom 3 zilizotumika.


Nilisikia kufa nikaziweka kitandani nikaacha kufanya usafi nikaondoka kwa hasira. Aliporudi alipozikuta akaanza kupiga simu na kuomba msamaha, kwa kuwa bado nilikuwa nampenda yakaisha. Lakini tabia hiyo iliendelea na nilipozidi kumbana akatamka kwamba hatujaoana kwahiyo bado anachagua yupi atakayemfaa kuwa mke kwa kweli niliumia sana na mapenzi yakaanza kupungua.


Ikafikia mahali nikawa nasikia tetesi kwa majirani anavyobadili wanawake kama haitoshi akatembea na rafiki yangu nilipojua hilo kwa kweli nikaamua kuachana nae. Alikiri na kuomba msamaha lakini ilikuwa nimeshachoshwa nae, akawa anaomba msamaha sana na kunibembeleza kwa bahati mbaya nikaja kushika ujauzito wake. Alipojua akaanza kuharakisha kufunga ndoa na kunisihi nisitoe.

Kama binadamu nikamuua kusamehe na tukafunga ndoa 2005, nikajua atabadilika ktk ndoa lakini wapi mambo yakawa yaleyale kufuma msg, akisafiri nakuta condom kwenye begi kasahau, mbaya zaidi akaanza manyanyaso na kashfa ndani ya nyumba na vipigo bila sababu za msingi.


Nikaamua kuvumilia nilee mtoto, Mungu amenisaidia mwanangu ana miaka mitatu sasa na nimebahatika kupata kazi kwenye Shirika moja nje ya Dar nikaamua kuondoka na nimeanza maisha mapya. Kwa kweli mapenzi naye yameisha kabisa hata yale ya kujilazimisha.

Sasa anaomba msamaha nirudi atajirekebisha na kwa mwezi anakuja mara 3. Jamani mie nimechoka kurudi siwezi na ninamuogopa saana kukutana nae kimwili kwa tabia zake tusijepeana maradhi huwa namsihi tutumie condom hataki.

Mie nimeamua kuachana nae kabisa na yeye nimemwambia lakini anazidi kuomba msamaha na kukiri makosa yake na anahidi kujirekebisha, kaahidi mpaka kuninunulia gari nimsamehe. Jamani hebu mnishauri mie nimechoka nae na sitaki kurudiana nae maisha nayoishi sasa ni ya amani sana."

Jawabu: Hongera sana kwa hatua uliyoichukua na msimamo unaoendelea nao. Inasikitisha kuona kwamba kile kipindi ambacho watu ndio hufurahia zaidi wewe ulikutana na vituko vingi kuliko umri uliokuwa nao kipindi hicho.

Nashindwa kujizuia kufikiria kuwa ulikubali kufunga ndoa kwa vile tu ulikuwa na Mimba, kama isingekuwa mimba labda usingeolewa nae.....kwa bahati mbaya hatuwezi kubadili yaliyokwisha tokea.

Kwa kawaida wanandoa huwa wanashauriwa kuto kuachana au kuvunja ndoa, hata mimi sipendi kabisa kuharibu ndoa au uhusiano lakini ikiwa mhusika anahatarisha maisha yako basi inabidi ndoa ivunjike tu ili kuokoa maisha yako.

Kuachana nae kienyeji tu haitomfanya aache kukusumbua. Suala muhimu ni kutafuta Wanasheria wanajihusiaha na masuala ya Ndoa na Talaka kwa msaada zaidi ili umtaliki mumeo kisheria kitu kitakachomuondolea "mamlaka" anayodhani anayo juu yako kwa vile tu mlifunga ndoa.

Kama unapata taabu kuwapata Wanasheria (najua Wakibongo wanamaringo sana, watakuzunguusha weee), unaweza kutembelea Mahakama yeyote iliyokaribu na wewe na kuomba kuonana na Jaji na kumueleza nia yako ya kumtaliki mumeo na sababu ya kutaka kufanya hivyo.


Yeye atakuuliza maswali machache kama vile, mara ya mwisho kufanya mapenzi ilikuwa lini? Sasa anaishi wapi? na wewe unaishi wapi? Mmetengena kwa muda gani? pia unaweza kuulizwa kama unaweza kumudu mahitaji ya mtoto n.k. kisha utapatiwa barua ya kumulika mumeo hapo Mahakamani ili wasikilize upande wake wa "hadithi".....haijalishi hata kama atatoa machozi ya damu na kuomba misamaha yote hakikisha unabaki na msimamo wako, kuwa ndoa imekushinda kutokana na tabia yake chafu.


Pamoja na kuwa wewe na soon Ex mume wako mnatofauti na hutaki kubaki kwenye ndoa, hakikisha mtoto anakuwa na uhusiano mzuri na baba yake. Kamwe usim-feed mtoto wako na uchafu aliokuwa anaufanya baba'ke, kwani kwa kufanya hivyo kunaweza kusababisha Binti yako kujenga chuki na baba yake kitu ambacho nisingeshauri.

Kila la kheri!

No comments:

Pages