Monday

Alinitega, sasa anataka urafiki wa karibu-Ushauri

"Hello dada dinah. Nakupa pongezi kwa kazi unayoifanya ya kushauri watu mbalimbali kuhusu mambo ya mapenzi. Mimi nimekumbana na mkasa na nashindwa kuelewa kama nilikuwa nachezewa akili au la.


Maana haijawahi kutokea maishani mwangu. Hivi majuzi nikiwa Nairobi nilikutana na mrembo mmoja ambaye nilikuwa nafahamiana nae kwa muda mrefu (lakini sio mahusiano ya karibu sana). Sasa huyu dada alinichangamkia na akawa ananipa company pale ninapokuwa free kwenye shughuli zangu nilizoenda kufanya hapo Nairobi.



Labda niwaeleze pia kuwa nilikaa Nairobi kwa muda wa wiki mbili tu. Sasa siku moja nilitoka nae(huyo dada) out na tulipokuwa katikati ya maongezi yetu aliniambia kuwa hana hamu ya kulala kwake. So nikamchomekea kuwa aje kulala kwangu.



Kwa maajabu akakubali. Basi ilipofika mida ya usiku kama unavyojua tena kidume majaribu yakanizidia. Hivyo nikaamua kumtokea. Kwa kweli huyo dada alikataa kata kata kunipa mchezo. Alikubali nimguse baadhi ya maeneo ya mwili lakini sio sehemu zote.



Na pia wakati tumelala alivaa suruali na blouse. So you can imagine jinsi alivyoziba direct access kwenye mwili wake. Nilipojaribu kumbembeleza alikataa na kusema kuwa hayuko tayari kufanya kitendo na pia yeye haitaji kuwa na mtu kwa sasa.


Hivyo nikaamua kuheshimu matakwa yake ingawa kwa shingo upande. Sasa je dada dinah na wanablog wengine. Hembu niambieni huyu dada alikuja kunichezea akili tu au alikuwa anataka nini?


Je ningetumia nguvu kidogo na kumvua nguo na kutombana nae ningekuwa nimefanya makosa?? Mpaka leo ananisalimia na anainsist close friendship. Nipeni ushauri wakuu. Maana hili ni kasheshe sijawahi kukutana nalo.

Wenu mdau.....David"

Jawabu:David nashukuru kwa kuniandikia. Natumaini wasomaji wangu wamekupa majibu yaliyosaidia kuelewa kwanini hasa huyu binti aligoma kungonoka na wewe siku hiyo. Ila nakupa hongera sana, na hapo naweza kukuamini kuwa kweli unampenda huyo binti, angekuwa mwanaume mwingine mjinga-mjinga angebaka.

Wanawake hatutongozi wanaume kama wanaume mnavyotongoza, wanawake huwa tunatumia uanamke wetu kutuma ujumbe kuwa "tumekuzimikia", lakini kama hujaona au unajifanya kudharau (play hard to get) mwanamke anaweza kukata tamaa au anaweza kutumia mbinu nyingine anayoona inaweza kufikisha ujumbe na wakati huohuo kujua kama mwanaume huyo anahisia kama zake.

Sasa kutokana na maelezo yako huyu binti ni wazi anakutaka wewe kama mpenzi lakini hukuliona hilo hapo awali mlipokijuana na kitendo cha yeye kusema kachoka kulala kwake na kukubali offer ya kwenda kulala kwako ni wazi alikuwa anataka kujua msimamo wako wa kihisia....kwa kifupi alikutongoza.

Huyu binti anataka uhusiano "serious" na wewe na kutokana na "mawazo" ya wanawake wengi ni kuwa kufanya ngono siku ya kwanza ni kujidharaulisha na pengine kuna weza kum-put off mwanaume na kukudhania wewe ni "maharage ya mbeya" yaani rahisi, kama tumengonoka mara tu baada ya kukutana utakuwa umengonoka na watu wangapi kabla yangu.....mwanaume atajiuliza.

Lakini ktk hali halisi kufanya ngono ni makubaliano yenu ninyi watu wawili ambayo yanategemea zaidi mmefahamiana kwa muda gani, unajisikia comfy kiasi gani mbele ya mtu huyo, nguvu za hisia zenu na Chemistry itakayojitokeza pale miili yenu itakapokuwa zero distance. Kufanya ngono siku ya kwanza haina uhusiano na tabia ya mtu au sio kigezo kuwa mtu huyo ni mlala ovyo(Malaya).


Huyu binti inawezekana kabisa kuwa anakupenda na ndio maana alikubali kabisa kubadilishana mate na wewe nakushikana hapa na pale ila anataka muwe na uhusiano mzuri na wakudumu sio ule wa kungonoana kila mnapokuwa na hamu (casul).

Nini cha kufanya- Kubali kuwa na urafiki nae wa karibu kama kweli unampenda na sio kwamba unataka ngono tu kutoka kwake. Utakapo kuwa kwenye uhusiano ambao ni urafiki itakuwa rahisi zaidi kuwa na uhusiano madhubuti ambao utakuwa umejengwa ktk misingi ya urafiki.

Nenda taratibu na kama kuna "kemikali" zinazoendana kati yenu basi mambo yatakuwa mambo before you know it.

Kila la kheri.

No comments:

Pages