
"Hi, dada Dinah, Mie ni yule msichana mwenye miaka 28 ambaye niliehisi nikahakiki na kupoteza mapenzi.
Nini cha kufanya-Muonyeshe mapenzi ya hisia na sio ya mwili, jitahidi kuwa karibu nae na kuzungumza nae kwa kumuangalia machoni (ana kwa ana) kuhusiana na unavyojisikia juu yamapenzi yako kwake (sio kulalamika), Muulize kama alipofunga ndoa na wewe hakuwa tayari au hakuwa na mapenzi ya dhati juu yako.
Sema wazi kuwa kama alikuoa kwa sababu nyingine na sio kwa mapenzi unaelewa anavyojisikia na hata kama ingekuwa wewe ungejisikia hivyo ajisikiavyo yeye......lakini wewe unampenda sana, (hapa mmwagie misifa zinazokaribia na ukweli)........sio kumuambia yeye mzuri hapana, sifa kutokana na utendaji wake kitandani, uongeaji wake, muonekano wake, busu zake, mwendo, misuli yake ya kiume n.k tena fanya hivyo ukionyesha ashiki lakini usipitilize, kumbuka unaonyesha mapenzi ya hisia na sio ya mwili hapa.
Hoji kwa upole na upendo kama kuna tatizo lolote ambalo labda wewe hulijui akueleze na mtafute suruhisho kwa pamoja kama familia, husisha watoto kwenye maongezi hayo, kuwa wanahitaji kukua kwenye mazingira ya upendo na amani utokao kwa wazazi wao ambao ni wewe na yeye.
Mawasiliano hayo yatasaidia kumfanya awe huru kutoa yaliyouaza moyo wake (inategemea na utakavyo muanza na jinsi utakavyo m-bembeleza na kumshawishi kwa mapenzi ya hisia, wanawake tuna uwezo huo)......ikiwa alikuoa wewe bila mapenzi yake anaweza kueleza hilo, kama ni "maujuzi yako" yanam-put off atasema (kumbuka unatafuta suluhisho), sasa hata akikuku-offend wewe chukulia kawaida.
Baada ya hapo utakuwa umejua ukweli kwanini amekuwa na tabia ya ajabu, hapo atakuwa amekupa mwanga wa kuweka mikakati madhubuti kurekebisha mambo. Usimtenge, endelea kumuonyesha mapenzi ya dhati. Siku akitaka ngono mmpe kwa mapenzi yako yote na wewe i-tune akili yako kuwa unafanya mapenzi na mumeo ili uweze kufurahia.
Ikitokea wewe unataka usimuambie moja kwa moja kuwa unataka kutiwa na badala yake fanya vitendo vitakavyomfanya awe-relaxed......kabla hujalianzisha, na unapolianzisha sio unakimbilia kufungua zipu na kumnyonya "abdala kipara" na badala yake cheza na zile kona za kumnyegesha mwanaume kwa kutumia ulimi au mikono na vidole.
Nasikitika kusema kuwa mwanaume anapokuambia mambo fulani na kuyarudia mara kwa mara tambua kuwa kati ya hayo moja au mawili ni kweli, hivyo ni wajibu wako kufanya mabadiliko. Sasa angalia kwa undani haya yafuatayo ambayo nitayafafanua ili unielewe vema.
Ujeuri-Kutokana na kukosa ngono ipasavyo ni wazi kuwa huna raha na inakusababishia hasira hivyo chochote mumeo atakacho kuuliza au kukuambia unaweza kumjibu kijeuri, pengine sio yeye tu bali kila mtu aliye karibu na wewe. Badilika.
Uchafu-Pamoja na kujiswafi kwako na kuoga, huenda manukato unayotumia (waoga maji ya hiriki au marumba-rumba, wajifukiza udi, mafuta uzuri yatokanayo na mkaratusi etc) ambayo Bibi alikuambia humvutia mwanaume huyu mumeo yanamchefua.
Unajua harufu za manukato (hata kama ni Oganza) zikijichanganya na harufu asilia ya mwili inaweza kutoa harufu mbaya mmno na harufu ya mwili ni bonge la pu-off. Vilevile inawezekana jinsi unavyoiweka nyuma, iweke nyumba ionenkane kuna mwanamke, jipende, badilisha mpangilio wa vitu kila baada ya miezi 3-6, ipambe lakini isiwe too much.
