Wednesday

Nahisi Mtumwa ndani ya ndoa yangu!-Ushauri

"MAMBO DADA DINAH,
POLE NA MAJUKUMU YA HAPA NA PALE PALE. NAOMBA SANA MY DIA UNISHAURI MAANA NIKO NJIA PANDA. JAMANI MWENZENU MIE NIMECHOKA SANA NA MAISHA YA KUKWARUZANA NA KUPIGIANA KELELE KILA WAKATI NA MUME WANGU.

MUME WANGU NI MTU ANAEPENDA KULAUMU SANA NA KITU KIDOGO KIKITOKEA KINAKUZWA KINAKUA KIKUBWA HASA, HATA UKIOMBA MSAMAHA HAELEWI. IMAGINE MIMI NAFANYA KAZI ARUSHA NA NINAISHI MOSHI KILA SIKU ANATAKA NIWE NAENDA NA KURUDI KWAVILE NAMPENDA NIKAKUBALI INGAWA NACHOKA SANA.


MARA NYINGI NAFIKA USIKU KWENYE SAA MOJA AU MBILI USIKU NA NINAKUA NIMECHOKA KWELI, WAKATI MWINGINE HATA MUDA WA KUANGALIA MAZINGIRA YA NYUMBANI SINA.

BASI AKIKUTA HATA GLASS ALIOACHA ASUBUHI CHUMBANI ATAONGEA MANENO MENGI SANA MARA OOH "WEE MWANAMKE HUJUI WAJIBU WAKO" UKIMWOMBA MSAMAHA BADO ATANUNUA.

KWA KWELI MIMI SIMUELI, KWA KIFUPI YEYE ALISHAISHI NAWANAWAKE WAWILI TOFAUTI MMOJA KWA MIAKA 4NA MWINGINE KWA MIAKA 10 ANAWATOTO 4 LAKINI WALISHINDANA NA HAWAKUFUNGA NDOA MIMI NDIO NILIEFUNGA NAE NDOA NA TUNAISHI NA MTOTO MMOJA WA KWAKWE.

YAANI HATAKI MTOTO AULIZWE KITU AGOMBESHWE ANAONA KAMA VILE ANAONEWA YAANI MIMI SIJABAHATIKA KUPATA MTOTO NA MUME WANGU HUYU INGAWA NINA MTOTO MMOJA KUTOKA UHUSIANO WANGU WA AWALI.

MATUMIZI NDANI YA NYUMBA KUTOA NI KWA SHIDA SHIDA UKIMWAMBIA AACHE HELA YA CHAKULA MARA ASEME AMESAHAU UKIMPA LIST YA VITU VYA KUNUNUA BADO ATADAI KASAHAU.

ANANICHOSHA KWAKWELI, WAKATI MWINGINE NAAUMUA KUFANYA MWENYEWE TU KUEPUKA KERO HANIHUDUMII CHOCHOTE KAMA MKEWE, NIFANYAJE JAMANI NA HUYU BABA?

MIMI NA MIAKA 29 YEYE ANAMIAKA 42 LAKINI VITUKO NAVYOFANYIWA NAHISI KAMA MTUMWA, MARA AJITENGE NA MWANAE YAANI KILA NALOFANYA ALIONI YEYE NI KULALAMIKA TU.

JAMANI EMBU NIAMBIENI KOSA LANGU NINI NA NIFANYAJE? SAMAHANINI KWA KUWACHOSHA ILA NILITAKA MPATE PICHA HALISI."

Dinah anasema: Mambo ni mazuri tu mdada, namshukuru Mungu. Shukrani kwa ushirikiano wako. Mumeo ni Mbahili/mchoyo, mlalamishi, mkorofi, hana huruma, hakuthamini, mvivu, sio mwelevu, hajali na mbinafsi hizi ni baadhi tu ya tabia ambazo mtu yeyote alie na akili timamu hawezi kuzivumilia.

Yaani unasafiri kutoka Mji mmoja kwenda mwingine kila siku na bado anakusimanga kuwa hujui wajibu wako? Wala sikulaumu kwa kuchoka mdogo wangu.

Huyu mwanaume anasumbuliwa na "mfumo" dume uliochanganyika na hali ya kutokujiamini kwa vile wewe ni mdada unaejitegemea kiuchumi, pia inawezekana ameathirika kisaikolojia kutokana na uhusiano wake na wanawake Mf mama yake, mama wa kambo, bibi, wapenzi wa awali n.k. Hali hiyo ndio iliyomsukuma kukulazimisha wewe kusafiri kila siku kutoka Arusha kwenda Moshi kwa kufanya hivyo anahisi kuwa ana-control juu yako wewe kama mwanamke.


Nijuavyo mimi maisha ya ndoa ya siku hizi ni kusaidiana sio kwa vile tu mwanamke unauwezo wa kiuchumi sawa au zaidi ya mumeo basi ndio iwe sababu ya kuchukua majukumu yote kuanzia ujenzi wa nyumba/kodi mpaka shughuli za nyumbani....ni sawa na kuwa single mama mwenye watoto na mume.

Hakika unampenda mumeo lakini vilevile unamuogopa, kwa sababu hata kama unampenda mtu huwezi kukubali kufanya kitu ambacho unajua wazi kitahatarisha afya na maisha yako, pamoja na kuwa unampenda unatakiwa kujiamini pia kuwa na msimamo na kumpa challenges mumeo sio kila akisema wewe ni "ndio bwana"......"nisamehe mume wangu" hata kama kosa ni lake!


