Sunday

Aruka hedhi, nikioa tutapata mtoto?-Ushauri

"Dada Dinah ur a great hero in all about sex education and health in general, Kwa kweli mimi nataka kukuuliza hili kuhusiana na huyu girlfriend wangu niliye naye. Ni kweli nampenda na nilianza naye akiwa bikira kiasi nimeamua kama mungu akipenda tuoane naye na nimeanza kumtambulisha kwa baadhi ya ndugu zangu.

Dada dinah nisaidie mwenzio cz huyu girlfriend wangu ana tatizo la kuruka hedhi zake ila ya mwisho imeniacha na mawazo mengi mpaka sasa maana siku ya mwisho amepata period ni mwezi wa saba mwaka huu mpaka sasa tumesubiria lakini hatujaona dalili zozote naogapa mpaka nikampeleka mwenyewe kupima mimba lakini hamna maana nilihofu ana mimba lakini wapi.

Sasa nikamshauri aende kwa Daktari anasema amemuulizia rafiki yake amemwambia huwa inatokea kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa stress na n.k lakini naona imezidi na ananipa wakati mgumu kwani sijui ni kwa nini iwe ivyo maana nataka kumuoa ila kama ndo ivi tutaweza kupata mtoto kama mungu atatusaidia kuoana naye? Naomba msaada wako wa kina dada pls tusaidie wana jamii.
Mdau, Kahama. "

Jawabu: Kukosa hedhi kunaweza kusababishwa na vitu mbalimbali pamoja na hali ya hewa ambayo inaweza kuhoroganya/kanganya Homono, mahangaiko ya akili yanayosababishwa na maisha(stress) pia inaweza kusababisha mwanamke kukosa hedhi.

Ni kweli kabisa kuwa "stress" na hali ya hewa inaweza kuwa sababu. Kama mpenzi wako amehamia huko mliko hivi sasa for the past 12months basi mmpe muda ili mwili wake uzoee.

Ikiwa mpenzi wako anatumia madawa ya kuzuia mimba hakika anaweza kuwa anaruka sana siku zake, kuna baadhi hupata Hedhi mara tatu kwa mwaka, wengine mara nne nakadhalika inategemea aina gani ya kinga ya mimba unatumia.


Kwa vile mpenzi wako anapata damu yake mara fulani fulani sio kwamba anakosa kabisa ana kwa mwaka anakwenda mara tatu basi sidhani kama anaweza kupata matatizo ya kushikamimba ya hatimae kujifungua.


Suala muhimu kwake na kwako wewe ni kufuatilia terehe zake kila mwenzi hasa miezi ile ambayo anaona damu yake(hedhi). Mtakapo funga ndoa na mkaamua kuwa ni wakati muafaka wa kujaribu kwa ajili ya mtoto (kushika mimba) basi mfanye hivyo kwenye zile siku ambazo yai liko tayari kurutubishwa yaani limepevuka na linasubiri kushuka.


Ili kujua siku hizo mpenzi wako anaweza akatumia kalenda(tarehe) na vilevile anaweza kutumia njia za kiasili kama vile kuangalia na kufuatilia mabadiliko ya mwili wake.

Nitakueleza mabadiliko hayo ya mwili mara baada ya masaa machache.....

Bofya hapa kusoma maelezo ambayo ni majibu ya swali kuhusu kuruka hedhi

No comments:

Pages