Monday

Kwanini wanaume mnapenda kuterekeza Familia zenu?

"Habari yako Dinah, pole na majukumu. Mimi ni mama wa miaka 40 sasa nina watoto 2 lakini nimetengana na mume wangu kwa miaka mitano sasa. Uniwie radhi kwa hii habari ni ndefu sana ila nataka kushare na wamama na wababa kwa ajili ya kile kinachotokea ktk maisha ya ndoa unapobainika udanganyifu kwa mmoja wapo.


Tumekuwa kwenye ndoa kwa miaka 11 mpaka nilipoamua kumuacha mume wangu January 2006, kwa muda wote tulioishi pamoja tulipitia maisha magumu na ya wastani na tulikuwa tunasaidiana sana. Nilikuwa nampenda mume wangu kwa dhati, akiwa hana kitu nilifanya kwa niaba yake na sikuona tatizo.

Mwaka 2002 mume alipunguzwa kazini na kwa maelezo yake hakulipwa hela ya maana, mimi nikaona sio tatizo nilikuwa na kipato cha kutuwezesha kuyamudu maisha ya familia yetu kwa furaha, hapo tayari nilikuwa nimenunua kiwanja maeneo ya Tegeta.


Mume alikuwa hayapendi maeneo hayo ya Tegeta hivyo hakujishughulisha hata kukiona hicho kiwanja. Muda mwingi mume wangu alikuwa anabaki nyumbani mimi nikiwa kazini. Hapo nyumbani tulikuwa na msaidiza wa kazi na watoto 2.

Wakati huo mtoto wetu mkubwa alikuwa anasoma darasa la 2 na mdogo alikuwa chekechea, nilikuwa na akiba niliokuwa naitunza kwa ajili ya kujenga lakini tukajadiliana tukaona bora tununue gari ili mume wangu awe na shughuli kwa kutumia hivyo gari. Mume wangu alitafuta gari nikalinunua na yeye akawa analitumua kama tax. Tatizo likaanzia hapo.

Naomba niwaambie hivi mimi ni mama mwaminifu ninamwamini Mungu katika kweli yote sikuwahi kumfikiria mume wangu vibaya au kama angaliweza kuwa na mwanamke mwingine au kutembea na house girl nilikuwa namwamini sana na nilikuwa bize sana nikidhani namsaidia mwenzangu kumbe wapi.


Gari lilianza kunionyesha mambo, mume akawa hataki kufanyia kazi akawa anazunguka nalo tu, asubuhi naulizwa hela ya mafuta, matengenezo mpaka nikajuta kununua hilo gari. Nikaamua kuwaambia ndugu zake waongee nae.


Walipoongea nae yeye akasema hawezi kuendesha taxi kama nataka ninunue fuso ndio atafanya kazi hiyo, hilo likaniwia gumu nikachukua gari nikampa dereva mwingine. Jamani! wakati mimi ninahangaika kutafuta pesa za matumizi na kusomesha watoto kumbe mwenzangu kaanzisha uhusiano na dada wa nyumbani ndio maana hata kazi hataki kufanya ila mimi nilikuwa sijui kinachoendelea.


Mwaka 2003 tulianza kujenga na yeye ndio alikuwa anasimamia ujenzi ila cha moto nilikiona, tunapanga bajeti ya site vizuri namkabidhi pesa akirudi jioni ana shoti laki 2 au laki inategemea na wingi wa pesa utakayompatia lazima apunguze materials bila sababu mpaka nikaanza kumchunguza.

Hapo tulikuwa tunaishi Kinondoni kumbe bila mimi kujua alikuwa kampangishia mwanamke chumba huko Gongo la Mboto. Tukaanza kukorofishana maana ukiweka hela ndani yeye kazichukua hata simu anabeba.

Alivyojua kuwa najua habari za huyo mwanamke akaanza kusema mimi nataka kumwacha kwasababu hana kazi, oh sababu unajenga na mambo mengi mabaya kwa kweli. Tulisuluhishwa lakini hakuwa tayari kuacha tabia ya wanawake wa nje na mimi nilimchukia sana kwa tabia zake ndicho kilichotutenganisha mimi na huyo mume wangu.

Tulipoamua kutengana aliniambia niondoke na watoto niliondoka nao na wanasoma vizuri tu kwani niliamua kuwapeleka Boarding School ili wasiadhirike na kutengana kwetu japokuwa wakirudi likizo Mume wangu anakuja kuwaona lakini hawasaidii kwa chochote hata chupi hawanunulii.

Kwa sasa anafanya kazi nzuri tu lakini hataki kuwasaidia watoto. Mwaka huu kabla watoto hawajarudi Shuleni waliniomba sana nimsamehe baba yao na nilifikiri sana nikawaita wazee na nikawaambia kuwa nimemsamehe kilichotushangaza ni kwamba yeye hajakubali kusamehewa anachotaka ni nyumba niandikwe kwa jina lake kwanza na gari ninalotumia nimpe au niliuze ndio atarudi.

Kwa masharti hayo mie nimesema basi na kila mtu aishi peke yake maana naona mwenzangu anawivu na nilichonacho ambacho kimsingi ni cha familia yetu, nimeogopa masharti yake maana anaweza kutufanya tuanze kupanga tena.

Kinamama ninachotaka kujua ni hiki; Kwa kina mama hivi waume zenu nao wakijua kuwa umejua anachokukosea na kutengana huwa wanawasusia familia?

..... na kina baba naomba kuwauliza mpaka lini mtawatesa wake zenu kwa kuwasusia familia zenu?

Samahani sana Dinah usilitoe jina langu.
Nina hasira sana na wanaume na ninawachukia kwa kweli."