Tabia za mumeo zinaweza kubadilika ikiwa wewe mwenyewe utasimama imara na kutaka mabadiliko, akijua wazi kuwa anayofanya ni makosa na ukampa nafasi ya kujirekebisha atafanya hivyo hasa kama anakupenda na anataka ndoa yenu iendelee. Lakini kabla ya kumtaka abadilike unatakakiwa kujua historia ya maisha yake.


MF; Kama mumeo aliwahi kuishi na mama wa kambo na mama huyo wa kambo kwa namna moja au nyingine alikuwa akimnyanyasa yeye kama mtoto pia mama huyo wa kambo alikuwa akimtawala baba yake (baba mkwe wako) then itakuwa imejiweka wazi kuwa Mumeo anakuwa na tabia hiyo kama sehemu ya kujilinda dhidi ya "mwanamke" kwa kifupi atakuwa ameathirika kisaikolojia.

Na suala la kujitenga na mtoto wake pia linaashiria "maumivu yake ya kisaikolojia" kwa vile wewe sio mama wa mtoto huyo anadhani kuwa utamfanyia vile alivyofanyiwa yeye na mama wa kambo, hivyo chochote utakachokifanya kwa vile tu wewe sio mama mzazi basi inaonekana ni uonevu hata kama unafanya hivyo kumsaidia au kumkanya mtoto.


Nini cha kufanya: Chukua likizo ya uhusiano, nenda kwa wazazi/ndugu ukatulize akili kwa siku mbili-tatu au hata wiki mbili. Utakaporudi utakuwa tayari kujaribu na kuweka mambo sawa ili ndoa yenu iendelee au kuimaliza.

Sasa, kwa vile wewe ni mdogo kwa mumeo (kibongo bongo huna nguvu) itakuwa ngumu kusikilizwa, hivyo jaribu kutumia watu wazima (wazee) unaowafahamu nakuwaamini, itakuwa vema kama watakuwa wale waliowafungisha ndoa.

Hawa watawapa ushauri na kuwapatanisha ninyi kama pea ili muishi kwa amani na upendo kiimani zaidi na sio kivitendo kwa maana kuwa maelezo yao hayatomfanya mumeo kubadilika kwa vitendo lakini itatoa nafasi kwako wewe kama mwanamke mdogo (kwa mumeo) kuweza kuwakilisha hoja zako za kutaka mabadiliko kirahisi.

Zungumza na mumeo kwa uwazi, weka hisia zako zote ili ajue kuwa anayokufanyia yanakuumiza na yanakusukuma nje ya ndoa yenu kitu ambacho wewe usingependa kitokee. Mwambie ni jinsi gani unampenda, unamheshimu na kumthamini.

Weka wazi hisia zako kwa mtoto wake, kwamba huna nia mbaya na unamjali kama unavyomjali mtoto wako.....kama historia yake inahusisha mateso ya mama wa kambo, itakubidi umhakikishie kuwa wewe sio kama wanawake wengine wenye roho mbaya.

Sema, kamwe hutomtesa wala kumnyanyasa mtoto wake, utamsaidia kila atakapohitaji msaada wako, utamfunza ili awe mtoto mwema na mwenye adabu kama unavyofanya kwa mtoto uliemzaa. Hutombagua wala kumnyanyapaa.

Mueleze ni kiasi gani unachoka kusafiri kutoka mkoa hadi mkoa kila siku, na kwa pamoja mtafute njia ya kuodoa kero hiyo (sio kuacha kazi tafadhali), ni mmoja wenu kuomba uhamisho ili kumfuata mwenzie.

Zamani kisheria ilikuwa mwanamke anamfuata mume siku hizi hata mume anaweza kumfuata mke, angalieni nani kazi yake inalipa zaidi na hivyo mmoja wenu kutafuta kazi nyingine huko ambako mwenzie analipwa vizuri zaidi (kamwe usikubali kuacha kazi) hata akikupa choice kazi au yeye, mama chagua kazi kwani wee bado mdogo na kumbuka unajukumu lingine hapo ambalo ni mtoto wako kutoka uhusiano wa awali.

Acha uzembe wa kukubali kila anachokisema mumeo, mpe challenges, pia sahau suala la kuomba misahama isiokuwa na sababu, omba masamaha pale tu unapojua kuwa umemkosea.

Ukifanikiwa hapa, njoo tena ili nikupe mbinu za kumfanya ajifuze kukusaidia shughuli za ndani unapokuwa kazini......ukimjulia mwanaume vijishughuli vya ndani sio deal sana kwake, sema tu sisi wanawake huwa tunawazoesha vibaya hawa wanaume ktk harakati za kuwakosa ili watangaze ndoa.

Mara wanapofunga ndoa nasi tunagundua kuwa hatuwezi kufanya yote, kazi Ofisini, kazi za nyumbani, kupika, kuwa mbunifu ili kumridhisha kingono, kuweka vionjo ili mapenzi yasifubae, kuangalia, watoto n.k Jamani eeh maisha ya sasa ni Tofauti, mwanamke huwezi kufanya yote hayo peke yako!

Natumaini wachangiaji na maelezo yangu yatasaidia kwa kiasi fulani ktk kufanya uamuzi,
Kila la kheri!

No comments:

Pages