Wednesday

Hana shukrani na a'niponda tu kwa Marafiki-Ushauri

"Pole na kazi dada Dinah. Mimi ni Kijana mwenye umri wa miaka 24, ni mwaka mmoja sasa tangu nimeoa. Nina tatizo ambalo linaniumiza kichwa na sijui nifanye nini, thats why nimeamua kukuandkia hii e mail ili nipate ushauri wako na comments from other people.


Tabia ya mke wangu ni kuchukua mambo ya ndani na kuyapeleka nje, na amekua mtu wa kulalamika everyday, Najitahidi kadri ya uwezo wangu kuhakikisha anapata kila anachohitaji lakini imekua kazi bure.


Kutokana na kipato changu hua nikipata pesa nanunua kila kitu ambacho ni muhimu kwa matumizi ya nyumbani kuanzia chakula na mahitaji yake mengine muhimu yaani kwa kifupi everything needed I give to her, lakini kwake yeye ni complaint tu.


Na kitu kina choniumiza zaidi ni pale anapokuwa either with my friends or her friends, yaani hakuna stori nyingine isipokuwa ni kuniponda na kusema namtesa, na mnyanyasa sasa sielewi kama kweli ana mapenzi ya dhati na mimi au la.


Na nikimwambia kama vipi akapumzike home hataki anasema nikimpeleka nyumbani nimpe na Talaka. So dada nahitaji ushauri wako nini nifanye? na je ananipenda au hanipendi kwa hali hii?"


Jawabu:Asante kwa kuniandikia. Mkeo ama hana mapenzi na wewe au hapati kile ambacho anakitaka au alitegemea kukipata kutoka kwako mara baada ya kufunga nae ndoa pamoja na kusema hivyo inawezekana huyu binti alilelewa kwenye mazingira ya kutokujua na kuheshimu miiko ya nyumbani kwako, kwamba kinachotokea kwenu kinabaki palepale kwenu, kwa kifupi hana heshima....utoto pia unaweza kuchangia yeye kuendelea kuwa na katabia hako kabaya kabisa.


Kutokana na maelezo yako umesema kuwa unahakikisha kuwa anapata kila kitu anachotaka na unampa mahitaji yake muhimu ndani ya nyumba, hakuna mahali umeelezea kuhusu kumpa mapenzi ya kutosha.....maisha yenu ya kingono yakoje? Unadhani kuwa unamridhisha linapokuja suala la mahitaji yake ya mwili na hisia?


Tatizo la baadhi yenu wanaume mnadhani kuwa mwanamke ukimpa kila kitu in terms of material things na chakula cha kumwaga basi karidhishwa huyo......kuna mahitaji mengine ambayo kwa baadhi yetu wanawake ni muhimu lakini kwenu wanaume hayana umuhimu kwavile ni madogo.


Ninyi mmefunga ndoa mkiwa wadogo sana (ukilinganisha na maisha tunayishi hivi sasa) hivyo mnatakiwa kufanya mambo kama "young couple" more like bf and gf kuliko baba na mama......have fun!


Kitu kama kujenga urafiki kati yako wewe na mkeo hii itasaidia kuwa karibu zaidi na wewe na kukuambia yaliyomsibu au nini hakimfurahishi ndani ya ndoa yenu. Kumuonyesha mapenzi kwa vitendo sio kufanya hivyo only unapotaka kufanya ngono bali fanya hivyo kila unapopata muda....vitu vidogo kama kumshika, kumbatia wakati mnaangalia Tv, kutoka kwa ajili ya matembezi, kumbusu kila unapokuwa karibu yake.


Akikatiza mbele yako kuelekea jikoni mvute na mpe busu mate, mshike tako na vitu kama hivyo, kumuonyesha kuwa unavutiwa nae na unampenda, msaidie kufanya vijishughuli ndani ya nyumba ukipata nafasi sio kila kitu afanye yeye kwa vile tu umeoa n.k.


Hakikisha mnapofanya mapenzi anaridhika kwanza alafu ndio wewe unamalizia, hakikisha unajua uwezo wake wa kungonoka badala ya kuwa unafanya nae kila siku wakati yeye ni twice a week type(hapo lazima atahisi kuteswa ofcoz) au kama yeye ni wale wanaotaka kila siku na wewe ni mtu wa once a week ofcoz utakuwa unamtesa.


Nini cha kufanya-Kaeni chini na mzungumzie tofauti zenu, weka wazi kuwa hupenzi tabia yake ya kwenda kueleza watu maisha yenu binafsi, mwambie kama kuna tatizo lolote au kuna kitu hakifurahii ungependa akuambie wewe moja kwa moja ili ujirekebishe.


Anza kwa kumuambia akueleze kwa uwazi vitu gani unafanya havipendi tangu mmekuwa pamoja, akivisema basi hakikisha unajirekebisha na kuwa mume bora kwake. Mawasiliano ndio ufunguo wa kurekebisha mambo na kuondoa tofauti ndani ya uhusiano wowote wa kimapenzi kwani ni njia pekee itakufanya wewe na yeye kujua tatizo liko wapi na lilekebishwe vipi.


Mwambie yeye ndio mama mwenye nyumba na yeye ndio anaweza kuibomoa au kuijenga nyumba yenu na kuwa bora zaidi na mfano kwa wanandoa wadogo wengine.


Shirikianeni ili muweze kuishi kwa amani na upendo, kwani mnasafari ndefu sana ya kuendelea kuishi pamoja since wote ni wadogo ndani ya ndoa. Kumbuka ili ndoa iwe bora inahitaji kufanyiwa kazi, Uhusiano wa kimapenzi sio lelemama ni hard work.

Kila la kheri!


***Dinah anawatakia usherekeaji mzuri wa sikukuu ya Noeli, nawapa pole wale wote wanaouguliwa na wale waliofiwa, Mungu awapeuponaji wa haraka wagonjwa na kuwapa moyo wa uvumilivu wafiwa kipindi hiki......Mungu awe nanyi!

No comments:

Pages