Tuesday

Nahisi naibiwa-Ushauri.

"Dinah pole na kazi ya kutuelimisha! kwanza nianze na kukushukuru kwa elimu unayotoa pamoja na wadau wengine kwani mengi tumeyajua kupitia blog yako.

Dada Dinah samahani mimi ni mwanaume nina miaka 28, na nakaribia kuoa kama Mungu akipenda mwishoni mwa 2010 au mwanzoni 2011.Tatizo lililo nileta hapa ni kuuliza vitu 61. Kwanini Girlfrend wangu kila akiwa kwenye siku anakuwa mgonjwa kabisa, anatapika haswa, maumivu ya tumbo ndio usiseme huwa anajigaragaza tu chini na dawa ya kutuliza kama diclofenac kameza?

Pia nilimshawishi amuone Doctor kwa hilo anasema ni mara kwa mara kauliza wanasema akizaa mara ya kwanza hilo tatizo linaisha kuna ukweli hapo??


2.Kuna kipindi hakupata siku zake miezi kwa miezi miwili lakini mwezi wa tatu ulipoanza ali-bleed kidogo sana ,mwezi wa nne pia then akaja akaugua vichomi akapelekwa Hospitali yeye anasema Doctor kasema ile damu ya bleed iliganda so akapewa dawa akapona lakini rafiki zake wameni dokeza kuwa katoa mimba nielewe lipi hapa na kama ilikuwa yangu kwanini atoe yaani sielewi kabisa ila yeye akiulizwa anakataa kutoa mimba na anasema hajawahi fanya mapenzi bila kinga. Mimi ni wa kwanza baada ya kupima, yaani sielewi lipi ni lipi!


3. Simu yake mara nyingine hataki niishike, sina kawaida yakuiangalia napenda uhuru ila yangu ruksa sina hiyana. Kuna siku sasa msg iliingia yaani kama machale hivi nikasema huyo lazima atakuwa mwizi wangu ngoja niifungue, kufungua lahaula! ni kama maneno yangu, yaani ni full dear, sijui honey sasa lini tunaonana, nina njaa na vitu kama hivyo.

Siku nyingine msg dear leo nipo Kibaha njoo tulale huku msg hazina majina ni namba tu, nilipo muuliza ni nani akajibu ni jamaa tu anamtongoza ila yeye hamtaki, lakini siku zote nilimwambia nahisi kama naibiwa hivi ila yeye akasema nisiwe na presha wala hana mtu zaidi yangu na kunisifia eti hawezi kumpa penzi mtu mwingine kwani hakuna mwanume kamfikisha kama mimi.


Ila kwa kweli nililazimika kubadili namba yake ya simu aliyokuwa akitumia nikaichukua nikaiweka hewani nilishangaa siku kama 3 simu inaita saa nane au kumi usiku nikipokea anakata nilimpelekea ile namba nikauliza ni ya nani akasema ya baba yake, nilishangaa kwanini baba apige simu muda huo?!


4.Kuna siku alienda kwa shangazi mtu ambako alitakiwa kuangalia watoto wakati shangazi yusafari, aliniambia kuwa uncle mme wa shangazi alimtaka. Mara kuna siku alisahau kufunga mlango wa chumbani uncle kaja na pensi imetuna mboo akimkumbushia kumtaka.


Mimi nikamwambia awe mwangalifu pia amwambie shangazi kuwa kuna hilo limetokea, hakumwambia. Siku nyingine akasema anaumwa akaenda Hospital peke yake uncle akiwa home akatibiwa akarudi.

Si muda mrefu akadai anaumwa tena hiyo siku uncle akampeleka hospital saa 5 asubuhi ,mimi nilipiga simu saa tisa akadai bado wapo hospital?!! saa kumi wapo tangi bovu na huyo huyo uncle wanakula nyama choma yeye akidai mgonjwa!!!?!,vile vile amesema uncle alijituma sana kumletea zawadi hapo home.


Siku nyingine mimi nilikuwa na wasi sana na hilo so nilikuwa napiga simu kila mara. Kuna siku nilipiga simu kuanzia saba usiku mpaka 2 asubuhi hola, haipokelewi, saa nne hivi nakuja kupiga anapokea nikamuuliza hajaona miscalls zangu nyingi nilimpigia akasema hajaona lakini hazikuwa less than 40 na kudai pengine mtoto aliyelala naye kazifuta kwani pengine alishituka usiku na kuchezea simu????!!!!!..