Pia isije kuwa jinsi unavyovyaa.....mwanamke kujipenda na kuvutia, hivyo sio unatilia mavazi mazuri ukienda harusini tu bali mvalie mumeo vizuri ili avutiwe na wewe. Badilisha mtindo wako wa kimavazi na jinsi unavyoiweka nyumba yako.
Uchoyo-Kutokana na hasira, kutokuwa na furaha, inawezekana unapika chakula cha aina moja au hupiki kabisa kumkomoa au kutuma ujumbe kuwa wewe ni muhimu, lakini yeye halioni hilo bali anakudhania kuwa wewe ni mchoyo. Vilevile inawezekana anapokuja na wageni na wewe huonyeshi kufurahi (kutokana na matatizo yako ya ndoa), lakini wageni hao na mumeo wanahisi kuwa hupendi waje kwako kula, ukidhani wanakuja kula n.k.
Ubishi-Unayokumbana nayo kwenye uhusiano wako yanaweza kuwa ni matokeo ya wewe kujaribu kupigania haki yako, mumeo anapokuambia kitu au kuomba kitu unabisha kukifanya kwa vile yeye huwa hafanyi lolote unapohitaji. Kumbuka nimekuambia onyesha mapenzi ya hisia, basi acha ubishi.
Baada ya yote haya mumeo haonyeshi kubadilika hata robo? Girl go for the Talaka, tunafunga ndoa ili kuwa na furaha, kupata ushirikiano ktk nyanja zote lakini wewe huzipati, kisa cha kuwa single mum with a husband??
Kila la kheri!
Kitendo cha yeye kuonyesha anataka kurudiana na wewe mimi nadhani ni kwavile unampa ngono, isijekuwa anakuja hapo kwa ajili ya mwili wako lakini hana mpango na wewe kama mpenzi wake wa kudumu.
Kuona ujumbe wa kukupa Hongera ya kujifungua kutoka kwa Ex sio kosa kubwa la kumfanya ahitaji muda wa kufikiri, anafikiri nini kisichofikirika kwa muda wa miezi zaidi ya miwili? Ingekuwa amekukuta na mwanaume mwingine ningeelewa kuwa nahitaji muda hata wa miezi sita kufikiri na kujitahidi kukusamehe na kusahau lakini barua pepe tu!.....anawalakini huyo.
Nini cha kufanya-Sitisha uhusiano wa kingono na yeye tangu anahitaji muda kufikiri basi aendelee kufikiri na akimaliza nakuamua kurudiana na wewe moja kwa moja ndio Ngono itapatikana. Muambie kuwa huwezi kufanya ngono nje ya uhusiano kwa vile unahofia afya yako na ya mtoto kwani hakuna sababu ya kupewa mapenzi ya mwili wakati yeye hakupi mapenzi wala amani moyoni, vilevile hujui anafanya nini huko anakotumia muda wake kufikiri. Hilo mosi.
Pili, Rudisha uhusiano kwa marafiki na ndugu zako na tumia muda wako mwingi na watu hao hali itakayokusiaidia kuondokana na mawazo juu ya mwanaume asiye muelevu na wala hajui kuthamini hisia za mtu anaempenda kwa dhati ambae ni wewe mama wa mtoto wake.
Kitendo cha kuwa karibu na watu hao (ndugu na marafiki zako) kama ilivyokuwa zamani itasaidia kuboresha utendaji wako wa kazi nakuongeza furaha kwenye maisha yako, kumbuka kuwa unajukumu lingine ambalo ni mtoto. Hakikisha huruhusu matatizo yako ya kimapenzi kuathiri utendaji wako wa kazi ili usije fukuzwa kazi.
Jitahidi kutumia muda wako mwingi na watu hao pale unapopata nafasi, ikiwezekana badilisha kabisa mtindo wa maisha yako na mtindo wa kimavazi na jinsi unavyokuwa ukijiweka wakati uko na huyo "mzee wa kufikiri". Kumbuka wewe bado Kijana, Mzuri, unapendeza na kuvutiaa sasa muonyeshe kuwa unamtaka kwa vile unampenda lakini humuhitaji (Unaweza kuishi bila yeye) ikiwa hana mpango na wewe......hapo humuambii unamuonyesha kwa vitendo, kutokana na utakavyokuwa ukijiweka, sawa?
