Thursday

hivi kusamehe ni ugonjwa? kila akicheat mie nasamehe tu-Ushauri


"Pole na kazi dada dinah,
mimi ni mwanamke wa umri wa kati nina boyfriend wangu ambaye hadi sasa tuna kama miaka 2 na nusu. Nilikutana nae wakati yupo mwaka wa mwisho Chuoni. Wakati huo mimi nilikuwa nimeshaanza kazi.

Nilimvumilia hadi akamaliza Chuo na kufanikiwa kupata kazi Benki akapangiwa kituo cha kazi Wilayani hapa hapa kwenye Mkoa huu tunaoishi. Wakati nakutana na huyu bwana alikuwa ndio ametoka kuachana na demu wake wa chuo, ila kipindi hicho pia niligundua kuwa ana demu mwingine ambaye alikuwa anasoma Chuo mkoani Arusha.

Nilipomuuliza inakuwaje akaniambia huyo mtu ni kama wameachana kwani kwa umbali waliokuwa nao asingeweza kuwa nae tena na ndio maana alikuwa na mahusiano na yule demu wa chuo, Basi nikaamua tu kuendelea nae nikijua atakuja kubadilika kwani tangu mwanzo nilihisi jamaa yangu ana utulivu.

Matatizo yalianza wakati alipoitwa kwenye interview ya kazi, kumbe kule alipoenda alikutana na msichana aliewahi kuwa nae kipindi wanasoma. Kwa maelezo yake ya awali aliwahi kuniambia kuwa yule dada ndie msichana ambae alimpenda sana kuliko wasichana wote aliowahi kuwa nao ila walipotezana.

Sasa aliporudi tu nikagundua mabadiliko kwa mtu wangu, kwanza kwenye simu yake alikuwa ameweka jina langu lakini nikakuta kaweka jina la kwanza la huyo dada, pili nikakuta msg za mapenzi akimwambia huyo dada kuwa yeye ndio mkewe aliepangiwa na mambo mengine yanayoumiza sana moyo.

Mbaya zaidi mimi mwenyewe hajawahi kuniambia maneno kama hayo tangu nimfahamu, basi nikamuuliza kwasababu jina nililolikuta ni kama la mtu yule ambaye alishaniambia je ni yeye ndie amekutana nae huko kwenye interview?

Akaniambia hapana ila huyo ni mtu mwingine ambaye amemkuta hiyo sehemu anafanya kazi Benki na akaomba msamaha kuwa ni bahati mbaya na hatarudia tena. Siku ya mwaka mpya wa kuingia mwaka 2009 tulibadilishana line kwa bahati mbaya. Ya kwake aliiweka kwenye handset yangu basi wakati tupo kwenye mkesha mida kama ya saa 5 nusu hivi.

Nikapigiwa simu na mdada sasa kwa kuwa nilisahau kama line iliyokuwepo haikuwa ya kwangu, nikapokea huyo dada akaniambia anaomba kuongea na mwenye simu, nikmjibu anti simu ni yangu akan'gan'gania nimpe mwenye simu.

Nikakumbuka nikampa simu huyo boyfriend wangu, akaangalia tu no akakata simu alafu akaitoa line na kuitupa simu yangu kwenye moto. Ukweli kile kitu mmii kiliniboa sana nikaamua kuondoka kurudi nyumbani.

Kesho yake akaniomba msamaha na kuahidi kuninunulia smu nyingine, pia ndio akaniambia ukweli kuwa yule dada aliepiga simu ni yule mwanamke wake wa zamani na ndiye aliekutana nae kwenye intrview. Nikamuuliza sasa itakuwaje?akaniambia kuwa yale yalishapita na hawezi kuniacha kwani ananipenda sana.

Nikamuuliza tena nitaamini vipi asemayo? akampigia simu yule dada mbele yangu na kumwambia kuwa hawezi kuwa nae tena ana mtu mwingine hivyo huyo dada aendelee tu na maisha yake.

Nikasahau kabisa dada dinah kuhusu huyo dada na kufungua ukurasa mpya na mpenzi wangu, Ikaja kipindi cha valentine mwaka huo huo, tulikuwa Dar basi huyo dada akapiga simu usiku wa saa kumi wakati bado tulikuwa tumelala, nikaamka na nikapokea mimi akanijibu kwa jeuri kubwa kuwa kwa nini napokea simu zisizonihusu?

Nikamwamsha boyfried wangu kama mara ya kwanza akakata simu, tukagombana sana siku hiyo akasema anamshangaa huyo dada kwa nini bado anamfuata wakati yeye hampendi! basi akanidanganya nikajikuta nimemsamehe dada dinha.