5. Wakati anatoka huko kwa shangazi siku mbili baada ya ile siku nilopiga simu kuanzia saba usiku hadi asubuhi hakupokea, nilimuomba ngono alikubali round ya kwanza tu niliona hahimili kabisa, na mimi nilitaka ku-prove kama niliibiwa au laa na kawaida huwa naunga sometime bao 2 za kwanza kama round moja, siku hiyo ya kwanza ilikuwa kama 7min,nika unga dakika kama ya 10/13 hivi alilalamika anaumia na kuomba apumzike kitu ambacho sijawahi kukiona ni mwaka na miezi kadha sasa tangu tumekuwa pamoja.


Huwa anahimili round zote vizuri 3-6, sasa hapa nina doubt kuibiwa hii kuchoka round ya 2 tena fupi kabisa! aidha kwa mujibu wa marafiki zake huyo uncle alikuwa anamnunulia hadi pad akiwa period sasa hapa jamani ni sahihi kweli hakunakitu kweli hapa? Yeye nikimuuliza anasema hakuna hawezi share na aunt yake!!!?!


6. Na mwisho kabisa dada D ni kuhusu marafiki,anao wengi wakiume, nikimuuliza oooh nilisoma nao, ndugu, sasa hutaki niongee na wanaume!,aaah wivu umekujaa, kwanza watoto wadogo mimi siwataki unanitosha, unanitafutia visa unataka kuniacha lakini kuna wengine mimi nampunguzia credit halafu yeye anawapunguzia ile nilomtumianaomba msaada wa ufafanuzi wa haya mimi naona hapa kama hakuna kitu ingawa yeye anadai kunipenda sana au ni ya kawaida? nitashukuru
by mdau Baraka.M DSM"

Jawabu:Baraka asante kwa kuungana nasi mahali hapa, baadhi ya watu mnapitia mambo mazito kwenye safari hii ya mahusiano ya kimapenzi lakini mnauvumilivu wa ajabu sana au sijui niseme mapenzi ya dhati!

1-Tatizo la kuumwa tumbo wakati wa hedhi kwa baadhi yetu wanawake ni la kawaida, kwa wengine kama ulivyosema hapo hali hiyo huambatana na dalilizote ambazo mwanamke anakuwa nazo anaposhika mimba(sio wanawake wote wakiwa na mimba wanapitia hatu ahii), lakini vilevile wanawake wengine linaweza kuwa sio tatizo la kawaida la hedhi bali tatizo lingine ambalo labda linaweza likahitaji matibabu au hata upasuaji kutokana na ushauri wa Daktari.


2-Mpenzi anapokuwa mchoyo wa simu yake (wengine wanaweka na password kabisa0 au hata neno la siri la barua pepe yake mara zote huwa kuna kitu anaficha na asingependa wewe ujue. Kwa kawaida wapenzi walio kwenye uhusiano "serious" unaoelekea kwenye kufunga ndoa huwa hakuna sababu ya kutokuwa huru mwenzako ashike au kuangalia simu yako. Hata kama huna tabia hiyo bado mpenzi anatakiwa kutohofia kama wewe utaifungua simu yake n.k.


3-Sasa kutokana na tabia ya mpenzio nadhani ulipoteza ile hali ya kumuamini na ukaamua kufanya ulichofanya na kukutana na kile ambacho ulikuwa ukitegemea kukikuta simuni mwake. Kutokana na mapenzi yako ukabadili namba yake ili kuzuia mawasiliano na huyo "mwizi wako" ktk hali halisi angekuwa mwanaume mwingine angemtibua huyo binti kwa ku-cheat!


Kama hiyo haitosho binti huyo alidiliki kuigawa ile namba mpya kwa mpenzi wake wa nje ya uhusiano wenu, wanasema "a cheater will always be a cheater" na hii imethibitishwa na mpenzi wako huyo baada ya kuwa akipigiwa simu na "baba" usiku wa manane.


