Friday

Naogopa uhusiano mpya, nikizidiwa najichezea je kunamadhara?

"Habari zenu wakubwa kwa wadogo,
Mimi ni mwanamke umri wangu ni miaka 25 tatizo langu ni mimi nilikuwa na mume wangu ambaye tuliishi pamoja kwa miaka 4 na nilikuwa nikimpenda sana mume wangu lakini kutokana na kutokuwa mwaminifu kwangu na mateso aliyokuwa ananipa kwa sababu alijua wazi nampenda nilishindwa kuendelea kuvumilia na mwaka jana mwezi wa 4 tukaachana.


Mimi nikaanza maisha ya peke yangu basi sikuhitaji tena mwanaume kwani nilimpenda sana mume wangu na sikupenda kuachana naye ila tabia zilinichosha.Kama unavyojua binadamu huwezi ishi mwenyewe mwezi wa 7 nikapata mkaka mmoja ambaye mwanzo sikumpenda kabisa lakini baadae nikajikuta nimeingia kwenye mapenzi yake.

Tumedumu na huyu kaka kwa muda wa miezi 3 kumbe naye hakuwa mwaminifu, sasa tatizo langu kubwa ni hili; tangu niachane na huyu bwana'ngu nimekuwa muoga kuanzisha uhusiano mpya wa kimapenzi kwahiyo nipatapo hamu ya kufanya mapenzi huwa najilaza kitandani kajichezea kinena hadi najiasikia raha kama vile nakojoa.

Nimekuwa nikijifanyia hivyo kwa muda mrefu, je inamadhara gani? na je huku ni kujichua? maana najua kujichua kuna madhara nifanyaje jamani na kuanzisha mahusiano na mtu mwingine naogopa isije kuwa yale yale.

ASANTENI NASUBIRI MAWAZO YENU
TINA-MOROGORO"

Dinah anasema: Siku zote sio vema kukimbilia uhusiano mpya baada ya ndoa kuvunjika au hata kutoka kwenye uhusiado uliodumu kwa muda mrefu. Kihisia na kimapenzi unakuwa hauko tayari kujua kama unampenda mtu au unakubali kuwa na mtu kwa ajili ya comfort. Hii inajieleza wazi pale uliposema kuwa hukumpenda bwana'ko mwanzo lakini ukaendelea nae kwa muda wa miezi 3.

Kuchezea kinena huwezi kusikia raha yeyote (kinena ni eneo linaloota nywele/mavuzi) na dhani unamaanisha kisimi a.k.a kiharage hicho ndio pekee kitakachokufanya usikie raha. Kuna njia nyingi za kujichua/chezea.....tafuta topic ya kujichua kwa mwanamke.

Kujichua kwa mwanamke kiasili hakuna madhara yeyote, lakini kama unatumia au unajingizia vitu au vifaa Ukeni (Sanamu) zinaweza kukusababishia maaambukizo, "kutifua" misuli ya uke na kusababisha uke wako kulegea, nyama kujitokeza kwa nje.

Ukizoea kutumia Sanamu kujichua utashindwa kusikia utamu kila utakapofanya ngono na mwanaume kwa vile sanamu ni ngumu japokuwa watu watakudanganya kuwa ziko na texture kama uume asilia lakini sio kweli, Mungu aliumba uume kwa ajili ya kuingia ukeni na sio sanamu.

Mazoea hayo yatakufanya kihisia udhani kuwa mwanaume hana uwezo wa kukuridhisha kingono na hivyo kumuomba akufanye kwa kutumia sanamu badala ya uume wake kitu ambacho nitakiita "madhara ya kujichua kwa kutumia sanamu".

Kujichua kiasilia kunakusaidia wewe kama mwanamke kuujua mwili wako, kuongeza nguvu kingono na hali ya kupenda tendo (utakapokuwa tayari kwa ajili ya uhusiano mpya), kukaza misuli ya tumbo na kufanya kuwa na shape nzuri ya makalio......inategemea na mtindo wa kujichua unaotumia, sio lazima iwe kidole.

Kila la kheri!

No comments:

Pages