Sasa kilichonifanya niombe ushauri kwa wadau ni hiki,ulipofika mwezi wa 7 nikapata ujauzito nikamwambia mwenzangu inakuwaje mimi naona wakati wa kufunga ndoa umeshafika kwani sitaki kuzaa nje ya ndoa.

Huwezi kuamini alikataa eti yeye hayuko tayari kwa ndoa hivyo mimi nizae tu na yeye atalea mtoto ndoa bado sana, nikamwambia naona sitaweza kuendelea kufanya mapenzi na yeye tena kwani hayupo tayari na mimba nitatoa siwezi kuzaa nje ya ndoa tena hasa ukizingatia siku za nyuma nilishazaa nyumbani wazazi wangu watanielewaje?

Basi tukawa na ugomvi mkubwa kwa kweli na sikwenda kumtembelea tena kama kwa miezi 2 hivi na hata mawasiliano yakawa hafifu sana. Sasa nahisi kipindi hicho ndio alikitumia kufufua tena mahusiano na yule dada.

Siku moja nikatumiwa msg na rafiki yangu kuwa anamuona mtu wangu na mwanamke nyumbani kwake je nimeachana nae?kama naweza niende nikahakikishe mwenyewe! Kweli nikapanda gari nikaenda nikamkuta huyo dada nyumbani kwake, sikumuliza kitu huyo dada nikamfuata huyo bwana ofisini kwake nikamuuliza akanijibu kuwa yule ndio yule dada niliekuwa namsikia mwanzo.

Nikamwambia vipi kuhusu mimi? akanijibu kuwa yeye hajui na majibu mengine ya kifedhuli tu, siku hiyo nililala guest da dinah,baada ya hapo alikuja nyubani kuniomba msamaha nikaamua kumsamehe, ila tatizo ni kwamba amekuwa sio mwaminifu kwani siku ya valentine nilimkuta tena na mtu mwingine akimlalamikia kuwa hamuelewi bora aachane nae kwani haoni faida ya kuwa nae.

Nikamuuliza ila majibu yake bado hayaeleweki na hataki kabisa tuachane, naomba ushauri kwa wadu nifanyeje?

Dinah anasema: Pole sana kwa usumbufu unaoupata Mdada, maelezo yako yanafanana sana na ya Binti mmoja wa Kikoloni nilikuwa na-share nae nyumba nilipokuwa Chuoni. Binti alikuwa na Bf ambae alikuwa anamtreat kama unavyofanyiwa wewe. Wakati mwingine wanawake aliolala nao jana yake wanampigia simu yule Binti (my housemate) nakuwambia kuwa walichokifanya na jamaa, binti anakuja kwangu na kulia.

Lakini kila nikimpa ushauri wa kuweka miguu yake chini na kumpa ukweli jamaa, binti anaomba kuonana na jamaa, ile njemba imefika tu inaanza kumfokea, wanagombana wee kisha wanaishia kufanya ngono as unasikia kukurukakara zao huko chumbani.....akitoka hapo naenda kuchovya kwingine....kesho yake binti anasamehe.

Nikachoka kuliliwa nikaamua kumwambia ukweli kuwa, jamaa yako anajua kuwa wewe unampenda kwa dhati na anauhakika wa kusamehewa kwa makosa na uchafu wake wowote atakaoufanya, kitu ambacho mwanamke mwingine yeyote hawezi kufanya. Ili kumuonyesha kuwa unathamani kubwa kuliko anavyodhania mtose bila kumwambia.

Nikamwambia kuanzia sasa mchunie, badili mawasiliano, badili kitasa cha mlango, anza kujichanganya na watu wengine, ndugu,jamaa na marafiki yaani keep busy na maisha yako......... Hivi ndivyo nitakavyo kuambia na wewe Binti mrembo.

Mwanaume akikutenda kwa kuwa na wanawake wengine kabla hamajafunga ndoa na ukamsamehe ni wazi ataendelea kufanya hivyo akijua atasamehewa tena na tena, sasa unachotakiwa kufanya hapa ni kutoka Nduki (achana nae) kabla hujapewa HIV.

Huyu mwanaume hakuthamini, hakupendi, hakuheshimu na hana mpango wowote wa kuishi na wewe maishani mwake, Mshukuru Mungu kuwa aliweka wazi hilo mapema pale uliposhika mimba, katika hali halisi siku hiyo ndio ilitakiwa kuwa mwisho wa uhusiano wenu.

Hataki muachane sio kwa kuwa anakupenda.....ni kwasababu anajua wazi hakuna mwanamke yeyote hapa Duniani ambae anaweza kusamehe unayomsamehe wewe, uko hapo ili kutumiwa kama back up! na si vinginevyo. Mpe buti la meno huyo hakufai kabisa.

Wachangiaji wamesema mengi mazuri na haya yangu kwa namna moja au nyingine yatasaidia kum-buti huyo looser!
Kila la kheri.

No comments:

Pages