4-Watoto wa shangazi yake (binamu) wanaishi na baba yako ambae kutokana na maelezo yako nahisi kuwa ndio "baba" na ndio mwizi mkuu wa mpenzi wako. Sababu ya yeye kuwa kule kwa Shangazi kuangalia watoto haimpi ruhusa kulala kuho huko kwani baba yako anakuwepo usiku. Hivyo ktk hali halisi huyu Mpenzi wako alipaswa kutumia akili akisaidiwa na wewe kimawazo kuwa akae na watoto during the day nakurudi kwake/kwenu usiku badala ya kulala huko huko.


Baada ya kuja tuhuma kuwa Mjomba anamtokea, yeye kama binti muaminifu alipaswa kutumia akili na kutokuwepo pale nyumbani usiku (asilale pale), yule ni mjomba ambae hana uhusiano kidamu na mpenzi wako hivyo attraction inaweza kabisa kujitokeza na watu wakapendana......watu wataamua kutoendelea kwa sababu ya kuheshima kuwa ni mume wa shangazi ambae ni dada wa baba......(kwenye jamii nyingine wapwa ni marufuku kuwa karibu na wajomba walio oa dada wa baba yako).


Badala ya kumuambua awe muangalifu ulitakiwa kumshauri asiwe akilala pale kwa mjomba kama nilivyoeleza hapo juu. Nasikitika kusema kuwa kisingizio cha kutokupokea simu na kupokea baadae na kudai kuwa "labda mtoto alichezea" hakina nguvu ya kushawishi ukweli ndani yake.


Kuhusu swala la yeye kuumwa mara kwa mara linatia wasiwasi, hebu mshauri akaangalie afya yake kwa ujumla na zaidi VVU, pia wewe mwenyewe kaangaliwe afya ili ufahamu mapema kama uko huru dhidi ya VVU na kama ni matibabu yaanze haraka na vilevile suala zima la kubadili mtindo wako wa maisha(Lishe, matumizi ya madawa, kuwa muangalifu zaidi kuhusu swala zima la ngono inategemeana na majibu).


5-Kutokana na maelezo yako ni wazi kuwa siku hiyo ya mwisho walikuwa wakifanya "kamuagano" nahuenda alichoka sio kutokana na ngono ya mjomba bali pia hali yake ya kuumwa (natumaini ulitumia kinga siku hiyo).....ila na wewe una moyo wa ajabu!!

Kununuliwa pads sio kitu cha ajabu, hata baba/kaka anaweza kukununulia pads kwani anajua kabisa kuwa unazihitaji kama mwanamke hasa kama huna kipato (hufanyi kazi).


6-Hata kama ingekuwa mimi nisingeweza kuamini rafiki zake wengine wenye jinsia tofauti na yeye. Maelezo yako yameweka wazi tabia halisi ya mpenzi wako kuwa sio muaminifu, sio kwamba unahisi tu bali ushahidi unao kuwa "anachezea hisia zako" kwamba hajatulia hivyo ni ngumu sana kuamini chochote anachosema au kukuambia.


Nini cha kufanya-Nenda kaangalie afya kujua kama una VVU au huna. Majibu utakayoyapata yachukulie kuwa ni ufunguo wa wewe kuanza maisha mapya. Baada ya majibu yako, mshauri na yeye akafanye hivyo (ikiwezekana muende pamoja ili kusiwe na rushwa, mana'ke wengine hulipa ili majibu yabadilishwe).


Ikiwa wote mko safi kiafya au mmeathirika na unahisi kumpenda na unaamini kuwa atabadilika kitabia basi zungumzieni yote na hofu yako juu ya uhusiano wenu, jaribu kuhoji kitu gani anakitaka kutoka kwako ambacho anakwenda kutafuta huko kwa "mjomba". Mawasiliano hayo yatakusaidia wewe kujua mapungufu yako wapi na kuyarekebisha.


Baada ya kukubaliana kuwa mjaribu tena uhusiano wenu basi ni vema kuweka miiko/sheria/rules ndani ua uhusiano wenu na itekelezwe na ninyi wote (mf. kuwa huru kutumia simu zenu, kutokwenda kwa "mjomba" peke yake, kupunguza marafiki wa kiume ambao sio muhimu kwake,n.k.) kisha mpe muda (trial) wa kubadilika bila kuharakisha ndoa.


Vinginevyo (ukihisi hutaki tenakuendelea nae) wewe endelea tu na maisha yako na siku moja utakutana na binti mzuri, mwenye haiba ya kike na mwenye kuthamini penzi.

Heri ya mwaka mpya na kila la kheri!

No comments:

Pages