Dinah anasema: Asante sana kwa maelezo yako uliyoyapangilia vema kabisa. Maelezo ambayo hakika yanatia Moyo wote waliopatwa na matatizo ya kindoa, Inaonyesha kuwa hata sisi wanawake tunaweza kusimama Imara na kuhakikisha watoto wanapata maisha bora hata kama baba yao hataki kusaidia.


Hongera sana kwa kutumia muda wako mwingi kuhakikisha kuwa familia inaendelea kula na kuishi mahali bila usumbufu wowote, lakini kujituma kwako kumezaa tatizo lingine ambao ni hali ya kutokujiamini kwa mumeo.

Mwanaume yeyote hapendi kulishwa na mwanamke, kwa maana ya kuwa na mwanamke mwenye nguvu kiuchumi. Huyu mwanaume atahisi kuwa unamdharau hata kamahufanyi hivyo bado atadhani kuwa unamdharau kwa vile tu hana kazi au hata kitu.

Mwanaume huyu atatafuta namna nyingine ili ku-gain ile hali ya yeye " kuheshimika" nakuwa in control na ndipo sasa anakwenda kuanzisha uhusiano na mwanamke mwingine na ili kurudisha hali ya kujiamini na nguvu as a man akatumia pesa za kujengea nyumba kuhonga, akatumia gari kufanyia shughuli zake nyingine na sio kazi ya kubeba abiria.....hii yote ilikuwa inamfanya ahisi kuwa bado ni MWANAUME out there!


Lakini kitu ambacho wanaume sio tu mumeo ni wote, huwa wanakisahau au hawajali ni kuwa unapoamua kufanya uchafu nje na kuharibu ndoa yako atakae umia sio Mkeo bali ni watoto ambao hakika hawana hatia na hawakuomba kuzaliwa na nanyi bali uamuzi wenu ndio umesababisha uwepo wao hapa Duniani.


Ndoto ya Mtoto yeyote Duniani ni kuwaona baba na mama yake wako pamoja, na mtoto huyo hatopenda kuona mtu mwingine anaingilia uhusiano wa baba na mama yake. Inasikitisha unaposhuhudia watoto wanatamani ndoto hiyo itimie lakini mzazi mmoja anaendelea kuwa mbinafsi na kutokujali matakwa, hisia na haki ya watoto hao.


Mumeo hapendezwi na maendeleo yako kiuchumu na anahisi kuwa humueshimu tena kwa vile alikuwa hana kitu napengine hata aliwahi kudhani kuwa kuna mwanaume mwingine anakupa hizo pesa za kujenga nakufanya mambo mengine ya kifamilia na kimaendeleo.....wanaume wengine ni wanadhana potofu sana, wanadhani mwanamke huwezi kufanikiwa kimaendeleo unless kuna mtu unamtumia.

Yeye kutaka Gari iuzwe na Nyumba iandikwe jina lake ni wazi anataka ku-gain power au control kama mwanaume. Hakuna dalili za yeye kutaka kuendeleza penzi ili kuwa na maisha bora kama familia.

Kama unahisia za kimapenzi juu yake, kwamba bado unampenda na yeye anakupenda na ungependa ndoa yenu ifufuliwe then ni vema wote wawili kushirikiana na kupata ushauri wa kitaalamu zaidi na baada ya hapo mali zote ziandikwe majina ya watoto kama alivyogusia mmoja wa Wachangiaji nami nitaongeza maelezo yangu kwenye hili kama utakuwa tayari.


Lakini kama unataka kurudiana na Mumeo kwa vile tu watoto wanataka kuwa na baba yao karibu then nakushauri utafute Mwanasheria wa masuala ya ndoa (unaweza tu kwenda Mahakamani ukaeleza nia yako na wao watakupa ushauri wa nini cha kufanya) ili kumtaliki mumeo Kisheria ili asije kukupa matatizo baadae, pia Talaka itakusaia wewe kuwa huru na kuendeleza maisha yako.

Nikijibu swali lako kama mwanamke: Inategemea na asili ya Mwanaume, mazingira aliyokulia, uzoefu wake, maisha ya wazazi wake n.k., ila wanaume wa Kibongo kuterekeza familia zo ni kawaida sijui wamerogwa?

Hata kama baba yako alikuwa mchafuzi au alimterekeza mama yako haina maana kuwa na wewe "urithi" hayo, jitahidi na uwe tofauti, kuwa baba bora kuliko alivyokuwa baba yako. Muonyeshe baba yako kuwa alichokifanya sio Uanaume ni upumbavu na wewe ni mwanaume na unafanya kinyume kabisa na lichokifana.

Wanaume wa kibongo wenye t abia ya kuterekeza Familia zetu kwa sababu ya Vimada mnatakiwa ku-MAM UP!

Ninyi wanawake (Vimada) kama unajua kabisa jamaa anafamilia yake kwanini ukubali aiterekeze? Kwanini unakubali mwanamke mwenzio ateseke? Hebu fikiria ingekuwa ndio wewe umeterekezwa ungejisikiaje?

Wanawake wote mnaopenda kunyatia/kubali waume za watu mnatakuwa ku-WOMAN UP nakujifunza kusema "SITAKI kuharibu maisha ya watoto wako"....utakuwa umesaidia watoto hao kuendelea kuwa na wazazi wao wote wawili. Jifunzeni kujitegemea na kuendesha maisha yenu bila kutegemea kubebwa na wanaume wa watu.

Dada tafadhali kama utaamua kuendelea na ndoa kwa vile bado mnapendana basi hakikisha afya yake ni safi na unasimamia hapo kwenye mali kuwa ni za watoto, vinginevyo atakumsikinisha (kukufanya uwe masikini) huyo mwanaume.


Kila la kheri mwanamke wa Shoka!

No comments:

Pages