Tatu, Ji-keep busy na mambo yako na mtoto, lakini siku akitaka kuja kumuona mtoto usimkatalie lakini hakikisha kuna kuwa na "limit" ya yeye kuwepo hapo kwako na vilevile anapokuwa na mtoto wewe endelea na shughuli zako nyingine, yaani usimpe muda wa kuongea na wewe au kulianzisha zali la kutaka ngono.
Ukiendelea kumsubiri utakuwa unajipotezea muda, unajinyima amani na uhuru wa kuwa karibu na ndugu, jamaa na marafiki na vilevile kukataa wanaume wengine wanaokutokea na wanakupenda kwa kudhani kuwa baba mtoto wako anafikiria na siku moja atarudi. Siku hazitokusubiri wewe, zinasonga mbele kama ifuatavyo.......
Nne,(ukifikia hatua hii kama anakupenda kweli na anampango nawe, ataomba mzungumze), akiomba mazungumzo na wewe usikubali haraka haraka, mpe muda......mwambie leo unashughuli nyingi hivyo muonane keshokutwa na siku ya siku ikifika usisahau kujiweka ktk hali ya kupendeza na kuvutia kwa maana ya "sexy".
......na kabla hajaanza muwahi na muambie jinsi gani umejitahidi kufanya yale yote ambayo alitaka uyafanye, ulijiweka mbali na marafiki, ndugu na jamaa kwa ajili yake, umebadili nambari ya simu na anuani ya barua pepe ili Ex wako asiwasiliane na wewe kwa vile hukutaka kumuumiza hisia zake.
Kisha muambie msimamo wako na unachokitaka kutoka kwake, iwe ni commitment au unataka kujua uhusiano wenu na mtoto unakwenda wapi na mengine unayodhani ni muhimu na unayataka kutoka kwenye uhusiano wenu huo......alafu mpe nafasi aseme alichotaka kusema!
***Lakini baada ya kufanya yote hayo bado hajaonyesha dalili ya kutaka mazungumzo ili kurudisha "majeshi", basi ujue alikuwa anakutumia kwa ngono kila anapokuja kumuona mtoto wake. Achana nae na keep sexy, keep happy, work hard na siku moja utakutana na mwanaume anaejiamini, atakae kupenda kwa dhati na kukuthamini.
Wewe bado mdada mdogo na kumbuka penzi halilazimishwi.
Kila la kheri.
Natambua wanawake wakati mwingine tunapenda "attention", ukijua kuwa kuna wanaume wengine wanakutamani na kuku-chat up unajisikia raha na mwenye nguvu fulani kama mwanamke, kutongozwa ni kawaida kwa baadhi yetu, kwani kuolewa haina maana kuwa hatutamaniwi na wanaume wengine.
Lakini hiyo haina maana kuwa umkubali kila anaekutongoza na kuanzisha uhusiano ukijua uko ndani ya uhusiano mwingine na mtu unaempenda na ulieahidi kuishi nae maisha yako yote!
Uhusiano wa rafiki yako na mke wa rafiki yake ukoje? bado wanaendelea baada ya mwenye mke kuacha? Je wanadhani kuwa wanapendana?......kama uhusiano wao mzuri basi waendelee lakini kama jamaa alikuwa anataka kuharibu ndoa ya mwenzie kutokana na tamaa au wivu basi akamuombe rafiki yake msamaha alafu ajitenge nae (yaani urafiki ufe), asijaribu kuendeleza urafiki na jamaa baada yakumtombea mkewe.
Ushauri wangu ni wewe kumaliza urafiki na huyo mharibifu wa ndoa ya watu kwani ni wazi kabisa na wewe ukioa ataweza kufanya exactly alichokifanya kwa rafiki yake nakusababisha ndoa yako kufa.
Majibu ya wengi yaliegemea kutokana na maelezo yako ambayo sasa umegundua kuwa hayakuwa yamejitosheleza au hayakuwa wazi kwenye points muhimu ambazo ni hizi:-