Friday

Rafiki kaua ndoa ya mshikaji'ke, afanye nini-Ushauri!

"Kuna jambo nataka mnisaidie nini nifanye,
Mim ni mwanaume, kuna lafiki yangu ambaye ni mtu mzima amabe ana mke na watoto. Huyu rafiki yangu ana rafiki yake kipenzi na wamekua kama familia moja, kibaya zaidi huyu jamaa (rafiki yangu) amefanya kitendo kibaya sana cha kumtongoza mke wa rafiki yake na hatimaye kufanya naye vitendo ngono.


Mie nikiwa kama msiri wake mkubwa aliponiambia mambo yale nilimkatalia kabisa na kumwambia ache mambo hayo kwani yatakuja mletea shida baadae lakini hakusikia na kuendelea na mambo yale.


Sasa kilicho kuja kutokea ni mume wa huyo mwanamke Rafiki yake) kuja kujua huo mchezo wao mchafu,alipobanwa mwanamke alikili kuwepo ukweli wa jambo hilo na uadui kuanzia hapo baina ya mumewe na huyu jamaa yangu ambae pia alikuwa rafiki yake.


Kibaya zaidi huyo jamaa kamwacha mke wake kwa sababu hiyo na kumtaalifu mshikaji kuwa amemwacha mke kwa sababu yake. Sasa amenirudia mimi nimsaidie,binafsi sijui nini cha kumshauri na kwa sababu nilimkataza mambo hayo mapema hana cha kunilaumu.

Sijui Dinah na watu wangu mna nini cha kusema juu ya hili. "

Jawabu:Hata mimi sijui cha kumshauri honestly! Rafiki yako hana utu hata kidogo, alijua ni mke wa rafiki yake na bado akatongoza na mpaka kufanya nae ngono, huyo mwanamke ambae ni mke wa rafiki yake pia ni mshenzi na hafai kuwa ktk jamii tena hana hulka kabisa. Kitu gani hasa kilimfanya akubali kutoka na rafiki ya mume wake akiwa ndani ya ndoa?



Natambua wanawake wakati mwingine tunapenda "attention", ukijua kuwa kuna wanaume wengine wanakutamani na kuku-chat up unajisikia raha na mwenye nguvu fulani kama mwanamke, kutongozwa ni kawaida kwa baadhi yetu, kwani kuolewa haina maana kuwa hatutamaniwi na wanaume wengine.

Lakini hiyo haina maana kuwa umkubali kila anaekutongoza na kuanzisha uhusiano ukijua uko ndani ya uhusiano mwingine na mtu unaempenda na ulieahidi kuishi nae maisha yako yote!

Uhusiano wa rafiki yako na mke wa rafiki yake ukoje? bado wanaendelea baada ya mwenye mke kuacha? Je wanadhani kuwa wanapendana?......kama uhusiano wao mzuri basi waendelee lakini kama jamaa alikuwa anataka kuharibu ndoa ya mwenzie kutokana na tamaa au wivu basi akamuombe rafiki yake msamaha alafu ajitenge nae (yaani urafiki ufe), asijaribu kuendeleza urafiki na jamaa baada yakumtombea mkewe.

Ushauri wangu ni wewe kumaliza urafiki na huyo mharibifu wa ndoa ya watu kwani ni wazi kabisa na wewe ukioa ataweza kufanya exactly alichokifanya kwa rafiki yake nakusababisha ndoa yako kufa.


Watu kama hawa, wanapaswa kutengwa na jamii, kwani wanasababisha watu hasa vijana kuhofia suala zima la kufunga ndoa, wanaifanya ndoa kutokuwa na thamani tena.



Kila lililojema!

No comments:

Pages