Tuesday

Alinitenda na rafiki yangu, sasa niko Ughaibuni anitaka tena-Ushauri

"Habari za kazi dada dinah, Mungu akubariki sana kwa kuanzisha uwanja huu wa ushauri kwa watu wenye matatizo, kwa kweli kupitia Blog hii watu mbalimbali tumeweza kuelimika. Nami kama walivyo tangulia wenzangu kuomba ushauri nami naomba ushauri wako na wachangiaji wengine wote kutoka na tatizo hili linalonisumbua.

Mimi ni mwanamke nilikuwa na mwanaume naishi nae kwa bahati nzuri tukabahatika kupata mtoto mmoja, mapenzi yetu yalivunjika baada ya mpenzi wangu huyo kutembea na rafiki yangu mpenzi. Mwanzo wa mapenzi yao nilikuwa naletewa taarifa na watu wa karibu yangu lakini kutokana na kumuamini sana huyo jamaa na rafiki yangu nikawa napuuza nikijua ni maneno ya watu tu.

Lakini siku moja ndipo nilipokuja kupata ukweli baada ya kuzikuta msg za mapenzi kwenye simu yake. Mimi katika kupata ushahidi nikatumia zile msg dada yangu, baadae mpenzi wangu alipokuja kujua kuwa nimegundua hakuonyesha hata dalili ya kuomba msamahaa na siku moja tukagombana sana mbele ya mama yake mzazi kuhusiana na suala hilo na katika kunionyesha ujeuri akazungumza mbele ya mama yake kuwa hawezi kumwacha huyo rafiki yangu.

Mimi sikuona sababu ya kuendelea kuwa nae ikabidi niondoke. Baada ya hapo akaamua kuhamia kwa huyo rafiki yangu na kuishi nae kama mke na mume, Mungu si athuman nilikaa kwa muda wa mwaka mmoja na nusu bila mpenzi wala rafiki wa kike kutokana na jinsi nilivyotendwa.

Baada ya hapo nikapata rafiki wa kiume ambaye alionesha kunipenda na kutaka kunioa lakini kwa vile nilishatendwa nikawa makini, huyo rafiki wa kiume nimefahamiana nae kwa muda wa miezi mitatu tu nikapata safari ya nje ya nchi na kipindi chote cha miezi mitatu sikuwahi kufanya nae mapenzi.

Rafiki huyu wa kiume aliniambia kuwa anataka kunivisha pete ya uchumba kabla sijaondoka, lakini hadi naondoka hajatimiza ahadi yake nami sikutaka kumkumbusha. Sasa baada ya kuwa huku nje yule mwanaume wa kwanza ameanza kunibembeleza eti turudiane na kwamba yeye alifanya vile kwa bahati mbaya.

Huyu rafiki yangu mpya nae ambaye tulipanga kufunga ndoa nitakaporudi nae amepata safari ya kwenda nje kulinda amani kwani yeye ni Mwanajeshi na tangu alipopata taarifa hizo za safari hajagusia tena nia yake ya kunivisha pete ya uchumba, hadi sasa nashindwa kujua la kufanya, sina uhakika kama huyu mpya anania ya kweli nami au nirudiane na yule wa zamani ambaye kwa watu wa karibu wananiambia kuwa bado wanaendelea na yule rafiki yangu.

Naombeni ushauri wenu ndugu yangu na wachangiaji wengine kwani nimechanganyikiwa. Watinga"

Dinah anasema:Tubarikiwe wote Watinga, asante sana kwa ushirikiano wako. Huyo baba mtoto wako hafai kabisa na futa wazo la kurudiana nae kwani hakukuheshimu na wala hakukuthamini sio tu kama mpenzi wake bali mama wa mtoto wake na akakutenda na rafiki yako.


Kama ulivyosema mwenyewe alipogundua kuwa umejua uchafuzi wake bado hakuonyesha kujutia makosa yake, hakuomba msamaha na badala yake alionyesha kiburi. Mimi binafsi naamini kuwa kama mtu anakupenda kwa dhati kamwe hawezi kukuumiza na ikitokea mnashindwa kuelewana kwa sababu zozote zile na mmoja wenu kutaka kuondoka.


Lazima mtu huyo (mkosaji) atapigania penzi lake kwa kuomba msamaha, kujutia makosa na kuahidi na kuhakikisha anabadilisha mwenendo wake na ikibidi kuwekeana "sheria" hasa kama wewe ulietendwa unataka kuendelea na uhusiano. Uamuzi uliochukua ni wa busara hasa ukizingatia hamkuwa kwenye ndoa hivyo hakukuwa na suala la kupoteza muda kujiuliza shold i stay...should I go?


Siku hizi nasikia wanaume wa wetu wa Kibongo wanapenda sana kutumia wanawake kiuchumi, akijua tu umefanikiwa kimtindo au uko nje (as wanaamini kuwa Ulaya = kupata senti kiurahisi) basi Exes wengi hujaribu sana kujipendekeza kwa kujidai kuwa wanataka kuoa au kurudiana na wewe kwa vile wanauhakika ulikuwa unawapenda hivyo utakubali haraka kurudiana nao. Lakini ukweli ni kuwa hawana nia na wewe bali wanataka kukutumia nahuko waliko wanaendeleza mahusiano na wanawake wengine.


Muda uliochukua kupumzika (kuwa nje ya uhusiano) unatosha kabisa kwa wewe kuwa tayari kujaribu tena uhusiano wa kimapenzi japokuwa, lakini miezi mitatu ya kuwa kwenye uhusiano mpya ni mapema sana kwa wewe na yeye kupeleka uhusiano huo kwenye level ya juu ambayo ni uchumba kuelekea Ndoa.

Huyu Mpiganaji huenda anania njema sana tu na wewe lakini baada ya kutumwa kwenda kulinda amani huenda imeingilia mipango yake hasa ukizingatia kuwa wewe uko Ughaibuni. Kuna mawili-matatu huenda yalikuwa yanasumbua akili yake Moja ni kukuchumbua na yeye kupoteza maisha by doing that atakuwa amekuumiza sana kuliko akijifia bila kujicommit kwako kama mume wako wa baadae.

Pili huenda amepoteza ile hali ya kujiamini baada ya wewe kwenda Ughaibuni, amekuwa na wewe kwa muda mfupi sana hivyo ni rahisi kwako wewe kama mwanamke kubadilisha mawazo mara baada ya kukutana na wanaume wengine Makini huko Ulaya.


Kama unampenda kiukweli huyu Mwanajeshi basi mimi nakushauri uendeleze urafiki ambao ni a bit special kwa vile mnapendana kimapenzi hii itawasaidia sana wote wawili kujua nini mnataka out of uhusiano/urafiki wenu na Mungu akijaalia kila mtu akamaliza shughuli zake huko aliko na kurudi Nyumbani basi mtaungana na kuwa full time wapenzi na hata ndoa kama mtapenda iwe hivyo.

Hapo hakuna cha kuchanganyikiwa wala nini, ni uamuzi tu. Kama unataka keep urafiki na Mpiganaji au achana nae uanze upya pale utakapo kutana na mtu mwingine aliekua na kutulia kiakili.

Natumaini ushauri wa wachangiaji na nyiongeza ya maelezo yangu yatakuwa yamekusaidia kufanya uamuzi wa busara.

Kila lililo jema!

No comments:

Pages